< Leviticus 17 >
1 And YHWH speaks to Moses, saying,
Yahweh akamwambia Musa,
2 “Speak to Aaron and to his sons, and to all the sons of Israel; and you have said to them: This [is] the thing which YHWH has commanded, saying,
“Zungumza na Aroni na wanawe, na watu wote wa Israeli. Waambie mambo ambayo ameamru Yahweh:
3 Any man of the house of Israel who slaughters ox, or lamb, or goat in the camp, or who slaughters [it] at the outside of the camp,
Mtu yeyote wa Isreli anayeua fahali au mwana—kondoo au mbuzi kambini, au amuuaye nje ya kambi, ili kumtoa dhabihu—
4 and has not brought it in to the opening of the Tent of Meeting to bring an offering near to YHWH before the Dwelling Place of YHWH, blood is reckoned to that man—he has shed blood—and that man has been cut off from the midst of his people;
kama hamleti katika ingilio la hema la kukutania ili kumtoa dhabihu kwa Yahweh mbele za hema lake la kukutania, mtu huyo ana hatia ya damu iliyomwagika. Amemwaga damu, na mtu huyo ni sharti akatiliwe mabali kutoka miongoni mwa watu wake.
5 so that the sons of Israel bring in their sacrifices which they are sacrificing on the face of the field, indeed, they have brought them to YHWH, to the opening of the Tent of Meeting, to the priest, and they have sacrificed sacrifices of peace-offerings to YHWH with them.
Kusudi la amri hii ni kwamba watu wa Israeli wataleta dhabihu zao kwa Yahweh kwenye ingilio la hema la kukutania, watazileta kwa kuhani ziweze kutolewa kuwa matoleo ya shukrani kwa Yahweh, badala ya kutoa dhabihu hadharani katika shamba.
6 And the priest has sprinkled the blood on the altar of YHWH, at the opening of the Tent of Meeting, and has made incense with the fat for refreshing fragrance to YHWH;
Kuhani atainyunyiza damu juu ya madhabahu ya Yahweh kwenye ingilio la hema la kukutania; atayachoma mafuta yake ili kutoa harufu ya kupendeza mbele za Yahweh.
7 and they do not sacrifice their sacrifices anymore to the goat [idols] after which they are going whoring; this is a continuous statute to them, throughout their generations.
Ni lazima watu wasitoe tena dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi, ambazo kwazo hutenda kama makahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yao katika vizazi vya watu wao vyote.
8 And you say to them: Any man of the house of Israel, or of the sojourners who sojourns in your midst, who causes burnt-offering or sacrifice to ascend,
Ni lazima uwaambie, 'Mtu yeyote wa Israeli, au Mgeni yeyote aishiye miongoni mwao, atoweye dhabihu
9 and does not bring it in to the opening of the Tent of Meeting to make it to YHWH—that man has been cut off from his people.
na asiilete kwenye ingilio la hema la kukutania ili kuitoa kwa Yahweh, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'
10 And any man of the house of Israel, or of the sojourners who is sojourning in your midst, who eats any blood, I have even set My face against the person who is eating the blood, and have cut him off from the midst of his people;
Na Mtu yeyote wa Israeli, au yeyote wa Wageni anayeishi miongoni mwao, ambaye hunywa damu; nitamkatilia mbali atoke miongoni mwa watu wake.
11 for the life of the flesh is in the blood, and I have given it to you on the altar, to make atonement for your souls; for it [is] the blood which makes atonement for the soul.
Kwa kuwa uhai wa mnyama yeyote umo katika damu yake. Nimeitoa damu yake kwenu kufanya upatanisho juu ya madhabahu kwa ajili ya uhai wenu, kwa sababu ni damu ndiyo ifanyayo upatanisho, kwa kuwa ni damu ipatanishayo kwa ajili ya uhai
12 Therefore I have said to the sons of Israel: No person among you eats blood, and the sojourner who is sojourning in your midst does not eat blood;
Kwa hiyo Niliwaambia Watu wa Israeli kwamba hayupo miongoni mwenu impasaye kula damu, wala yeyote wa Wageni aishiye miongoni mwenu atakaye kula damu.
13 and any man of the sons of Israel, or of the sojourners who is sojourning in your midst, who hunts game, beast or bird, which is eaten—has even poured out its blood and covered it with dust;
Na yeyote miongoni mwa watu wa Israeli, au yeyote wa Wageni aishiye miongoni mwenu ni lazima aimwage damu ya mnyama na kuifukia hiyo damu kwa mafumbi.
14 for [it is] the life of all flesh, its blood is for its life; and I say to the sons of Israel: You do not eat [the] blood of any flesh, for the life of all flesh is its blood; anyone eating it is cut off.
Kwa kuwa uhai wa kila kiumbe umo katika damu yake. Ni kwa sababu hii niliwaambia watu wa Israeli, ni lazima msile damu ya kiumbe cho chote, kwa kuwa maisha ya kila kiumbe chenye uhai ni damu yake. Yeyeote ailaye ni lazima akatiliwe mbali.
15 And any person who eats a carcass or torn thing, among natives or among sojourners, has washed his garments and bathed with water, and been unclean until the evening—then he has been clean;
Mtu yeyote alaye mnyama aliyekufa au ambaye amelaruliwa na wanyama pori, ama yule mtu ni mwenyeji wa kuzaliwa au ni mgeni aishiye miongoni mwenu, ni lazima atazifua nguo zake na kujiosha katika maji, naye atakuwa najisi hata jioni. Kisha atakuwa safi.
16 and if he does not wash, and does not bathe his flesh—then he has borne his iniquity.”
Lakini kama hazifui nguo zake au kuosha mwili wake, ni lazima aichukue hatia yake”.