< Judges 16 >
1 And Samson goes to Gaza, and sees a woman there, a harlot, and goes in to her;
Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake.
2 [it is told] to the Gazathites, saying, “Samson has come in here”; and they go around and lay wait for him all the night at the gate of the city, and keep themselves silent all the night, saying, “Until the morning light—then we have slain him.”
Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”
3 And Samson lies down until the middle of the night, and rises in the middle of the night, and lays hold on the doors of the gate of the city, and on the two side-posts, and removes them with the bar, and puts [them] on his shoulders, and takes them up to the top of the hill, which [is] on the front of Hebron.
Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
4 And it comes to pass afterward that he loves a woman in the Valley of Sorek, and her name [is] Delilah,
Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila.
5 and the princes of the Philistines come up to her, and say to her, “Entice him, and see wherein his great power [is], and wherein we are able for him—and we have bound him to afflict him, and each one of us gives eleven hundred pieces of silver to you.”
Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”
6 And Delilah says to Samson, “Please declare to me wherein your great power [is], and with what you are bound, to afflict you.”
Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”
7 And Samson says to her, “If they bind me with seven green cords which have not been dried, then I have been weak, and have been as one of mankind.”
Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
8 And the princes of the Philistines bring up to her seven green cords which have not been dried, and she binds him with them.
Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni.
9 And the ambush is abiding with her in an inner chamber, and she says to him, “Philistines [are] on you, Samson!” And he breaks the cords as a thread of tow is broken in its touching fire, and his power has not been known.
Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.
10 And Delilah says to Samson, “Behold, you have played on me, and speak lies to me; now, please declare to me with what you are bound.”
Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”
11 And he says to her, “If they certainly bind me with thick bands, new ones, by which work has not been done, then I have been weak, and have been as one of mankind.”
Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
12 And Delilah takes thick bands, new ones, and binds him with them, and says to him, “Philistines [are] on you, Samson!” And the ambush is abiding in an inner chamber, and he breaks them from off his arms as a thread.
Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.
13 And Delilah says to Samson, “Until now you have played on me, and speak lies to me; declare to me with what you are bound.” And he says to her, “If you weave the seven locks of my head with the web.”
Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo,
14 And she fixes [it] with the pin and says to him, “Philistines [are] on you, Samson!” And he awakens out of his sleep, and pulls out the pin of the loom, and with the web.
na kuvikaza kwa msumari. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.
15 And she says to him, “How do you say, I have loved you, and your heart is not with me? These three times you have played on me, and have not declared to me wherein your great power [is].”
Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.”
16 And it comes to pass, because she distressed him with her words all the days, and urges him, and his soul is grieved to death,
Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.
17 that he declares all his heart to her, and says to her, “A razor has not gone up on my head, for I [am] a Nazarite to God from the womb of my mother; if I have been shaven, then my power has turned aside from me, and I have been weak, and have been as all of mankind.”
Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”
18 And Delilah sees that he has declared all his heart to her, and she sends and calls for the princes of the Philistines, saying, “Come up this time, for he has declared all his heart to me”; and the princes of the Philistines have come up to her, and bring up the money in their hand.
Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao.
19 And she makes him sleep on her knees, and calls for a man, and shaves the seven locks of his head, and begins to afflict him, and his power turns aside from off him;
Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.
20 and she says, “Philistines [are] on you, Samson!” And he awakens out of his sleep and says, “I go out as time by time, and shake free”; but he has not known that YHWH has turned aside from off him.
Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!” Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.
21 And the Philistines seize him, and pick out his eyes, and bring him down to Gaza, and bind him with two bronze chains; and he is grinding in the prison-house.
Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani.
22 And the hair of his head begins to shoot up when he has been shaven,
Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.
23 and the princes of the Philistines have been gathered together to sacrifice a great sacrifice to their god Dagon, and to rejoice; and they say, “Our god has given our enemy Samson into our hand.”
Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”
24 And the people see him, and praise their god, for they said, “Our god has given into our hand our enemy, and he who is laying waste to our land, and who multiplied our wounded.”
Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema: “Sasa mungu wetu amemtia adui yetu mikononi mwetu, yule aliyeharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”
25 And it comes to pass, when their heart [is] glad, that they say, “Call for Samson, and he entertains for us”; and they call for Samson out of the prison-house, and he entertains their faces, and they cause him to stand between the pillars.
Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao. Wakamweka kati ya nguzo mbili.
26 And Samson says to the young man who is keeping hold on his hand, “Let me also feel the pillars on which the house is established, and I lean on them.”
Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.”
27 And the house has been full of the men and the women, and all the princes of the Philistines [are] there, and about three thousand men and women [are] on the roof, who are watching Samson entertain.
Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza.
28 And Samson calls to YHWH and says, “Lord YHWH, please remember me and please strengthen me only this time, O God; and I am avenged—vengeance at once—because of my two eyes, on the Philistines.”
Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.”
29 And Samson turns aside [to] the two middle pillars, on which the house is established, and on which it is supported, [to] one with his right hand and one with his left;
Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto.
30 and Samson says, “Let me die with the Philistines,” and he inclines himself powerfully, and the house falls on the princes, and on all the people who [are] in it, and the dead whom he has put to death in his death are more than those whom he put to death in his life.
Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.
31 And his brothers come down, and all the house of his father, and lift him up, and bring him up, and bury him between Zorah and Eshtaol, in the burying-place of his father Manoah; and he has judged Israel [for] twenty years.
Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.