< John 4 >
1 When therefore the LORD knew that the Pharisees heard that Jesus makes and immerses more disciples than John,
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (though indeed Jesus Himself was not immersing, but His disciples),
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 He left Judea and went away again to Galilee,
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 and it was necessary [for] Him to go through Samaria.
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 He comes, therefore, to a city of Samaria, called Sychar, near to the place that Jacob gave to his son Joseph;
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 and there was there a well of Jacob. Jesus therefore having been weary from the journeying, was thus sitting on the well; it was as it were the sixth hour;
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 there comes a woman out of Samaria to draw water. Jesus says to her, “Give Me to drink”;
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 for His disciples were gone away into the city that they may buy food;
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 the Samaritan woman therefore says to Him, “How do You, being a Jew, ask drink from me, being a Samaritan woman?” For Jews have no dealing with Samaritans.
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 Jesus answered and said to her, “If you had known the gift of God, and who it is who is saying to you, Give Me to drink, you would have asked Him, and He would have given you living water.”
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 The woman says to Him, “Lord, You do not even have a vessel to draw with, and the well is deep; from where, then, have You the living water?
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Are You greater than our father Jacob, who gave us the well, and himself drank out of it, and his sons, and his livestock?”
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 Jesus answered and said to her, “Everyone who is drinking of this water will thirst again;
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but whoever may drink of the water that I will give him, may not thirst—throughout the age; and the water that I will give him will become in him a well of water, springing up to continuous life.” (aiōn , aiōnios )
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn , aiōnios )
15 The woman says to Him, “Lord, give me this water, that I may not thirst, nor come here to draw.”
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 Jesus says to her, “Go, call your husband, and come here”;
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 the woman answered and said, “I do not have a husband.” Jesus says to her, “Well did you say—I do not have a husband;
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 for you have had five husbands, and now, he whom you have is not your husband; you have said this correctly.”
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 The woman says to Him, “Lord, I perceive that You are a prophet;
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 our fathers worshiped in this mountain, and You say that in Jerusalem is the place where it is required to worship.”
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 Jesus says to her, “Woman, believe Me, that there comes an hour when neither in this mountain, nor in Jerusalem, will you worship the Father;
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 you worship what you have not known; we worship what we have known, because salvation is of the Jews;
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 but there comes an hour, and it now is, when the true worshipers will worship the Father in spirit and truth, for the Father also seeks such to worship Him;
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God [is] Spirit, and those worshiping Him should worship in spirit and truth.”
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 The woman says to Him, “I have known that Messiah comes, who is called Christ, when that One may come, He will tell us all things”;
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Jesus says to her, “I who am speaking to you am [He].”
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 And on this came His disciples, and were wondering that He was speaking with a woman, no one, however, said, “What do You seek?” Or “Why do You speak with her?”
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 The woman then left her water-jug and went away into the city, and says to the men,
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 “Come, see a Man who told me all things—as many as I did; is this the Christ?”
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 They went forth therefore out of the city, and were coming to Him.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 And in the meanwhile His disciples were asking Him, saying, “Rabbi, eat”;
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 and He said to them, “I have food to eat that you have not known.”
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 The disciples then said to one another, “Did anyone bring Him anything to eat?”
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 Jesus says to them, “My food is that I may do the will of Him who sent Me, and may finish His work;
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 do not say that it is yet four months, and the harvest comes; behold, I say to you, lift up your eyes, and see the fields, that they are white to harvest already.
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 And he who is reaping receives a reward, and gathers fruit to continuous life, that both he who is sowing and he who is reaping may rejoice together; (aiōnios )
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios )
37 for in this the saying is the true one, that one is the sower and another the reaper.
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 I sent you to reap on that which you have not labored; others labored, and you have entered into their labor.”
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 And many from that city believed in Him, of the Samaritans, because of the word of the woman testifying, “He told me all things—as many as I did.”
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 When, then, the Samaritans came to Him, they were asking Him to remain with them, and He remained there two days;
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 and many more believed because of His word,
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 and said to the woman, “We no longer believe because of your speaking; for we ourselves have heard and known that this is truly the Savior of the world—the Christ.”
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 And after the two days He went forth from there, and went away to Galilee,
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 for Jesus Himself testified that a prophet will not have honor in his own country;
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 when then, He came to Galilee, the Galileans received Him, having seen all things that He did in Jerusalem in the celebration—for they also went to the celebration.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 Jesus came, therefore, again to Cana of Galilee, where He made the water wine, and there was a certain attendant, whose son was ailing in Capernaum,
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 he, having heard that Jesus comes out of Judea to Galilee, went away to Him, and was asking Him that He may come down and may heal his son, for he was about to die.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Jesus then said to him, “If you may not see signs and wonders, you will not believe.”
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 The attendant says to Him, “Lord, come down before my child dies”;
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 Jesus says to him, “Be going on; your son lives.” And the man believed the word that Jesus said to him, and was going on,
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 and he now going down, his servants met him, and told, saying, “Your child lives”;
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 he inquired then of them the hour in which he became better, and they said to him, “Yesterday at the seventh hour the fever left him”;
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 then the father knew that [it was] in that hour in which Jesus said to him, “Your son lives,” and he himself believed, and his whole house;
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 this again [was] a second sign Jesus did, having come out of Judea to Galilee.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.