< John 8 >
1 And at dawn He came again to the temple [courts],
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Yesu alienda mlima wa Mizeituni.
2 and all the people were coming to Him, and having sat down, He was teaching them;
Mapema asubuhi akaja tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; akakaa na kuwafundisha.
3 and the scribes and the Pharisees bring to Him a woman having been taken in adultery, and having set her in the midst,
Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha kuzini. Wakamweka katikati.
4 they say to Him, “Teacher, this woman was taken in the very crime [of] committing adultery,
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Ndipo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, mwanamke huyu amekamatwa katika uzinzi, katika kitendo kabisa.
5 and in the Law, Moses commanded us that such be stoned; You, therefore, what do You say?”
Sasa, katika sheria, Musa ametuamuru kuwaponda mawe watu kama hawa, unasemaje juu yake?
6 And this they said, trying Him, that they might have to accuse Him. And Jesus, having stooped down, with the finger He was writing on the ground,
Walisema haya ili kumtega ili kwamba wapate jambo la kumshitaki, lakini Yesu akainama chini akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
7 and when they continued asking Him, having bent Himself back, He said to them, “The sinless of you—let him cast the first stone at her”;
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Walipoendelea kumwuliza, alisimama na kuwaambia, “Yeye asiyekuwa na dhambi miongoni mwenu, awe wa kwanza kumponda mawe.”
8 and again having stooped down, He was writing on the ground,
Akainama tena chini, akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
9 and they having heard, and being convicted by the conscience, were going forth one by one, having begun from the elders—to the last; and Jesus was left alone, and the woman standing in the midst.
(Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Waliposikia hayo, waliondoka mmoja baada ya mwingine, kuanzia aliye mzee. Mwishowe Yesu aliachwa peke yake, pamoja na mwanamke aliyekuwa katikati yao.
10 And Jesus having bent Himself back, and having seen no one but the woman, said to her, “Woman, where are those—your accusers? Did no one pass sentence on you?”
Yesu alisimama na kumwambia, “Mwanamke, waliokushitaki wako wapi? Hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
11 And she said, “No one, Lord”; and Jesus said to her, “Neither do I pass sentence on you; be going on, and sin no more.”]]
Akasema, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda njia yako; kuanzia sasa na kuendelea usitende dhambi tena.”
12 Again, therefore, Jesus spoke to them, saying, “I AM the light of the world; he who is following Me will not walk in the darkness, but he will have the light of life.”
Tena Yesu akazungumza na watu akisema, “Mimi ni nuru ya ulimwengu; yeye anifuataye hatatembea gizani bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 The Pharisees, therefore, said to Him, “You testify of Yourself, Your testimony is not true”;
Mafarisayo wakamwambia, “Unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako siyo wa kweli.”
14 Jesus answered and said to them, “And if I testify of Myself—My testimony is true, because I have known from where I came, and to where I go, and you have not known from where I come, or to where I go.
Yesu alijibu akawaambia, “Hata kama nitajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli. Ninajua mahali nilikotoka na kule ninakoenda, lakini ninyi hamjui mahali ninapotoka au kule ninakoenda.
15 You judge according to the flesh; I do not judge anyone,
Nyinyi mnahukumu kimwili; mimi simhukumu yeyote.
16 and even if I do judge My judgment is true, because I am not alone, but I and the Father who sent Me;
Mimi hata nikihukumu, hukumu yangu ni kweli kwa sababu siko peke yangu, bali niko pamoja na baba aliyenituma.
17 and also in your law it has been written that the testimony of two men is true;
Ndiyo, na katika sheria yenu imeandikwa kwamba ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
18 I am [One] who is testifying of Myself, and the Father who sent Me testifies of Me.”
Mimi ndiye ninayejishuhudia, na Baba aliyenituma ananishuhudia.”
19 They said, therefore, to Him, “Where is Your father?” Jesus answered, “You have neither known Me nor My Father: if you had known Me, you had also known My Father.”
Wakamwambia, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu, “mimi hamnijui wala Baba yangu hammjui; mngelikuwa mnanijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
20 Jesus spoke these sayings in the treasury, teaching in the temple, and no one seized Him, because His hour had not yet come;
Alisema maneno haya akiwa karibu na hazina alipokuwa akifundisha hekaluni, na hakuna hata mmoja aliyemkamata kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
21 therefore Jesus said again to them, “I go away, and you will seek Me, and you will die in your sin; to where I go away, you are not able to come.”
