< Job 3 >

1 After this Job has opened his mouth, and reviles his day.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 And Job answers and says:
Kisha akasema:
3 “Let the day perish in which I am born, And the night that has said: A man-child has been conceived.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 That day—let it be darkness, Do not let God require it from above, Nor let light shine on it.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Let darkness and death-shade redeem it, Let a cloud dwell on it, Let them terrify it as the most bitter of days.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 That night—let thick darkness take it, Let it not be united to days of the year, Let it not come into the number of months.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Behold! That night—let it be barren, Let no singing come into it.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Let the cursers of day mark it, Who are ready to wake up Leviathan.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Let the stars of its twilight be dark, Let it wait for light, and there is none, And let it not look on the eyelids of the dawn.
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Because it has not shut the doors Of the womb that was mine! And hide misery from my eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why do I not die from the womb? I have come forth from the belly and gasp!
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why have knees been before me? And what [are] breasts, that I suck?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For now, I have lain down, and am quiet, I have slept—then there is rest to me,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 With kings and counselors of earth, These building ruins for themselves.
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Or with princes—they have gold, They are filling their houses [with] silver.
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 (Or I am not as a hidden abortion, As infants—they have not seen light.)
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There the wicked have ceased troubling, And there the wearied rest in power.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 Together prisoners have been at ease, They have not heard the voice of an exactor,
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Small and great [are] the same there. And a servant [is] free from his lord.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Why does He give light to the miserable, and life to the bitter soul?
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Who are waiting for death, and it is not, And they seek it above hid treasures.
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Who are glad—to joy, They rejoice when they find a grave.
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 To a man whose way has been hidden, And whom God shuts up?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For before my food, my sighing comes, And my roarings [are] poured out as waters.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For I feared a fear and it meets me, And what I was afraid of comes to me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I was not safe—nor was I quiet—Nor was I at rest—and trouble comes!”
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< Job 3 >