< John 2 >

1 And [on] the third day a wedding happened in Cana of Galilee, and the mother of Jesus was there,
Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
2 and also Jesus was called, and His disciples, to the wedding;
Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
3 and wine having failed, the mother of Jesus says to Him, “They have no wine”;
Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
4 Jesus says to her, “What [is that] to Me and to you, woman? My hour is not yet come.”
Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
5 His mother says to the servants, “Whatever He may say to you—do.”
Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
6 And there were six water-jugs of stone there, placed according to the purifying of the Jews, holding each two or three measures.
Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
7 Jesus says to them, “Fill the water-jugs with water”; and they filled them—to the brim;
Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
8 and He says to them, “Draw out, now, and carry to the headwaiter”; and they bore.
Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
9 And as the headwaiter tasted the water become wine, and did not know where it is from (but the servants knew, who have drawn the water), the headwaiter calls the bridegroom,
Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
10 and says to him, “Every man, at first, sets forth the good wine; and when they may have drunk freely, then the inferior; you kept the good wine until now.”
kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
11 This [is the] beginning of the signs Jesus did in Cana of Galilee, and revealed His glory, and His disciples believed in Him;
Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
12 after this He went down to Capernaum, He, and His mother, and His brothers, and His disciples; and they did not remain there many days.
Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
13 And the Passover of the Jews was near, and Jesus went up to Jerusalem,
Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14 and He found in the temple those selling oxen, and sheep, and doves, and the money-changers sitting,
Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
15 and having made a whip of small cords, He put all forth out of the temple, also the sheep, and the oxen; and He poured out the coins of the money-changers, and He overthrew the tables,
Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
16 and He said to those selling the doves, “Take these things from here; do not make the house of My Father a house of merchandise.”
Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
17 And His disciples remembered that it is written: “The zeal of Your house ate Me up”;
Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
18 the Jews then answered and said to Him, “What sign do You show to us—that You do these things?”
Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
19 Jesus answered and said to them, “Destroy this temple, and in three days I will raise it up.”
Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
20 The Jews, therefore, said, “This temple was built [in] forty-six years, and will You raise it up in three days?”
Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
21 But He spoke concerning the temple of His body;
Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
22 when, then, He was raised out of the dead, His disciples remembered that He said this to them, and they believed the Writing, and the word that Jesus said.
Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
23 And as He was in Jerusalem, in the Passover, in the celebration, many believed in His Name, beholding His signs that He was doing;
Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
24 and Jesus Himself was not trusting Himself to them, because of His knowing all [men],
Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
25 and because He had no need that any should testify concerning man, for He Himself was knowing what was in man.
Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.

< John 2 >