< Job 38 >

1 And YHWH answers Job out of the whirlwind and says:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 “Who [is] this—darkening counsel, By words without knowledge?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Now gird your loins as a man, And I ask you, and you cause Me to know.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Where were you when I founded the earth? Declare, if you have known understanding.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Who placed its measures—if you know? Or who has stretched out a line on it?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 On what have its sockets been sunk? Or who has cast its cornerstone—
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 In the singing together of [the] stars of morning, When all [the] sons of God shout for joy?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 And He shuts up the sea with doors, In its coming forth, it goes out from the womb.
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 In My making a cloud its clothing, And thick darkness its swaddling band,
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 And I measure My statute over it, And place bar and doors,
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 And say, To here you come, and no more, And a command is placed On the pride of your billows.
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Have you commanded morning since your days? Do you cause the dawn to know its place?
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 To take hold on the skirts of the earth, And the wicked are shaken out of it,
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 It turns itself as clay of a seal And they station themselves as clothed.
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 And their light is withheld from the wicked, And the arm lifted up is broken.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Have you come to springs of the sea? And in searching the deep Have you walked up and down?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Were the gates of death revealed to you? And do you see the gates of death-shade?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 You have understanding, Even to the broad places of earth! Declare—if you have known it all.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Where [is] this—the way light dwells? And darkness, where [is] this—its place?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 That you take it to its boundary, And that you understand the paths of its house.
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 You have known—for then you are born, And the number of your days [are] many!
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Have you come to the treasure of snow? Indeed, do you see the treasures of hail,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 That I have kept back for a time of distress, For a day of conflict and battle?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 Where [is] this, the way light is apportioned? It scatters an east wind over the earth.
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Who has divided a conduit for the flood? And a way for the lightning of the voices?
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 To cause [it] to rain on a land [with] no man, A wilderness [with] no man in it.
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 To satisfy a desolate and ruined place, And to cause to shoot up The produce of the tender grass?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Does the rain have a father? Or who has begotten the drops of dew?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 From whose belly came forth the ice? And the hoarfrost of the heavens, Who has begotten it?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Waters are hidden as a stone, And the face of the deep is captured.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Do you bind the chains of the Pleiades? Or do you open the cords of Orion?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Do you bring out the twelve signs in [their] season? And do you comfort the Great Bear over her sons?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Have you known the statutes of the heavens? Or do you appoint Its dominion in the earth?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Do you lift up your voice to the cloud, And abundance of water covers you?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Do you send out lightnings, and they go And say to you, Behold us?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Who has put wisdom in the inward parts? Or who has given understanding to the covered part?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Who numbers the clouds by wisdom? And the bottles of the heavens, Who causes to lie down,
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 In the hardening of dust into hardness, And clods cleave together?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Do you hunt prey for a lion? And fulfill the desire of young lions?
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 When they bow down in dens—Abide in a thicket for a covert?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Who prepares for a raven his provision, When his young ones cry to God? They wander without food.”
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< Job 38 >