Basi akawaambia tena, “Ninaenda zangu; mtanitafuta na mtakufa katika dhambi zenu. Kule niendako, hamuwezi kuja.”
22 The Jews, therefore, said, “Will He kill Himself, because He says, To where I go away, you are not able to come?”
Wayahudi wakasema, “Atajiua mwenyewe, yeye ambaye alisema, 'kule niendako hamuwezi kuja'?”
23 And He said to them, “You are from beneath, I am from above; you are of this world, I am not of this world;
Yesu akawaambia, “Mnatoka chini; mimi natoka juu. Ninyi ni wa Ulimwengu huu; mimi si wa ulimwengu huu.
24 I said, therefore, to you, that you will die in your sins, for if you may not believe that I AM, you will die in your sins.”
Kwa hiyo, naliwaambieni kuwa mtakufa katika dhambi zenu. Vinginevyo muamini kuwa MIMI NDIYE, mtakufa katika dhambi zenu”.
25 They said, therefore, to Him, “You—who are You?” And Jesus said to them, “Even what I spoke of to you at the beginning;
Kwa hiyo wakamwambia, “Wewe ni nani?” Yesu akawaambia, Yale niliyowaambia tangu mwanzo.
26 many things I have to speak concerning you and to judge, but He who sent Me is true, and I—what things I heard from Him—these I say to the world.”
Ninayo mambo mengi ya kuzungumza na kuhukumu juu yenu. Hata hivyo, yeye aliyenituma ni wa kweli; na mambo niliyoyasikia kutoka kwake, mambo haya nayasema kwa Ulimwengu.”
27 They did not know that He spoke to them of the Father;
Hawakumuelewa kwamba alikuwa akiongea nao kuhusu Baba.
28 Jesus, therefore, said to them, “When you may lift up the Son of Man then you will know that I AM; and I do nothing of Myself, but according as My Father taught Me, these things I speak;
Yesu akasema, “Mtakapomwinua juu Mwana wa Mtu, ndipo mtakapojua kuwa MIMI NDIYE, na kwamba sifanyi lolote kwa nafsi yangu. Kama Baba alivyonifundisha, ninazungumza mambo haya.
29 and He who sent Me is with Me; the Father did not leave Me alone, because I always do the things pleasing to Him.”
Yeye aliyenituma yuko pamoja nami, na yeye hajaniacha peke yangu, kwani kila mara nafanya yale yanayompendeza.”
30 As He is speaking these things, many believed in Him;
Wakati Yesu akisema mambo haya, wengi walimwamini.
31 Jesus, therefore, said to the Jews who believed in Him, “If you may remain in My word, you are truly My disciples,
Yesu akasema kwa wale Wayahudi waliomwamini, “Ikiwa mtakaa katika neno langu, ndipo mtakuwa wanafunzi wangu kweli,
32 and you will know the truth, and the truth will make you free.”
nanyi mtaijua kweli, na kweli itawaweka huru.”
33 They answered Him, “We are seed of Abraham; and we have been servants to no one at any time; how do You say—You will become free?”
Walimjibu, “Sisi ni uzao wa Ibrahimu na kamwe hatujawahi kwa chini ya utumwa wa yeyote; utasemaje, “Tutawekwa huru?”
34 Jesus answered them, “Truly, truly, I say to you, everyone who is committing sin, is a servant of sin,
Yesu aliwajibu, “Amini, amini, nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 and the servant does not remain in the house—throughout the age, the Son remains—throughout the age; (aiōn )
Mtumwa hakai nyumbani wakati wote; mwana hudumu siku zote. (aiōn )
36 if then the Son may make you free, in reality you will be free.
Kwa hiyo, ikiwa Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kabisa.”
37 I have known that you are seed of Abraham, but you seek to kill Me, because My word has no place in you;
Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Ibrahimu; mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halina nafasi ndani yenu.
38 I speak that which I have seen with My Father, and you, therefore, do that which you have seen with your father.”
Ninasema mambo ambayo nimeyaona pamoja na Baba yangu, na ninyi vile vile mnafanya mambo ambayo mliyasikia kutoka kwa baba yenu.”
39 They answered and said to Him, “Our father is Abraham”; Jesus says to them, “If you were children of Abraham, the works of Abraham you were doing;
Walijibu na kumwambia, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, Kama mngelikuwa watoto wa Ibrahimu, mngefanya kazi za Ibrahimu.
40 and now, you seek to kill Me—a Man who has spoken to you the truth I heard from God; Abraham did not do this;
Hata sasa mnatafuta kuniua, mtu aliyewaambia ukweli kwamba nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya hivi.
