< Job 37 >

1 “Also, my heart trembles at this, And it moves from its place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Listen diligently to the trembling of His voice, Indeed, the sound goes forth from His mouth.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He directs it under the whole heavens, And its light [is] over the skirts of the earth.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 A voice roars after it—He thunders with the voice of His excellence, And He does not hold them back, When His voice is heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God thunders with His voice wonderfully, Doing great things and we do not know.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For He says to snow: Be [on] the earth. And the small rain and great rain of His power.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Into the hand of every man he seals, For the knowledge by all men of His work.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 And the beast enters into [its] lair, And it continues in its habitations.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 From the inner chamber comes a windstorm, And from scatterings winds—cold,
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 From the breath of God is frost given, And the breadth of waters is constricted,
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Indeed, by filling He presses out a cloud, [and] His light scatters a cloud.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 And it is turning itself around by His counsels, For their doing all He commands them, On the face of the habitable earth.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Whether for a rod, or for His land, Or for kindness—He causes it to come.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Hear this, O Job, Stand and consider the wonders of God.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Do you know when God places them, And caused the light of His cloud to shine?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Do you know the balancings of a cloud? The wonders of the Perfect in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 How your garments [are] warm, In the quieting of the earth from the south?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 You have made an expanse with Him For the clouds—strong as a hard mirror!
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Let us know what we say to Him, We do not set in array because of darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Is it declared to Him that I speak? If a man has spoken, surely he is swallowed up.
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 And now, they have not seen the light, It [is] bright in the clouds, And the wind has passed by and cleanses them.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 It comes from the golden north, Fearful splendor [is] beside God.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 The Mighty! We have not found Him out, High in power and judgment, He does not answer! And abundant in righteousness,
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Therefore men fear Him, He does not see any of the wise of heart.”
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >