< Job 36 >
1 And Elihu adds and says:
Elihu aliendelea na kusema,
2 “Honor me a little, and I show you, That yet for God [are] words.
“Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 I lift up my knowledge from afar, And I ascribe righteousness to my Maker.
Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
4 For my words [are] truly not false, The perfect in knowledge [is] with you.
Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
5 Behold, God [is] mighty, and does not despise, Mighty [in] power [and] heart.
Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
6 He does not revive the wicked, And appoints the judgment of the poor;
Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
7 He does not withdraw His eyes from the righteous, And [from] kings on the throne, And causes them to sit forever, and they are high,
Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
8 And if prisoners in chains They are captured with cords of affliction,
Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
9 Then He declares to them their work, And their transgressions, Because they have become mighty,
kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
10 And He uncovers their ear for instruction, And commands that they turn back from iniquity.
Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
11 If they hear and serve, They complete their days in good, And their years in pleasantness.
Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
12 And if they do not listen, They pass away by the dart, And expire without knowledge.
Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
13 And the profane in heart set the face, They do not cry when He has bound them.
Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
14 Their soul dies in youth, And their life among the defiled.
Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
15 He draws out the afflicted in his affliction, And uncovers their ear in oppression.
Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
16 And He also moved you from a narrow place [To] a broad place—no constriction under it, And the sitting beyond of your table has been full of fatness.
Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
17 And you have fulfilled the judgment of the wicked, Judgment and justice are upheld because of fury,
Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
18 Lest He move you with a stroke, And the abundance of an atonement not turn you aside.
Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
19 Does He value your riches? He has gold, and all the forces of power.
Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
20 Do not desire the night, For the going up of peoples in their stead.
Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
21 Take heed—do not turn to iniquity, For you have fixed on this Rather than [on] affliction.
Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
22 Behold, God sits on high by His power, Who [is] like Him—a teacher?
Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who has appointed to Him His way? And who said, You have done iniquity?
Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
24 Remember that you magnify His work That men have beheld.
Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
25 All men have looked on it, Man looks attentively from afar.
Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
26 Behold, God [is] high, And we do not know the number of His years, Indeed, there [is] no searching.
Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
27 When He diminishes droppings of the waters, They refine rain according to its vapor,
Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
28 Which clouds drop, They distill on man abundantly.
ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
29 Indeed, do [any] understand The spreadings out of a cloud? The noises of His dwelling place?
Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
30 Behold, He has spread His light over it, And He has covered the roots of the sea,
Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
31 For He judges peoples by them, He gives food in abundance.
Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
32 By two palms He has covered the light, And lays a charge over it in meeting,
Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
33 His shout shows it, The livestock also, the rising [storm].”
Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.