41 you do the works of your father.” They said, therefore, to Him, “We have not been born of whoredom; we have one Father—God”;
Mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia, “Hatukuzaliwa katika uzinzi, tunaye Baba mmoja, Mungu.”
42 Jesus then said to them, “If God were your father, you were loving Me, for I came forth from God, and am come; for neither have I come of Myself, but He sent Me;
Yesu akawaambia, “Ikiwa Mungu ni Baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nimetoka kwa Mungu; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye alinituma.
43 why do you not know My speech? Because you are not able to hear My word.
Kwa nini hamyaelewi maneno yangu? Kwa sababu hamuwezi kuvumilia kuyasikia maneno yangu.
44 You are of a father—the Devil, and the desires of your father you will to do; he was a manslayer from the beginning, and he has not stood in the truth, because there is no truth in him; when one may speak the falsehood, he speaks of his own, because he is a liar—also his father.
Ninyi ni wa baba yenu, shetani, na mnataka kuzitenda tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo na hawezi kusimama katika kweli kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anapoongea uongo, anaongea kutoka kwenye asili yake kwa sababu ni mwongo na baba wa uongo.
45 And because I say the truth, you do not believe Me.
Hata sasa, kwa sababu ninasema iliyo kweli, hamniamini.
46 Who of you convicts Me of sin? And if I speak truth, why do you not believe Me?
Ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi? ikiwa ninasema iliyo kweli, kwa nini hamniamini?
47 He who is of God, he hears the sayings of God; because of this you do not hear, because you are not of God.”
Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; ninyi hamyasikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
48 The Jews, therefore, answered and said to Him, “Do we not say well, that You are a Samaritan, and have a demon?”
Wayahudi wakamjibu na kumwambia, hatujasema kweli kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?”
49 Jesus answered, “I do not have a demon, but I honor My Father, and you dishonor Me;
Yesu akajibu, sina pepo; lakini namheshimu Baba yangu, nanyi hamniheshimu.
50 and I do not seek My own glory; there is [One] who is seeking and is judging;
Sitafuti utukufu wangu; kuna mmoja atafutaye na kuhukumu.
51 truly, truly, I say to you, if anyone may keep My word, he may not see death—throughout the age.” (aiōn )
Amini, amini, nawaambia, iwapo yeyote atalishika neno langu, hataona mauti kamwe.” (aiōn )
52 The Jews, therefore, said to Him, “Now we have known that You have a demon; Abraham died, and the prophets, and You say, If anyone may keep My word, he will not taste of death—throughout the age! (aiōn )
Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kuwa una pepo. Abrahamu na mabii walikufa; lakini unasema, 'Ikiwa mtu atalishika neno langu, hataonja mauti'. (aiōn )
53 Are You greater than our father Abraham, who died? And the prophets died; whom do You make Yourself?”
Wewe si mkuu kuliko baba yetu Abrahamu aliyekufa, sivyo? Manabii pia walikufa. Wewe wajifanya kuwa nani?”
54 Jesus answered, “If I glorify Myself, My glory is nothing; it is My Father who is glorifying Me, of whom you say that He is your God;
Yesu akajibu, “Ikiwa nitajitukuza mwenyewe, utukufu wangu ni bure; ni Baba yangu anayenitukuza - yule mnayemsema kuwa ni Mungu wenu.
55 and you have not known Him, and I have known Him, and if I say that I have not known Him, I will be like you—speaking falsely; but I have known Him, and I keep His word;
Ninyi hamjamjua yeye, lakini mimi namjua yeye. Ikiwa nitasema, 'simjui,' nitakuwa kama nyinyi, muongo. Hata hivyo, ninamjua na maneno yake nimeyashika.
56 your father Abraham was glad that he might see My day; and he saw, and rejoiced.”
Baba yenu Abrahamu alishangilia atakavyoiona siku yangu; aliiona na alifurahi.”
57 The Jews, therefore, said to Him, “You are not yet fifty years old, and You have seen Abraham?”
Wayahudi wakamwambia,”Haujafikisha umri wa miaka hamsini bado, nawe umemuona Ibrahimu?”
58 Jesus said to them, “Truly, truly, I say to you, before Abraham’s coming—I AM”;
Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, MIMI NIKO.”
59 they took up, therefore, stones that they may cast at Him, but Jesus hid Himself, and went forth out of the temple, going through the midst of them, and so passed by.
Ndipo waliokota mawe wapate kumpiga, lakini Yesu alijificha na akatoka nje ya hekalu.