< Mark 6 >
1 And He went forth from there, and came to His own country, and His disciples follow Him,
Na akaondoka hapo na kwenda mjini kwao, na wanafunzi wake wakamfuata.
2 and Sabbath having come, He began to teach in the synagogue, and many hearing were astonished, saying, “From where [did] this One [hear] these things? And what [is] the wisdom that was given to Him, that also such mighty works are done through His hands?
Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika Sinagogi. Watu wengi walimsikia na wakashangazwa. Wakasema, “Amepata wapi mafundisho haya?” “Ni hekima gani hii aliyopewa?” “Anatendaje miujiza hii kwa mikono yake?”
3 Is this not the carpenter, the Son of Mary, and brother of James, and Joses, and Judas, and Simon? And are His sisters not here with us?” And they were being stumbled at Him.
“Je huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simioni? Je dada zake si wanaishi papa hapa pamoja nasi?” Na hawakufurahishwa na Yesu.
4 And Jesus said to them, “A prophet is not without honor, except in his own country, and among his relatives, and in his own house”;
Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika mji wake na miongoni mwa ndugu zake na nyumbani mwake.”
5 and He was not able to do any mighty work there, except having put hands on a few sick, He healed [them];
Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache akawaponya.
6 and He wondered because of their unbelief. And He was going around the villages, in a circle, teaching,
Alishangazwa sana kwa sababu ya kutokuamini kwao. Kisha alivitembelea vijiji vya jirani akifundisha.
7 and He calls near the Twelve, and He began to send them forth two by two, and He was giving them power over the unclean spirits,
Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili akaanza kuwatuma wawili wawili. Aliwapa mamlaka juu ya pepo wachafu,
8 and He commanded them that they may take nothing for the way, except a staff only—no leather pouch, no bread, no brass in the girdle,
na kuwaamuru wasichukue chochote wanapokwenda isipokuwa fimbo tu. Wasichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni;
9 but having been shod with sandals, and you may not put on two coats.
lakini wavae viatu, na siyo kanzu mbili.
10 And He said to them, “Whenever you may enter into a house, remain there until you may depart from there,
Na akawaambia, “Nyumba yoyote mtakayoingia, kaeni hapo mpaka mtakapoondoka.
11 and as many as may not receive you nor hear you, going out from there, shake off the dust that is under your feet for a testimony to them; [[truly I say to you, it will be more tolerable for Sodom or Gomorrah in [the] day of judgment than for that city.”]]
Na mji wowote usipowapokea wala kuwasikiliza, ondokeni kwao, kung'uteni mavumbi ya miguu yenu, iwe ushuhuda kwao.”
12 And having gone forth they were preaching that [men] might convert,
Nao wakaenda wakitangaza watu watubu na kuacha dhambi zao.
13 and they were casting out many demons, and they were anointing many sick with oil, and they were healing [them].
Waliwafukuza pepo wengi, na waliwapaka mafuta wagonjwa na wakaponywa.
14 And King Herod heard (for His Name became public), and he said, “John the Immerser was raised out of the dead, and because of this the mighty powers are working in him.”
Mfalme Herode aliposikia hayo, kwa kuwa jina la Yesu lilikuwa limejulikana sana. Baadhi walisema, “Yohana mbatizaji amefufuka na kwa sababu hiyo, hii nguvu ya miujiza inafanya kazi ndani yake.”
15 Others said, “It is Elijah,” and others said, “It is a prophet, or as one of the prophets.”
Baadhi yao wakasema, “Huyu ni Eliya,” Bado wengine wakasema, “Huyu ni nabii, kama mmoja wa wale manabii wa zamani.”
16 And Herod having heard, said, “He whom I beheaded—John—this is he; he was raised out of the dead.”
Lakini Herode aliposikia haya akasema, “Yohana, niliyemkata kichwa amefufuliwa.”
17 For Herod himself, having sent forth, laid hold on John, and bound him in the prison, because of Herodias, the wife of his brother Philip, because he married her,
Maana Herode mwenyewe aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani kwa sababu ya Herodia (mke wa kaka yake Filipo) kwa sababu yeye alikuwa amemuoa.
18 for John said to Herod, “It is not lawful for you to have the wife of your brother”;
Kwa maana Yohana alimwambia Herode, “Si halali kumuoa mke wa kaka yako.”
