< Mark 5 >
1 And they came to the other side of the sea, to the region of the Gadarenes,
Walikuja mpaka upande mwingine wa bahari, katika mkoa wa Gerasi
2 and He having come forth out of the boat, immediately there met Him out of the tombs a man with an unclean spirit,
Na ghafla wakati Yesu alipokuwa akitoka nje ya mtumbwi, mtu mwenye roho chafu alikuja kwake kutoka makaburini.
3 who had his dwelling in the tombs, and not even with chains was anyone able to bind him,
Mtu huyu aliishi makaburini. Hakuna aliyeweza kumzuia zaidi, hakuna hata kwa minyororo.
4 because that many times he had been bound with shackles and chains, and the chains had been pulled in pieces by him, and the shackles broken in pieces, and none was able to tame him,
Alikuwa amefungwa nyakati nyingi kwa pingu na minyororo. Aliikata minyororo na pingu zake zilivunjwa. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na nguvu za kumshinda.
5 and always, night and day, he was in the mountains, and in the tombs, crying and cutting himself with stones.
Usiku na mchana akiwa makaburini na milimani, alilia na kujikata yeye mwenyewe kwa mawe makali.
6 And having seen Jesus from afar, he ran and prostrated to Him,
Alipomwona Yesu kwa mbali, alikimbilia kwake na kuinama mbele yake.
7 and having called with a loud voice, he said, “What [regards] me and You, Jesus, Son of God the Most High? I adjure You by God, may You not afflict me!”
Alilia kwa sauti kuu, “Wataka nikufanyie nini, Yesu, Mwana wa Mungu aliye Juu sana? Ninakusihi kwa Mungu mwenyewe, usinitese.”
8 For He said to him, “Come forth, unclean spirit, out of the man!”
Kwa kuwa alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe roho mchafu.”
9 And He was questioning him, “What [is] your name?” And he answered, saying, “Legion [is] my name, because we are many”;
Naye alimwuliza, “Jina lako ni nani?” Naye alimjibu, “Jina langu ni Legion, kwa kuwa tuko wengi.”
10 and he was calling on Him much, that He may not send them out of the region.
Alimsihi tena na tena asiwapeleke nje ya mkoa.
11 And there was there, near the mountains, a great herd of pigs feeding,
Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likilishwa juu ya kilima,
12 and all the demons called on Him, saying, “Send us to the pigs, that into them we may enter”;
nao walimsihi, wakisema, “Tutume kwa nguruwe; tuingie ndani yao.”
13 and immediately Jesus gave them leave, and having come forth, the unclean spirits entered into the pigs, and the herd rushed down the steep place to the sea—and they were about two thousand—and they were choked in the sea.
Hivyo aliwaruhusu; roho wachafu waliwatoka na kuingia ndani ya nguruwe, nao walikimbilia chini ya kilima mpaka baharini, na karibia nguruwe elfu mbili walizama baharini.
14 And those feeding the pigs fled, and told in the city, and in the fields, and they came forth to see what it is that has been done;
Na wale waliokuwa wakiwalisha nguruwe walikimbia na kutoa taarifa ya kilichotokea katika mji na katika nchi. Ndipo watu wengi walitoka kwenda kuona kilichotokea.
15 and they come to Jesus, and see the demoniac, sitting, and clothed, and right-minded—him having had the legion—and they were afraid;
Ndipo walikuja kwa Yesu na walimwona mtu aliyepagawa na pepo—aliyekuwa na Jeshi—amekaa chini, amevikwa, na akiwa katika akili yake timamu, nao waliogopa.
16 and those having seen [it], declared to them how it had come to pass to the demoniac, and about the pigs;
Wale waliokuwa wameona kilichotokea kwa mtu aliyekuwa amepagawa na pepo waliwaambia kilichotokea kwake na pia kuhusu nguruwe.
17 and they began to call on Him to go away from their borders.
Nao walianza kumsihi aondoke katika mkoa wao.
18 And He having gone into the boat, the demoniac was calling on Him that he may be with Him,
Na alipokuwa akiingia ndani ya mtumbwi, mtu aliyekuwa amepagawa na mapepo alimsihi kwamba aende pamoja naye.
19 and Jesus did not permit him, but says to him, “Go away to your house, to your own [friends], and tell them how the LORD did great things to you, and dealt kindly with you”;
Lakini hakumruhusu, lakini alimwambia, “Nenda nyumbani kwako na kwa watu wako, na uwaambie alikufanyia Bwana, na rehema aliyokupa.”
20 and he went away, and began to proclaim in the Decapolis how Jesus did great things to him, and all were wondering.
Hivyo alienda na alianza kutangaza mambo makuu ambayo Yesu amefanya kwake katika Dekapoli, na kila mmoja alistaajabu.
21 And Jesus having passed over in the boat again to the other side, there was gathered a great multitude to Him, and He was near the sea,
Na wakati Yesu alipovuka tena upande mwingine, ndani ya mtumbwi, umati mkubwa ulikusanyika kumzunguka, alipokuwa kando ya bahari.
22 and behold, there comes one of the chiefs of the synagogue, by name Jairus, and having seen Him, he falls at His feet,
Na mmoja wa kiongozi wa sinagogi, aliyeitwa Yairo, alikuja, na alipomwona, alianguka miguuni pake.
