< Job 8 >
1 And Bildad the Shuhite answers and says:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 “Until when do you speak these things? And a strong wind—sayings of your mouth?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Does God pervert judgment? And does the Mighty One pervert justice?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 If your sons have sinned before Him, And He sends them away, By the hand of their transgression,
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 If you seek for God early, And make supplication to the Mighty,
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 If you [are] pure and upright, Surely now He wakes for you, And has completed The habitation of your righteousness.
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 And your beginning has been small, And your latter end is very great.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 For inquire, please, of a former generation, And prepare for a search of their fathers,
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 For we [are] of yesterday, and we do not know, For our days [are] a shadow on earth.
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Do they not show you—speak to you, And from their heart bring forth words?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Does a rush rise without a marsh? A reed increase without water?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 While it [is] in its budding—uncropped, Even before any herb it withers.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 So [are] the paths of all forgetting God, And the hope of the profane perishes,
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Whose confidence is loathsome, And the house of a spider his trust.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 He leans on his house—and it does not stand, He takes hold on it—and it does not abide.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 He [is] green before the sun, And over his garden his branch goes out.
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 His roots are wrapped by a heap, He looks for a house of stones.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 If [one] destroys him from his place, Then it has feigned concerning him, I have not seen you!
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Behold, this [is] the joy of His way, And from the dust others spring up.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Behold, God does not reject the perfect, Nor takes hold on the hand of evildoers.
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 While He fills your mouth with laughter, And your lips with shouting,
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Those hating you put on shame, And the tent of the wicked is not!”
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.