< Leviticus 14 >

1 And YHWH speaks to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 “This is a law of the leper, in the day of his cleansing, that he has been brought to the priest,
“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
3 and the priest has gone out to the outside of the camp, and the priest has seen, and behold, the plague of leprosy has ceased from the leper,
Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
4 and the priest has commanded, and he has taken for him who is to be cleansed, two clean living birds, and cedar wood, and scarlet, and hyssop.
kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
5 And the priest has commanded, and he has slaughtered one bird on an earthen vessel, over running water;
Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
6 [as for] the living bird, he takes it, and the cedar wood, and the scarlet, and the hyssop, and has dipped them and the living bird in the blood of the slaughtered bird, over the running water,
Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 and he has sprinkled on him who is to be cleansed from the leprosy seven times, and has pronounced him clean, and has sent out the living bird over the face of the field.
Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
8 And he who is to be cleansed has washed his garments, and has shaved all his hair, and has bathed with water, and has been clean, and afterward he comes into the camp, and has dwelt at the outside of his tent [for] seven days.
“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
9 And it has been, on the seventh day—he shaves all his hair, his head, and his beard, and his eyebrows, even all his hair he shaves, and he has washed his garments, and has bathed his flesh with water, and has been clean.
Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
10 And on the eighth day he takes two lambs, perfect ones, and one ewe-lamb, daughter of a year, a perfect one, and three-tenth parts of flour [for] a present, mixed with oil, and one log of oil.
“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
11 And the priest who is cleansing has caused the man who is to be cleansed to stand with them before YHWH, at the opening of the Tent of Meeting,
Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
12 and the priest has taken one male lamb, and has brought it near for a guilt-offering, also the log of oil, and has waved them [as] a wave-offering before YHWH.
“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
13 And he has slaughtered the lamb in the place where he slaughters the sin-offering and the burnt-offering, in the holy place; for like the sin-offering, the guilt-offering is for the priest; it [is] most holy.
Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
14 And the priest has taken of the blood of the guilt-offering, and the priest has put [it] on the tip of the right ear of him who is to be cleansed, and on the thumb of his right hand, and on the great toe of his right foot;
Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
15 and the priest has taken of the log of oil, and has poured [it] on the left palm of the priest,
Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
16 and the priest has dipped his right finger in the oil which [is] on his left palm, and has sprinkled of the oil with his finger seven times before YHWH.
na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
17 And of the remainder of the oil which [is] on his palm, the priest puts [it] on the tip of the right ear of him who is to be cleansed, and on the thumb of his right hand, and on the great toe of his right foot, on the blood of the guilt-offering;
Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
18 and the remnant of the oil which [is] on the palm of the priest, he puts [it] on the head of him who is to be cleansed, and the priest has made atonement for him before YHWH.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
19 And the priest has made the sin-offering, and has made atonement for him who is to be cleansed from his uncleanness, and afterward he slaughters the burnt-offering;
“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
20 and the priest has caused the burnt-offering to ascend, also the present, on the altar, and the priest has made atonement for him, and he has been clean.
na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
21 And if he [is] poor, and his hand is not reaching [these things], then he has taken one lamb [for] a guilt-offering, for a wave-offering, to make atonement for him, and one-tenth part of flour mixed with oil for a present, and a log of oil,
“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
22 and two turtle-doves, or two young pigeons, which his hand reaches to, and one has been a sin-offering and one a burnt-offering;
na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23 and he has brought them in on the eighth day for his cleansing to the priest, to the opening of the Tent of Meeting, before YHWH.
