< Judges 2 >
1 And the Messenger of YHWH goes up from Gilgal to Bochim,
Malaika wa Bwana akakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi.
2 and says, “I cause you to come up out of Egypt, and bring you into the land which I have sworn to your fathers, and say, I do not break My covenant with you for all time; and you make no covenant with the inhabitants of this land—you break down their altars; and you have not listened to My voice—what [is] this you have done?
Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu yao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili?
3 And I have also said, I do not cast them out from your presence, and they have been for adversaries to you, and their gods are for a snare to you.”
Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”
4 And it comes to pass, when the Messenger of YHWH speaks these words to all the sons of Israel, that the people lift up their voice and weep,
Malaika wa Bwana alipomaliza kusema mambo haya kwa Waisraeli wote, watu wakalia kwa sauti kuu.
5 and they call the name of that place Bochim, and sacrifice to YHWH there.
Wakapaita mahali pale Bokimu. Nao wakamtolea Bwana sadaka.
6 And Joshua sends the people away, and the sons of Israel go, each to his inheritance, to possess the land;
Baada ya Yoshua kuwapa watu ruhusa waende zao, Waisraeli wakaenda kwenye urithi wao wenyewe ili kumiliki nchi yao.
7 and the people serve YHWH all [the] days of Joshua, and all [the] days of [the] elderly who prolonged days after Joshua, who saw all the great work of YHWH which He did to Israel.
Watu wakamtumikia Bwana siku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, waliokuwa wameona mambo makuu ambayo Bwana alikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli.
8 And Joshua son of Nun, servant of YHWH, dies, a son of one hundred and ten years,
Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, akafa akiwa na umri wa miaka 110.
9 and they bury him in the border of his inheritance, in Timnath-Heres, in the hill-country of Ephraim, on the north of Mount Gaash;
Wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Heresi katika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima Gaashi.
10 and all that generation have also been gathered to their fathers, and another generation rises after them who have not known YHWH, and even the work which He has done to Israel.
Baada ya kizazi kile chote kukusanywa pamoja na baba zao, kikainuka kizazi kingine baada yao ambacho hakikumjua Bwana, wala matendo yale aliyokuwa ametenda kwa ajili ya Waisraeli.
11 And the sons of Israel do evil in the eyes of YHWH, and serve the Ba‘alim,
Kwa hiyo Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Bwana na kuwatumikia Mabaali.
12 and forsake YHWH, God of their fathers, who brings them out from the land of Egypt, and go after other gods (of the gods of the peoples who [are] around them), and bow themselves to them, and provoke YHWH,
Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri. Wakaifuata na kuiabudu miungu mbalimbali ya mataifa yanayowazunguka. Wakamkasirisha Bwana,
13 indeed, they forsake YHWH, and do service to Ba‘al and to Ashtaroth.
kwa sababu walimwacha na kutumikia Baali na Maashtorethi.
14 And the anger of YHWH burns against Israel, and He gives them into the hand of spoilers, and they spoil them, and He sells them into the hand of their surrounding enemies, and they have not been able to stand before their enemies anymore;
Hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa wavamizi waliowateka nyara. Akawauza katika mikono ya adui zao pande zote, hivyo hawakuweza tena kuwazuia adui zao.
15 in every [place] where they have gone out, the hand of YHWH has been against them for calamity, as YHWH has spoken, and as YHWH has sworn to them, and they are greatly distressed.
Popote Israeli walipotoka kwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa kinyume nao ili kuwashinda, kama vile alivyokuwa amewaapia. Nao wakawa katika taabu kubwa.
16 And YHWH raises up judges, and they save them from the hand of their spoilers;
Ndipo Bwana akawainua waamuzi, ambao waliwaokoa katika mikono ya hao watu waliowashambulia.
17 and they have also not listened to their judges, but have gone whoring after other gods, and bow themselves to them; they have turned aside [with] haste out of the way [in] which their fathers walked to obey the commands of YHWH—they have not done so.
Lakini hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, bali walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine na kuiabudu. Waligeuka mara na kuiacha njia ambayo baba zao waliiendea, yaani, njia ya kutii amri za Bwana.
18 And when YHWH raised up judges for them—then YHWH was with the judge, and saved them out of the hand of their enemies all [the] days of the judge; for YHWH sighs, because of their groaning from the presence of their oppressors, and of those thrusting them away.
Kila mara Bwana alipowainulia mwamuzi, Bwana alikuwa pamoja na huyo mwamuzi, naye aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao kwa kipindi chote alichoishi yule mwamuzi. Kwa kuwa Bwana aliwahurumia kwa sababu ya kilio chao cha huzuni kwa ajili ya wale waliokuwa wakiwatesa na kuwataabisha.
19 And it has come to pass, when the judge dies—they turn back and have done corruptly above their fathers, to go after other gods, to serve them, and to bow themselves to them; they have not fallen from their doings, and from their stiff way.
Lakini kila mara mwamuzi alipofariki, watu walirudia katika hali mbaya ya uovu zaidi kuliko baba zao, wakiifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao maovu na njia zao za ukaidi.
20 And the anger of YHWH burns against Israel, and He says, “Because that this nation has transgressed My covenant which I commanded their fathers, and have not listened to My voice—
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia sana Israeli na kusema, “Kwa kuwa taifa hili limevunja Agano lile nililofanya na baba zao na hawakunisikiliza,
21 I also do not continue to dispossess any from before them of the nations which Joshua has left when he dies,
mimi nami sitafukuza taifa lolote ambalo Yoshua aliliacha alipofariki.
22 in order to try Israel by them, whether they are keeping the way of YHWH, to go in it, as their fathers kept [it], or not.”
Nitayatumia ili nipate kuwapima Israeli na kuona kama wataishika njia ya Bwana na kuenenda katika hiyo kama njia baba zao walivyofanya.”
23 And YHWH leaves these nations, so as not to dispossess them quickly, and did not give them into the hand of Joshua.
Bwana alikuwa ameyaacha hayo mataifa yabaki; hakuyaondoa mara moja kwa kuyatia mikononi mwa Yoshua.