< Job 40 >
1 And YHWH answers Job and says:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 “Is the striver with the Mighty instructed? The reprover of God, let him answer it.”
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 And Job answers YHWH and says:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 “Behold, I have been vile, What do I return to You? I have placed my hand on my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 I have spoken once, and I do not answer, And twice, and I do not add.”
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 And YHWH answers Job out of the whirlwind and says:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 “Now gird your loins as a man, I ask you, and you cause Me to know.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Do you also make My judgment void? Do you condemn Me, That you may be righteous?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 And do you have an arm like God? And do you thunder with a voice like His?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Now put on excellence and loftiness, Indeed, put on splendor and beauty.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Scatter abroad the wrath of your anger, And see every proud one, and make him low.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 See every proud one—humble him, And tread down the wicked in their place.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together, Bind their faces in secret.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 And even I praise you, For your right hand gives salvation to you.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Now behold, behemoth, That I made with you: He eats grass as an ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Now behold, his power [is] in his loins, And his strength in the muscles of his belly.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He bends his tail as a cedar, The sinews of his thighs are wrapped together,
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones [are] tubes of bronze, His bones [are] as a bar of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He [is] a beginning of the ways of God, His Maker [alone] brings His sword near;
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 For mountains bear food for him, And all the beasts of the field play there.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He lies down under shades, In a secret place of reed and marsh.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Shades cover him, [with] their shadow, Willows of the brook cover him.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Behold, a flood oppresses—he does not hurry, He is confident though Jordan Comes forth to his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Does [one] take him by his eyes? Does [one] pierce the nose with snares?”
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?