< Job 30 >
1 “And now, laughed at me, Have the younger in days than I, Whose fathers I have loathed to set With the dogs of my flock.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Also—the power of their hands, why [is it] to me? On them old age has perished.
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 With want and with harsh famine, They are gnawing a dry place [in] the recent night, [In] desolation and ruin,
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 Those cropping mallows near a shrub, And their food [is] root of broom trees.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 They are cast out from the midst (They shout against them as a thief),
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 To dwell in a frightful place of valleys, Holes of earth and clefts.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 They groan among shrubs, They are gathered together under nettles.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Sons of folly—even sons without name, They have been struck from the land.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 And now, I have been their song, And I am to them for a byword.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 They have detested me, They have kept far from me, And from before me have not spared to spit.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Because He loosed His cord and afflicts me, And the bridle from before me, They have cast away.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 A brood arises on the right hand, They have cast away my feet, And they raise up against me, Their paths of calamity.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 They have broken down my path, They profit by my calamity: He has no helper.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 They come as a wide breach, Under the desolation have rolled themselves.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 He has turned terrors against me, It pursues my abundance as the wind, And as a thick cloud, My safety has passed away.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 And now, in me my soul pours itself out, Days of affliction seize me.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 [At] night my bone has been pierced in me, And my gnawing [pain] does not lie down.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 By the abundance of power, Is my clothing changed, As the mouth of my coat it girds me.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Casting me into mire, And I have become like dust and ashes.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 I cry to You, And You do not answer me, I have stood, and You consider me.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 You are turned to be fierce to me, With the strength of Your hand, You oppress me.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 You lift me up, You cause me to ride on the wind, And You melt—You level me.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 For I have known You bring me back [to] death, And [to] the house appointed for all living.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Surely not against the heap Does He send forth the hand, Though they have safety in its ruin.
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 Did I not weep for him whose day is hard? My soul has grieved for the needy.
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 When I expected good, then comes evil, And I wait for light, and darkness comes.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 My bowels have boiled, and have not ceased, Days of affliction have gone before me.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 I have gone mourning without the sun, I have risen, I cry in an assembly.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 I have been a brother to dragons, And a companion to daughters of the ostrich.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 My skin has been black on me, And my bone has burned from heat,
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 And my harp becomes mourning, And my pipe the sound of weeping.”
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.