< John 9 >
1 And passing by, He saw a man blind from birth,
Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
2 and His disciples asked Him, saying, “Rabbi, who sinned, this one or his parents, that he should be born blind?”
Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
3 Jesus answered, “Neither this one sinned nor his parents, but that the works of God may be revealed in him;
Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
4 it is necessary for Me to be working the works of Him who sent Me while it is day; night comes when no one is able to work:
Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
5 when I am in the world, I AM [the] light of the world.”
Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
6 Saying these things, He spat on the ground, and made clay of the spittle, and rubbed the clay on the eyes of the blind man, and said to him,
Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
7 “Go away, wash at the pool of Siloam,” which is, interpreted, Sent. He went away, therefore, and washed, and came seeing;
Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
8 the neighbors, therefore, and those seeing him before, that he was blind, said, “Is this not he who is sitting and begging?”
Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
9 Others said, “This is he”; and others, “He is like to him”; he himself said, “I am [he].”
Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
10 They said, therefore, to him, “How were your eyes opened?”
Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
11 He answered and said, “A man called Jesus made clay, and rubbed my eyes, and said to me, Go away to the pool of Siloam, and wash; and having gone away and having washed, I received sight”;
Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
12 they said, therefore, to him, “Where is that One?” He says, “I have not known.”
Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
13 They bring him who once [was] blind to the Pharisees,
Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
14 and it was a Sabbath when Jesus made the clay, and opened his eyes.
Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
15 Again, therefore, the Pharisees also were asking him how he received sight, and he said to them, “He put clay on my eyes, and I washed—and I see.”
Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
16 Certain of the Pharisees therefore said, “This Man is not from God, because He does not keep the Sabbath”; others said, “How is a man—a sinful one—able to do such signs?” And there was a division among them.
Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
17 They said to the blind man again, “You—what do you say of Him—that He opened your eyes?”
Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
18 And he said, “He is a prophet.” The Jews, therefore, did not believe concerning him that he was blind and received sight, until they called the parents of him who received sight,
Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
19 and they asked them, saying, “Is [this] your son, of whom you say that he was born blind? How then does he now see?”
Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
20 His parents answered them and said, “We have known that this is our son, and that he was born blind;
Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
21 and how he now sees, we have not known; or who opened his eyes, we have not known; he is of age, ask him; he himself will speak concerning himself.”
Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
22 His parents said these things, because they were afraid of the Jews, for the Jews had already agreed together, that if anyone may confess Him—Christ, he may be put out of the synagogue;
Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
23 because of this his parents said, “He is of age, ask him.”
Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
24 They called, therefore, the man who was blind a second time, and they said to him, “Give glory to God, we have known that this Man is a sinner”;
Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
25 he answered, therefore, and said, “If He is a sinner—I have not known, one thing I have known, that, being blind, now I see.”
Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
26 And they said to him again, “What did He do to you? How did He open your eyes?”
Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
27 He answered them, “I told you already, and you did not hear; why do you wish to hear [it] again? Do you also wish to become His disciples?”
Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
28 They reviled him, therefore, and said, “You are His disciple, and we are Moses’ disciples;
Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
29 we have known that God has spoken to Moses, but this One—we have not known where He is from.”
Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
30 The man answered and said to them, “Why, in this is a wonderful thing, that you have not known where He is from, and He opened my eyes!
Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
31 And we have known that God does not hear sinners, but if anyone may be a worshiper of God, and may do His will, He hears him;
Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
32 from the age it was not heard that anyone opened eyes of one who has been born blind; (aiōn )
Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn )
33 if this One were not from God, He were not able to do anything.”
Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
34 They answered and said to him, “In sins you were born altogether, and you teach us?” And they cast him forth outside.
Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
35 Jesus heard that they cast him forth outside, and having found him, He said to him, “Do you believe in the Son of God?”
Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
36 He answered and said, “Who is He, Lord, that I may believe in Him?”
Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
37 And Jesus said to him, “You have both seen Him, and He who is speaking with you is He”;
Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
38 and he said, “I believe, Lord,” and worshiped Him.
Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
39 And Jesus said, “I came to this world for judgment, that those not seeing may see, and those seeing may become blind.”
Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
40 And those of the Pharisees who were with Him heard these things, and they said to Him, “Are we also blind?”
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
41 Jesus said to them, “If you were blind, you were not having had sin, but now you say—We see, therefore your sin remains.”
Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.