< Luke 4 >
1 And Jesus, full of the Holy Spirit, turned back from the Jordan, and was brought in the Spirit into the wilderness,
Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2 being tempted by the Devil forty days, and He did not eat anything in those days, and they having been ended, He afterward hungered,
Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3 and the Devil said to Him, “If You are [the] Son of God, speak to this stone that it may become bread.”
Ndipo Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
4 And Jesus answered him, saying, “It has been written, that, Not on bread only will man live, but on every saying of God.”
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu.”
5 And the Devil having brought Him up to a high mountain, showed to Him all the kingdoms of the world in a moment of time,
Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6 and the Devil said to Him, “To You I will give all this authority, and their glory, because to me it has been delivered, and to whomsoever I will, I give it;
“Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7 You, then, if You may worship me—all will be Yours.”
Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu.”
8 And Jesus answering him said, “[[Get behind Me, Satan, for]] it has been written: You will worship the LORD your God, and Him only you will serve.”
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake.”
9 And he brought Him to Jerusalem, and set Him on the pinnacle of the temple, and said to Him, “If You are the Son of God, cast Yourself down from here,
Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10 for it has been written: To His messengers He will give charge concerning you, to guard over you;
kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11 and: On hands they will bear you up, lest at any time you may dash your foot against a stone.”
na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe.”
12 And Jesus answering said to him, “It has been said, You will not tempt the LORD your God.”
Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 And having ended all temptation, the Devil departed from Him until a convenient season.
Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14 And Jesus turned back in the power of the Spirit to Galilee, and a fame went forth through all the surrounding region concerning Him,
Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15 and He was teaching in their synagogues, being glorified by all.
Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16 And He came to Nazareth, where He has been brought up, and He went in, according to His custom, on the day of the Sabbaths, into the synagogue, and stood up to read;
Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17 and there was given over to Him a scroll of Isaiah the prophet, and having unfolded the scroll, He found the place where it has been written:
Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18 “The Spirit of the LORD [is] on Me, Because He anointed Me To proclaim good news to the poor, Sent Me to heal the broken of heart, To proclaim to captives deliverance, And to blind receiving of sight, To send the bruised away with deliverance,
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19 To proclaim the acceptable year of the LORD.”
na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”
20 And having folded the scroll, having given [it] back to the officer, He sat down, and the eyes of all in the synagogue were gazing on Him.
Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21 And He began to say to them, “Today this writing has been fulfilled in your ears”;
Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo.”
22 and all were bearing testimony to Him, and were wondering at the gracious words that are coming forth out of His mouth, and they said, “Is this not the Son of Joseph?”
Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
23 And He said to them, “Certainly you will say to Me this allegory, Physician, heal yourself; as great things as we heard done in Capernaum, do also here in Your country”;
Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako.”
24 and He said, “Truly I say to you, no prophet is accepted in his own country;
Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25 and of a truth I say to you, many widows were in the days of Elijah, in Israel, when the sky was shut for three years and six months, when great famine came on all the land,
Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 and to none of them was Elijah sent, but—to Sarepta of Sidon, to a woman, a widow;
Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27 and many lepers were in the time of Elisha the prophet, in Israel, and none of them was cleansed, but—Naaman the Syrian.”
Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria.”
28 And all in the synagogue were filled with wrath, hearing these things,
Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29 and having risen, they put Him forth outside the city, and brought Him to the brow of the hill on which their city had been built—to cast Him down headlong,
Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30 and He, having gone through the midst of them, went away.
Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31 And He came down to Capernaum, a city of Galilee, and was teaching them on the Sabbaths,
Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32 and they were astonished at His teaching, because His word was with authority.
Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33 And in the synagogue was a man having a spirit of an unclean demon, and he cried out with a great voice,
Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34 “Aah! What [regards] us and You, Jesus, O Nazarene? You came to destroy us; I have known who You are—the Holy One of God!”
“We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked him, saying, “Be silenced, and come forth out of him”; and the demon having cast him into the midst, came forth from him, having hurt him nothing;
Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: “Nyamaza! Mtoke mtu huyu!” Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36 and amazement came on all, and they were speaking together with one another, saying, “What [is] this word, that with authority and power He commands the unclean spirits, and they come forth?”
Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
37 And there was going forth a fame concerning Him to every place of the surrounding region.
Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38 And having risen out of the synagogue, He entered into the house of Simon, and the mother-in-law of Simon was pressed with a great fever, and they asked Him about her,
Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39 and having stood over her, He rebuked the fever, and it left her, and immediately, having risen, she was ministering to them.
Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40 And at the setting of the sun, all, as many as had any ailing with manifold diseases, brought them to Him, and He, having put hands on each one of them, healed them.
Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41 And demons were also coming forth from many, crying out and saying, “You are the Christ, the Son of God”; and rebuking, He did not permit them to speak, because they knew Him to be the Christ.
Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: “Wewe u Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42 And day having come, having gone forth, He went on to a desolate place, and the multitudes were seeking Him, and they came to Him, and were restraining Him—not to go on from them,
Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43 and He said to them, “Also to the other cities it is necessary for Me to proclaim good news of the Kingdom of God, because for this I have been sent”;
Lakini yeye akawaambia, “Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo.”
44 and He was preaching in the synagogues of Galilee.
Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.