< Joshua 15 >
1 And the lot for the tribe of the sons of Judah, for their families, is to the border of Edom; the wilderness of Zin southward, at the extremity of the south;
Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
2 and to them the south border is at the extremity of the Salt Sea, from the bay which is looking southward;
Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
3 and it has gone out to the south to Maaleh-Akrabbim, and passed over to Zin, and gone up on the south to Kadesh-Barnea, and passed over [to] Hezron, and gone up to Adar, and turned around to Karkaa,
Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
4 and passed over [to] Azmon, and gone out [at] the Brook of Egypt, and the outgoings of the border have been at the sea; this is the south border to you.
Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
5 And the east border [is] the Salt Sea, to the extremity of the Jordan, and the border at the north quarter [is] from the bay of the sea, at the extremity of the Jordan;
Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
6 and the border has gone up [to] Beth-Hoglah, and passed over on the north of Beth-Arabah, and the border has gone up [to] the stone of Bohan son of Reuben:
Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
7 and the border has gone up toward Debir from the Valley of Achor, and northward looking to Gilgal, which [is] opposite the ascent of Adummim, which [is] on the south of the brook, and the border has passed over to the waters of En-Shemesh, and its outgoings have been to En-Rogel;
Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
8 and the border has gone up the Valley of the Son of Hinnom, to the side of the Jebusite on the south (it [is] Jerusalem), and the border has gone up to the top of the hill-country which [is] on the front of the Valley of Hinnom westward, which [is] in the extremity of the Valley of the Rephaim northward;
kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
9 and the border has been marked out, from the top of the hill-country to the fountain of the waters of Nephtoah, and has gone out to the cities of Mount Ephron, and the border has been marked out [to] Ba‘alah (it [is] Kirjath-Jearim);
Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
10 and the border has gone around from Ba‘alah westward, to Mount Seir, and passed over to the side of Mount Jearim (it [is] Chesalon), on the north, and gone down [to] Beth-Shemesh, and passed over to Timnah;
Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
11 and the border has gone out to the side of Ekron northward, and the border has been marked out [to] Shicron, and has passed over to Mount Ba‘alah, and gone out [to] Jabneel; and the outgoings of the border have been at the sea.
Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
12 And the west border [is] to the Great Sea, and [its] border; this [is] the border of the sons of Judah all around for their families.
Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
13 And to Caleb son of Jephunneh he has given a portion in the midst of the sons of Judah, according to the command of YHWH to Joshua, [even] the city of Arba, father of Anak—it [is] Hebron.
Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
14 And Caleb is dispossessing there the three sons of Anak: Sheshai, and Ahiman, and Talmai, children of Anak,
Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
15 and he goes up there to the inhabitants of Debir; and the name of Debir [was] formerly Kirjath-Sepher.
Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
16 And Caleb says, “He who strikes Kirjath-Sephar, and has captured it—I have given my daughter Achsah to him for a wife.”
Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
17 And Othniel son of Kenaz, brother of Caleb, captures it, and he gives his daughter Achsah to him for a wife.
Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
18 And it comes to pass, in her coming in, that she persuades him to ask [for] a field from her father, and she comes down off the donkey, and Caleb says to her, “What do you [want]?”
Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
19 And she says, “Give a blessing to me; when you have given me the land of the south, then you have given springs of waters to me”; and he gives the upper springs and the lower springs to her.
Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
20 This [is] the inheritance of the tribe of the sons of Judah, for their families.
Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
21 And the cities at the extremity of the tribe of the sons of Judah are to the border of Edom in the south, Kabzeel, and Eder, and Jagur,
Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
22 and Kinah, and Dimonah, and Adadah,
Kina, Dimona, Adada,
23 and Kedesh, and Hazor, and Ithnan,
Kadeshi, Hazor, Ithinani,
24 Ziph, and Telem, and Bealoth,
Zifu, Telemu, Bealothi.
25 and Hazor, Hadattah, and Kerioth, Hezron (it [is] Hazor),
Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
26 Amam, and Shema, and Moladah,
Amamu, shema, Molada,
27 and Hazar-Gaddah, and Heshmon, and Beth-Palet,
Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
28 and Hazar-Shual, and Beer-Sheba, and Bizjothjah,
Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
29 Ba‘alah, and Iim, and Azem,
Baala, Limu, Ezemu,
30 and Eltolad, and Chesil, and Hormah,
Eltoladi, Kesili, Horma,
31 and Ziklag, and Madmannah, and Sansannah,
Ziklagi, Madimana, Sansana,
32 and Lebaoth, and Shilhim, and Ain, and Rimmon; all the cities [are] twenty-nine, and their villages.
Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
33 In the low country: Eshtaol, and Zoreah, and Ashnah,
Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
34 and Zanoah, and En-Gannim, Tappuah, and Enam,
Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
35 Jarmuth, and Adullam, Socoh, and Azekah,
Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
36 and Sharaim, and Adithaim, and Gederah, and Gederothaim; fourteen cities and their villages.
Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
37 Zenan, and Hadashah, and Migdal-Gad,
Zena, Hadasha, Migidagadi,
38 and Dilean, and Mizpeh, and Joktheel,
Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
39 Lachish, and Bozkath, and Eglon,
Lakishi, Bozikathi, Egloni.
40 and Cabbon, and Lahmam, and Kithlish,
Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
41 and Gederoth, Beth-Dagon, and Naamah, and Makkedah; sixteen cities and their villages.
Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
42 Libnah, and Ether, and Ashan,
Libna, Etheri, Ashani,
43 and Jiphtah, and Ashnah, and Nezib,
Ifuta, Ashina, Nezibu,
44 and Keilah, and Achzib, and Mareshah; nine cities and their villages.
Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
45 Ekron and its towns and its villages,
Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
46 from Ekron and westward, all that [are] by the side of Ashdod, and their villages.
kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
47 Ashdod, its towns and its villages, Gaza, its towns and its villages, to the Brook of Egypt, and the Great Sea, and [its] border.
Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
48 And in the hill-country: Shamir, and Jattir, and Socoh,
Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
49 and Dannah, and Kirjath-Sannah (it [is] Debir),
Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
50 and Anab, and Eshtemoh, and Anim,
Anabu, Eshitemo, Animu,
51 and Goshen, and Holon, and Giloh; eleven cities and their villages.
Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
52 Arab, and Dumah, and Eshean,
Arabu, Duma, Ehani,
53 and Janum, and Beth-Tappuah, and Aphekah,
Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
54 and Humtah, and Kirjath-Arba (it [is] Hebron), and Zior; nine cities and their villages.
Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
55 Maon, Carmel, and Ziph, and Juttah,
Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
56 and Jezreel, and Jokdeam, and Zanoah,
Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
57 Cain, Gibeah, and Timnah; ten cities and their villages.
Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
58 Halhul, Beth-Zur, and Gedor,
Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
59 and Maarath, and Beth-Anoth, and Eltekon; six cities and their villages.
Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
60 Kirjath-Ba‘al (it [is] Kirjath-Jearim), and Rabbah; two cities and their villages.
Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
61 In the wilderness: Beth-Arabah, Middin, and Secacah,
Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
62 and Nibshan, and the City of Salt, and En-Gedi; six cities and their villages.
Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
63 As for the Jebusites, inhabitants of Jerusalem, the sons of Judah have not been able to dispossess them, and the Jebusite dwells with the sons of Judah in Jerusalem to this day.
Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.