19 and Herodias was having a quarrel with him, and was willing to kill him, and was not able,
Lakini Herodia alianza kumchukia na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza,
20 for Herod was fearing John, knowing him [to be] a righteous and holy man, and was keeping watch over him, and having heard him, was doing many things, and hearing him gladly.
maana Herode alimwogopa Yohana; alijua kwamba ni mwenye haki mtu mtakatifu, na alimwacha salama. Na alipoendelea kumsikiliza alihuzunika sana, lakini alifurahi kumsikiliza.
21 And a seasonable day having come when Herod on his birthday was making a banquet to his great men, and to the chiefs of thousands, and to the first men of Galilee,
Hata ilipofika wakati mwafaka ikiwa imekaribia siku ya kuzaliwa Herode akawaandalia moafisa wake karamu, na makamanda, na viongozi wa Galilaya.
22 and the daughter of that Herodias having come in, and having danced, and having pleased Herod and those dining with him, the king said to the girl, “Ask of me whatever you will, and I will give to you,”
Ndipo binti wa Herodia akaingia na kucheza mbele yao, akamfurahisha Herode na wageni walioketi wakati wa chakula cha jioni. Ndipo mfalme akamwambia binti, “Niombe chochote unachotaka nami nitakupa.”
23 and he swore to her, “Whatever you may ask me, I will give to you—to the half of my kingdom.”
Akamwapia na kusema, chochote utakachoniomba, nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.”
24 And she, having gone forth, said to her mother, “What will I ask for myself?” And she said, “The head of John the Immerser”;
Akatoka nje akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Akasema, “Kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
25 and having come in immediately with haste to the king, she asked, saying, “I will that you may immediately give me the head of John the Immerser on a plate.”
Na mara moja akaingia kwa mfalme akaanza kusema, “Nataka unipatie ndani ya sahani, kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
26 And the king, made very sorrowful because of the oaths and of those reclining with him, would not put her away,
Mfalme alisikitishwa sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake na kwa ajili ya wageni, hakuweza kumkatalia ombi lake.
27 and immediately the king having sent a guardsman, commanded his head to be brought,
Hivyo, mfalme akatuma askari kati ya walinzi wake na kuwaagiza kwenda kumletea kichwa cha Yohana. Mlinzi alikwenda kumkata kichwa akiwa kifungoni.
28 and he having gone, beheaded him in the prison, and brought his head on a plate, and gave it to the girl, and the girl gave it to her mother;
Akakileta kichwa chake kwenye sahani na kumpatia binti, na binti akampa mama yake.
29 and having heard, his disciples came and took up his corpse, and laid it in the tomb.
Na wanafunzi wake waliposikia hayo, walikwenda kuuchukua mwili wake wakaenda kuuzika kaburini.
30 And the apostles are gathered together to Jesus, and they told Him all, and how many things they did, and how many things they taught,
Na mitume, walikusanyika pamoja mbele ya Yesu, wakamweleza yote waliyofanya na waliyoyafundisha.
31 and He said to them, “Come yourselves apart to a desolate place, and rest a little,” for those coming and those going were many, and not even to eat had they opportunity,
Naye akawaambia, “Njooni wenyewe mahali pa faragha na tupumzike kwa muda.” Watu wengi walikuwa wanakuja na kuondoka, hata hawakupata nafasi ya kula.
32 and they went away to a desolate place, in the boat, by themselves.
Hivyo wakapanda mashua wakaenda mahali pa faragha peke yao.
33 And the multitudes saw them going away, and many recognized Him, and they ran there by land from all the cities, and went before them, and came together to Him,
Lakini waliwaona wakiondoka na wengi wakawatambua, kwa pamoja walikimbia kwa miguu kutoka miji yote, nao wakafika kabla yao.
34 and having come forth, Jesus saw a great multitude, and was moved with compassion on them, that they were as sheep not having a shepherd, and He began to teach many things.
Walipofika pwani, aliona umati mkubwa na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.
35 And now the hour being advanced, His disciples having come near to Him, say, “The place is desolate, and the hour is now advanced,
Muda ulipoendelea sana, wanafunzi wakamjia wakamwambia,”Hapa ni mahali pa faragha na muda umeendelea.
36 let them away, that having gone away into the surrounding fields and villages, they may buy loaves for themselves, for they do not have what they may eat.”
Uwaage waende miji ya jirani na vijiji ili wakajinunulie chakula.”
