< Job 36 >

1 And Elihu adds and says:
Elihu akaendelea kusema:
2 “Honor me a little, and I show you, That yet for God [are] words.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 I lift up my knowledge from afar, And I ascribe righteousness to my Maker.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 For my words [are] truly not false, The perfect in knowledge [is] with you.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Behold, God [is] mighty, and does not despise, Mighty [in] power [and] heart.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 He does not revive the wicked, And appoints the judgment of the poor;
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 He does not withdraw His eyes from the righteous, And [from] kings on the throne, And causes them to sit forever, and they are high,
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 And if prisoners in chains They are captured with cords of affliction,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 Then He declares to them their work, And their transgressions, Because they have become mighty,
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 And He uncovers their ear for instruction, And commands that they turn back from iniquity.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 If they hear and serve, They complete their days in good, And their years in pleasantness.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 And if they do not listen, They pass away by the dart, And expire without knowledge.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 And the profane in heart set the face, They do not cry when He has bound them.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Their soul dies in youth, And their life among the defiled.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 He draws out the afflicted in his affliction, And uncovers their ear in oppression.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 And He also moved you from a narrow place [To] a broad place—no constriction under it, And the sitting beyond of your table has been full of fatness.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 And you have fulfilled the judgment of the wicked, Judgment and justice are upheld because of fury,
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Lest He move you with a stroke, And the abundance of an atonement not turn you aside.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Does He value your riches? He has gold, and all the forces of power.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Do not desire the night, For the going up of peoples in their stead.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Take heed—do not turn to iniquity, For you have fixed on this Rather than [on] affliction.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Behold, God sits on high by His power, Who [is] like Him—a teacher?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who has appointed to Him His way? And who said, You have done iniquity?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Remember that you magnify His work That men have beheld.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 All men have looked on it, Man looks attentively from afar.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Behold, God [is] high, And we do not know the number of His years, Indeed, there [is] no searching.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 When He diminishes droppings of the waters, They refine rain according to its vapor,
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Which clouds drop, They distill on man abundantly.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Indeed, do [any] understand The spreadings out of a cloud? The noises of His dwelling place?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Behold, He has spread His light over it, And He has covered the roots of the sea,
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 For He judges peoples by them, He gives food in abundance.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 By two palms He has covered the light, And lays a charge over it in meeting,
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 His shout shows it, The livestock also, the rising [storm].”
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.

< Job 36 >