< Judges 4 >

1 And the sons of Israel add to do evil in the eyes of YHWH when Ehud is dead,
Baada ya Ehudi kufa, watu wa Israeli walifanya tena yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
2 and YHWH sells them into the hand of Jabin king of Canaan, who has reigned in Hazor, and Sisera [is] the head of his host, and he is dwelling in Harosheth of the nations;
Bwana akawatia mkononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyewala huko Hasori. Kamanda wa jeshi lake aitwaye Sisera, naye aliishi Harosheti ya Mataifa.
3 and the sons of Israel cry to YHWH, for he has nine hundred chariots of iron, and he has oppressed the sons of Israel mightily [for] twenty years.
Wana wa Israeli wakamwomba Bwana awasaidie, kwa sababu Sisera alikuwa na magari ya chuma mia tisa na akawashinda wana wa Israeli kwa nguvu kwa miaka ishirini.
4 And Deborah, a woman, a prophetess, wife of Lapidoth, she is judging Israel at that time,
Basi Debora, nabii wa kike (mke wa Lapidothi), alikuwa mwamuzi anayeongoza katika Israeli wakati huo.
5 and she is dwelling under the palm-tree of Deborah, between Ramah and Beth-El, in the hill-country of Ephraim, and the sons of Israel go up to her for judgment.
Naye aliketi chini ya mtende wa Debora kati ya Rama na Betheli katika nchi ya mlima wa Efraimu, na watu wa Israeli walimwendea ili kutatua migogoro yao.
6 And she sends and calls for Barak son of Abinoam, out of Kedesh-Naphtali, and says to him, “Has YHWH, God of Israel, not commanded? Go, and you have drawn toward Mount Tabor, and have taken with you ten thousand men, out of the sons of Naphtali, and out of the sons of Zebulun,
Akamtuma Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali. Akamwambia, Bwana, Mungu wa Israeli, anakuamuru, Nenda katika mlima wa Tabori, uende pamoja nawe watu elfu kumi kutoka Naftali na Zabuloni.
7 and I have drawn to you, to the Brook of Kishon, Sisera, head of the host of Jabin, and his chariot, and his multitude, and have given him into your hand.”
Nitamfukuza Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, akutane nawe karibu na mto Kishoni, pamoja na magari yake na jeshi lake, na nitakupa ushindi juu yake. '
8 And Barak says to her, “If you go with me, then I have gone; and if you do not go with me, I do not go”;
Baraka akamwambia, 'Ikiwa utakwenda nami, nitakwenda, lakini ikiwa huendi pamoja nami, sitaenda.'
9 and she says, “I certainly go with you; only, surely your glory is not on the way which you are going, for YHWH sells Sisera into the hand of a woman”; and Deborah rises and goes with Barak to Kedesh.
Alisema, 'Nitakwenda nawe. Hata hivyo, njia unayoienda haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamuuza Sisera mkononi mwa mwanamke. Ndipo Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka Kedeshi.
10 And Barak calls Zebulun and Naphtali to Kedesh, and he goes up—ten thousand men [are] at his feet—and Deborah goes up with him.
Baraki akawaita wana wa Zebuloni na Naftali kusanyika Kedeshi. Watu elfu kumi walimfuata, na Debora akaenda pamoja naye.
11 And Heber the Kenite has been separated from the Kenite, from the sons of Hobab father-in-law of Moses, and he stretches out his tent to the oak in Zaanaim, which [is] by Kedesh.
Heberi (Mkeni) alijitenganisha na Wakeni - walikuwa wazao wa Hobabu (mkwe wa Musa) - na akaweka hema yake mwaloni uliopo huko Saanaimu karibu na Kedesh.
12 And they declare to Sisera that Barak son of Abinoam has gone up to Mount Tabor,
Walipomwambia Sisera kwamba Baraka, mwana wa Abinoamu, alikuwa amekwenda mlima wa Tabori,
13 and Sisera calls all his chariots, nine hundred chariots of iron, and all the people who [are] with him, from Harosheth of the nations, to the Brook of Kishon.
Sisera akawaita magari yake yote, magari ya farasi mia tisa, na askari wote waliokuwa pamoja naye, kutoka Haroshethi ya Mataifa mpaka Mto Kishoni.