37 And He answering said to them, “You give them to eat,” and they say to Him, “Having gone away, may we buy two hundred denarii worth of loaves, and give to them to eat?”
Lakini akawajibu akisema, “Wapeni ninyi chakula.” Wakamwambia, “Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa wale?”
38 And He says to them, “How many loaves do you have? Go and see”; and having known, they say, “Five, and two fishes.”
Akawambia,” Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie.” walipopata wakamwambia, “Mikate mitano na samaki wawili.”
39 And He commanded them to make all recline in companies on the green grass,
Akawaamuru watu waketi katika makundi juu ya majani mabichi.
40 and they sat down in squares, by hundreds, and by fifties.
Wakawaketisha katika makundi; makundi ya mamia kwa hamsini.
41 And having taken the five loaves and the two fishes, having looked up to the sky, He blessed, and broke the loaves, and was giving [them] to His disciples, that they may set [them] before them, and the two fishes He divided to all,
Kisha akachukua mikate mitano na samaki wawili, na kutazama mbinguni, akaibariki kisha akawapa wanafunzi waweke mbele ya umati. Na kisha aligawa samaki wawili kwa watu wote.
42 and they all ate, and were filled,
Walikula wote hadi wakatosheka.
43 and they took up of broken pieces twelve hand-baskets full, and of the fishes,
Walikusanya vipande vya mikate iliyobaki, Vikajaa vikapu kumi na viwili, na pia vipande vya samaki.
44 and those eating of the loaves were about five thousand men.
Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate.
45 And immediately He constrained His disciples to go into the boat, and to go before [Him] to the other side, to Bethsaida, until He may let the multitude away,
Mara akawaambia wapande kwenye mashua waende sehemu nyingine, hadi Bethsaida, wakati Yeye akiwaaga makutano.
46 and having taken leave of them, He went away to the mountain to pray.
Walipokuwa wamekwisha kuondoka, akaenda mlimani kuomba.
47 And evening having come, the boat was in the midst of the sea, and He alone on the land;
Kulipokuwa jioni, na mashua yao wakati huo ikiwa katikati ya bahari, naye alikuwa peke yake nchi kavu.
48 and He saw them harassed in the rowing, for the wind was against them, and about the fourth watch of the night He comes to them walking on the sea, and wished to pass by them.
Na aliwaona wakitaabika kupiga makasia kwa sababu upepo uliwazuia. Ilipokaribia asubuhi akawaendea, akitembea juu ya maji, na alitaka kuwapita.
49 And they having seen Him walking on the sea, thought [it] to be an apparition, and cried out,
Lakini walipomwona anatembea juu ya maji, wakaingiwa na wasiwasi wakidhani ni mzimu hata wakapiga kelele.
50 for they all saw Him, and were troubled, and immediately He spoke with them, and says to them, “Take courage! I AM; do not be afraid.”
kwa sababu walimwona wakajawa na hofu. Mara akasema nao akawaambia, “Muwe wajasiri! ni mimi! Msiwe na hofu.”
51 And He went up to them into the boat, and the wind stilled, and greatly out of measure they were amazed in themselves, and were wondering,
Akaingia ndani ya mashua, na upepo ukaacha kuvuma, nao wakamshangaa kabisa.
52 for they did not understand concerning the loaves, for their heart has been hard.
Hivyo hawakuwa wameelewa maana ya ile mikate. Maana akili zao zilikuwa na uelewa mdogo.
53 And having passed over, they came on the land of Gennesaret, and drew to the shore,
Nao walipovuka ng'ambo, walifika nchi ya Genesareti mashua ikatia nanga.
54 and they having come forth out of the boat, immediately having recognized Him,
Walipotoka nje ya mashua, mara wakamtambua.
55 they ran around through all that surrounding region, and they began to carry around on the pallets those being ill, where they were hearing that He is,
Wakakimbia kutangaza katika mkoa mzima na wakaanza kuwaleta wagonjwa kwa machela, kila waliposikia anakuja.
56 and wherever He was going, to villages, or cities, or fields, in the marketplaces they were laying the ailing, and were calling on Him, that they may touch if it were but the fringe of His garment, and as many as were touching Him were saved.
Popote alipoingia katika vijiji, au mjini, au katika nchi, waliwaweka wagonjwa mahali pa soko, na wakamsihi awaruhusu kugusa pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa waliponywa.