23 and he was calling on Him much, saying, “My little daughter is at the last extremity—that having come, You may lay on her [Your] hands, so that she may be saved, and she will live”;
Akamsihi zaidi na zaidi, akisema, “Binti yangu mdogo anakaribia kufa. Ninakusihi, njoo na uweke mikono yako juu yake ili kwamba aweze kupata afya na kuishi.”
24 and He went away with him. And there was following Him a great multitude, and they were thronging Him,
Hivyo alikwenda pamoja naye, na umati mkubwa ulimfuata nao walimzonga karibu wakimzunguka.
25 and a certain woman, being with a flow of blood [for] twelve years,
Kulikuwa na mwanamke ambaye damu yake ilikuwa imetoka kwa miaka kumi na miwili.
26 and having suffered many things under many physicians, and having spent all that she had, and having profited nothing, but rather having come to the worse,
Aliteseka vya kutosha chini ya matabibu wengi na alitumia kila kitu alichokuwa nacho. Hata hivyo hakusaidika kwa chochote, lakini badala yake alizidi kuwa na hali mbaya.
27 having heard about Jesus, having come in the multitude behind, she touched His garment,
Alisikia habari kuhusu Yesu. Hivyo alikuja nyuma yake wakati alipokuwa akitembea ndani ya umati, naye aliligusa vazi lake.
28 for she said, “If I may even touch His garments, I will be saved”;
Kwa kuwa alisema, “Kama nikiyagusa mavazi yake tu, nitakuwa mzima.”
29 and immediately the fountain of her blood was dried up, and she knew in the body that she has been healed of the plague.
Alipomgusa, kutokwa damu kulikoma, na alijisikia katika mwili wake kwamba aliponywa kutoka kwenye mateso yake.
30 And immediately Jesus having known in Himself that power had gone forth out of Him, having turned in the multitude, said, “Who touched My garments?”
Na ghafla Yesu aligundua ndani yake mwenyewe kwamba nguvu zimemtoka. Na aligeuka huku na huku katika umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyeligusa vazi langu?”
31 And His disciples said to Him, “You see the multitude thronging You, and You say, Who touched Me!”
Wanafunzi wake walimwambia, “Unaona umati huu umekusonga ukikuzunguka, nawe wasema, 'Ni nani aliyenigusa?'”
32 And He was looking around to see her who did this,
Lakini Yesu alitazama huku na huku kuona ambaye aliyekuwa amefanya hili.
33 and the woman, having been afraid, and trembling, knowing what was done on her, came, and fell down before Him, and told Him all the truth,
Mwanamke, akijua kilichotokea kwake, aliogopa na kutetemeka. Alikuja na alianguka chini mbele yake na kumwambia ukweli wote.
34 and He said to her, “Daughter, your faith has saved you; go away in peace, and be whole from your plague.”
Alisema kwake, “Binti, imani yako imekufanya uwe mzima. Enenda kwa amani na uponywe kutoka kwenye ugonjwa wako.”
35 As He is yet speaking, there come from the chief of the synagogue’s [house, certain], saying, “Your daughter died, why do you still harass the Teacher?”
Alipokuwa akizungumza, baadhi ya watu walikuja kutoka kwa kiongozi wa Sinagogi, wakisema, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua mwalimu?”
36 And Jesus immediately, having heard the word that is spoken, says to the chief of the synagogue, “Do not be afraid, only believe.”
Lakini Yesu aliposikia ambacho walikisema, alimwambia kiongozi wa Sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
37 And He did not permit anyone to follow with Him, except Peter, and James, and John the brother of James;
Hakumruhusu yeyote kuongozana naye, isipokuwa Petro, Yakobo, na Yohana, ndugu yake Yakobo.
38 and He comes into the house of the chief of the synagogue, and sees a tumult, much weeping and wailing;
Walikuja nyumbani kwa kiongozi wa Sinagogi naye aliona vurugu, kulia kwingi na kuomboleza.
39 and having gone in He says to them, “Why do you make a tumult, and weep? The child did not die, but sleeps”;
Alipoingia nyumbani, aliwaambia, “Kwa nini mmesikitika na kwa nini mnalia? Mtoto hajafa bali amelala.”
40 and they were laughing at Him. And He, having put all forth, takes the father of the child, and the mother, and those with Him, and goes in where the child is lying,
Walimcheka, lakini yeye, aliwatoa wote nje, alimchukua baba wa mtoto na mama na wale waliokuwa pamoja naye, na aliingia ndani alimokuwa mtoto.
41 and having taken the hand of the child, He says to her, “Talitha cumi”; which is, being interpreted, “Girl (I say to you), arise.”
Aliuchukua mkono wa mtoto na alimwambia, “Talitha koum,” ambayo ni kusema, “Binti mdogo, nakuambia, amka.”
42 And immediately the girl arose, and was walking, for she was twelve years [old]; and they were amazed with a great amazement,
Ghafla mtoto aliamka na kutembea (kwa kuwa alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Na ghafla walishikwa na mshangao mkubwa.
43 and He charged them much, that no one may know this thing, and He said that there be given to her to eat.
Aliwaamuru kwa nguvu kwamba hakuna yeyote anapaswa kujua kuhusu hili. Na aliwaambia wampatie yule binti chakula.