14 And Deborah says to Barak, “Rise, for this [is] the day in which YHWH has given Sisera into your hand; has YHWH not gone out before you?” And Barak goes down from Mount Tabor, and ten thousand men after him.
Debora akamwambia Baraka, Nenda! Kwa maana hii ndiyo siku ambayo Bwana amekupa ushindi juu ya Sisera. Je! si Bwana anayekuongoza? Basi Baraka akashuka kutoka mlima wa Tabori na watu kumi elfu wakamfuata.
15 And YHWH destroys Sisera, and all the chariots, and all the camp, by the mouth of the sword, before Barak, and Sisera comes down from off the chariot, and flees on his feet.
Bwana alifanya jeshi la Sisera kuchanganyikiwa, magari yake yote, na jeshi lake lote. Watu wa Baraka waliwashinda na Sisera akaanguka kutoka kwenye gari lake na kukimbia kwa miguu.
16 And Barak has pursued after the chariots and after the camp, to Harosheth of the nations, and all the camp of Sisera falls by the mouth of the sword—there has not been left even one.
Lakini Baraka akayafuata magari na jeshi mpaka Haroshethi ya Mataifa, na jeshi lote la Sisera likauawa kwa upanga, wala hakuna mtu aliyeokoka.
17 And Sisera has fled on his feet to the tent of Jael wife of Heber the Kenite, for [there is] peace between Jabin king of Hazor and the house of Heber the Kenite;
Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka hema ya Yaeli, mkewe Heberi Mkeni; kwa sababu kulikuwa na amani kati ya Yabini mfalme wa Hazori, na nyumba ya Heberi Mkeni.
18 and Jael goes out to meet Sisera and says to him, “Turn aside, my lord, turn aside to me, do not fear”; and he turns aside to her, into the tent, and she covers him with a mantle.
Jaeli akatoka kumlaki Sisera, akamwambia, karibu, bwana wangu; karibu kwangu, wala usiogope. Basi akakaribia kwake, akaingia hemani kwake, naye akamvika bushuti.
19 And he says to her, “Please give me a little water to drink, for I am thirsty”; and she opens the bottle of milk, and gives him to drink, and covers him.
Akamwambia, Tafadhali nipe maji kidogo ninywe, kwa maana nina kiu. Alifungua mfuko wa ngozi ya maziwa akampa anywe, kisha akamfunika tena.
20 And he says to her, “Stand at the opening of the tent, and it has been, if any comes in, and has asked you and said, Is there a man here? That you have said, There is not.”
Akamwambia, “Simama mlangoni pa hema. Ikiwa mtu atakuja na kukuuliza, 'Je, kuna mtu hapa?', Sema 'Hapana'.”
21 And Jael wife of Heber takes the pin of the tent, and takes the hammer in her hand, and goes to him gently, and strikes the pin into his temples, and it fastens in the earth—and he has been fast asleep, and is weary—and he dies.
Kisha Jaeli (mke wa Heberi) akachukua kigingi cha hema na nyundo mkononi mwake akamwendea kwa siri, kwa sababu alikuwa amelala usingizi mzito, naye akakitia kigingi cha hema upande wa kichwa chake akamchoma na kikapenya kushuka chini. Hivyo akafa.
22 And behold, Barak is pursuing Sisera, and Jael comes out to meet him, and says to him, “Come, and I show you the man whom you are seeking”; and he comes to her, and behold, Sisera is fallen—dead, and the pin [is] in his temples.
Baraka alipokuwa akimfuata Sisera, Jaeli alitoka kukutana naye akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Basi akaingia pamoja naye, tazama Sisera amekufa, na kigingi cha hema kando ya kichwa chake.
23 And God humbles Jabin king of Canaan before the sons of Israel on that day,
Basi siku hiyo Mungu alimshinda Jabin, mfalme wa Kanaani, mbele ya watu wa Israeli.
24 and the hand of the sons of Israel goes, going on and becoming hard on Jabin king of Canaan, until they have cut off Jabin king of Canaan.
Uwezo wa watu wa Israeli ulikua na nguvu zaidi dhidi ya Jabin mfalme wa Kanaani, hata walipomwangamiza.

< Judges 4 >