< Luke 1 >
1 Seeing that many took in hand to set in order a narration of the matters that have been fully assured among us,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 as they delivered to us, who from the beginning became eyewitnesses, and officers of the word,
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 it seemed good also to me, having followed from the first after all things exactly, to write to you in order, most noble Theophilus,
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 that you may know the certainty of the things wherein you were instructed.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judea, a certain priest, by name Zacharias, of the division of Abijah, and his wife of the daughters of Aaron, and her name Elizabeth;
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 and they were both righteous before God, going on in all the commands and righteousnesses of the LORD blameless,
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 and they had no child, because that Elizabeth was barren, and both were advanced in their days.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it came to pass, in his acting as priest, in the order of his division before God,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 according to the custom of the priesthood, his lot was to make incense, having gone into the temple of the LORD,
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 and all the multitude of the people were praying outside, at the hour of the incense.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 And there appeared to him a messenger of the LORD standing on the right side of the altar of the incense,
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 and Zacharias, having seen, was troubled, and fear fell on him;
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 and the messenger said to him, “Do not fear, Zacharias, for your supplication was heard, and your wife Elizabeth will bear a son to you, and you will call his name John,
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 and there will be joy to you, and gladness, and many will rejoice at his birth,
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 for he will be great before the LORD, and wine and strong drink he may not drink, and he will be full of the Holy Spirit, even from his mother’s womb;
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 and he will turn many of the sons of Israel to the LORD their God,
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 and he will go before Him, in the spirit and power of Elijah, to turn hearts of fathers to children, and disobedient ones to the wisdom of righteous ones, to make ready for the LORD, a people prepared.”
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 And Zacharias said to the messenger, “Whereby will I know this? For I am aged, and my wife is advanced in her days?”
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 And the messenger answering said to him, “I am Gabriel, who has been standing near before God, and I was sent to speak to you, and to proclaim this good news to you,
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 and behold, you will be silent, and not able to speak, until the day that these things will come to pass, because you did not believe my words that will be fulfilled in their season.”
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 And the people were waiting for Zacharias, and wondering at his lingering in the temple,
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 and having come out, he was not able to speak to them, and they perceived that he had seen a vision in the temple, and he was beckoning to them, and remained mute.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 And it came to pass, when the days of his service were fulfilled, he went away to his house,
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 and after those days, his wife Elizabeth conceived, and hid herself five months, saying,
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 “Thus the LORD has done to me, in days in which He looked on [me], to take away my reproach among men.”
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 And in the sixth month the messenger Gabriel was sent by God, to a city of Galilee, the name of which [is] Nazareth,
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 to a virgin, betrothed to a man, whose name [is] Joseph, of the house of David, and the name of the virgin [is] Mary.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 And the messenger having come in to her, said, “Greetings, favored one, the LORD [is] with you; blessed [are] you among women”;
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 and she, having seen, was troubled at his word, and was reasoning of what kind this salutation may be.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 And the messenger said to her, “Do not fear, Mary, for you have found favor with God;
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 and behold, you will conceive in the womb, and will bring forth a Son, and call His Name Jesus;
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 He will be great, and He will be called Son of the Highest, and the LORD God will give Him the throne of His father David,
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and He will reign over the house of Jacob for all ages; and of His kingdom there will be no end.” (aiōn )
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 And Mary said to the messenger, “How will this be, seeing I do not know a husband?”
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 And the messenger answering said to her, “The Holy Spirit will come on you, and the power of the Highest will overshadow you, therefore also the holy-begotten thing will be called Son of God;
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 and behold, Elizabeth, your relative, she also has conceived a son in her old age, and this is the sixth month to her who was called barren;
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 because nothing will be impossible with God.”
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 And Mary said, “Behold, the maidservant of the LORD; let it be to me according to your saying,” and the messenger went away from her.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 And Mary having arisen in those days, went into the hill-country, with haste, to a city of Judea,
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 and entered into the house of Zacharias, and greeted Elizabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 And it came to pass, when Elizabeth heard the salutation of Mary, the baby leapt in her womb; and Elizabeth was filled with the Holy Spirit,
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and spoke out with a loud voice and said, “Blessed [are] you among women, and blessed [is] the Fruit of your womb;
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 and from where [is] this to me, that the mother of my Lord might come to me?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For behold, when the voice of your salutation came to my ears, the baby in my womb leapt in gladness;
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 and blessed [is] she who believed, for there will be a completion to the things spoken to her from the LORD.”
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 And Mary said, “My soul magnifies the LORD,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 And my spirit was glad on God my Savior,
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 Because He looked on the lowliness of His maidservant, For behold, from now on all the generations will call me blessed,
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 For He who is mighty did great things to me, And holy [is] His Name,
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 And His kindness [is] to generations of generations, To those fearing Him;
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 He did powerfully with His arm, He scattered abroad the proud in the thought of their heart,
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 He brought down the mighty from thrones, And He exalted the lowly,
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 He filled the hungry with good, And the rich He sent away empty;
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He has taken hold of His servant Israel, To remember kindness,
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 As He spoke to our fathers, To Abraham and to his seed—throughout the age.” (aiōn )
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
56 And Mary remained with her about three months, and turned back to her house.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 And to Elizabeth was the time fulfilled for her bringing forth, and she bore a son,
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 and the neighbors and her relatives heard that the LORD was making His kindness great with her, and they were rejoicing with her.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 And it came to pass, on the eighth day, they came to circumcise the child, and they were calling him by the name of his father, Zacharias,
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 and his mother answering said, “No, but he will be called John.”
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 And they said to her, “There is none among your relatives who is called by this name,”
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 and they were making signs to his father, what he would wish him to be called,
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 and having asked for a tablet, he wrote, saying, “John is his name”; and they all wondered;
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 and his mouth was opened immediately, and his tongue, and he was speaking, praising God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came on all those dwelling around them, and in all the hill-country of Judea were all these sayings spoken of,
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 and all who heard laid them up in their hearts, saying, “What then will this child be?” And the hand of the LORD was with him.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And his father Zacharias was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 “Blessed [is] the LORD, the God of Israel, Because He looked on, And worked redemption for His people,
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 And raised a horn of salvation to us, In the house of His servant David,
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 As He spoke by the mouth of His holy prophets, Which have been from the age; (aiōn )
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
71 Salvation from our enemies, And out of the hand of all hating us,
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 To do kindness with our fathers, And to be mindful of His holy covenant,
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 An oath that He swore to Abraham our father,
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 To give to us, without fear, Having been delivered out of the hand of our enemies,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 To serve Him, in holiness and righteousness Before Him, all the days of our life.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 And you, child, Prophet of the Highest will you be called; For you will go before the face of the LORD, To prepare His ways.
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 To give knowledge of salvation to His people In forgiveness of their sins,
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 Through the yearnings of our God, In which the rising from on high looked on us,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 To give light to those sitting in darkness and death-shade, To guide our feet to a way of peace.”
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 And the child grew, and was strengthened in spirit, and he was in the deserts until the day of his showing to Israel.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.