“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
24 And the priest has taken the lamb of the guilt-offering, and the log of oil, and the priest has waved them [as] a wave-offering before YHWH;
Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 and he has slaughtered the lamb of the guilt-offering, and the priest has taken of the blood of the guilt-offering, and has put [it] on the tip of the right ear of him who is to be cleansed, and on the thumb of his right hand, and on the great toe of his right foot;
Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
26 and the priest pours of the oil on the left palm of the priest;
Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
27 and the priest has sprinkled with his right finger of the oil which [is] on his left palm, seven times before YHWH.
na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
28 And the priest has put of the oil which [is] on his palm, on the tip of the right ear of him who is to be cleansed, and on the thumb of his right hand, and on the great toe of his right foot, on the place of the blood of the guilt-offering;
Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
29 and he puts the remnant of the oil which [is] on the palm of the priest on the head of him who is to be cleansed, to make atonement for him, before YHWH.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
30 And he has made one of the turtle-doves or of the young pigeons (from that which his hand reaches to,
Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
31 [even] that which his hand reaches to), one a sin-offering and one a burnt-offering, besides the present, and the priest has made atonement for him who is to be cleansed before YHWH.
mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
32 This [is] a law of him in whom [is] a plague of leprosy, whose hand does not reach to his cleansing.”
Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
33 And YHWH speaks to Moses and to Aaron, saying,
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
34 “When you come into the land of Canaan, which I am giving to you for a possession, and I have put a plague of leprosy in a house [in] the land of your possession,
“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
35 then he whose the house [is] has come in and declared [it] to the priest, saying, Some plague has appeared to me in the house;
ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
36 and the priest has commanded, and they have prepared the house before the priest comes in to see the plague (that all which [is] in the house is not unclean), and afterward the priest comes in to see the house;
Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
37 and he has seen the plague, and behold, the plague [is] in the walls of the house, hollow streaks, greenish or reddish, and their appearance [is] lower than the wall,
Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
38 and the priest has gone out of the house to the opening of the house, and has shut up the house [for] seven days.
kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
39 And the priest has turned back on the seventh day, and has seen, and behold, the plague has spread in the walls of the house,
Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
40 and the priest has commanded, and they have drawn out the stones in which the plague [is], and have cast them to the outside of the city, to an unclean place;
ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
41 and he causes the house to be scraped all around inside, and they have poured out the clay which they have scraped off, at the outside of the city, at an unclean place;
Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
42 and they have taken other stones, and brought [them] to the place of the stones, and he takes other clay and has coated the house.
Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43 And if the plague returns, and has broken out in the house, after he has drawn out the stones, and after the scraping of the house, and after the coating,
“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
44 then the priest has come in and seen, and behold, the plague has spread in the house; it [is] a fretting leprosy in the house; it [is] unclean.
kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
45 And he has broken down the house, its stones, and its wood, and all the clay of the house, and he has brought [them] forth to the outside of the city, to an unclean place.
Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
46 And he who is going into the house all the days he has shut it up, is unclean until the evening;
“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
47 and he who is lying in the house washes his garments; and he who is eating in the house washes his garments.
Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
48 And if the priest certainly comes in, and has seen, and behold, the plague has not spread in the house after the coating of the house, then the priest has pronounced the house clean, for the plague has been healed.
“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
49 And he has taken two birds, and cedar wood, and scarlet, and hyssop for the cleansing of the house;
Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
50 and he has slaughtered one bird on an earthen vessel, over running water;
Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
51 and he has taken the cedar wood, and the hyssop, and the scarlet, and the living bird, and has dipped them in the blood of the slaughtered bird, and in the running water, and has sprinkled against the house seven times.
Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
52 And he has cleansed the house with the blood of the bird, and with the running water, and with the living bird, and with the cedar wood, and with the hyssop, and with the scarlet;
Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
53 and he has sent the living bird away to the outside of the city to the face of the field, and has made atonement for the house, and it has been clean.
Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
54 This [is] the law for every plague of the leprosy and for scale,
Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
55 and for leprosy of a garment, and of a house,
upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
56 and for a rising, and for a scab, and for a bright spot—
kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
57 to direct in the day of being unclean, and in the day of being clean; this [is] the law of the leprosy.”
kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

< Leviticus 14 >