< Job 24 >
1 “For this reason from the Mighty One Times have not been hidden, And those knowing Him have not seen His days.
“Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu? Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?
2 They reach the borders, They have taken a drove away violently, Indeed, they do evil.
Watu husogeza mawe ya mpaka; huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.
3 They lead away the donkey of the fatherless, They take in pledge the ox of the widow,
Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.
4 They turn aside the needy from the way, Together have hid the poor of the earth.
Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.
5 Behold, wild donkeys in a wilderness, They have gone out about their work, Seeking early for prey, A mixture for himself—food for young ones.
Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
6 They reap his provender in a field, And they glean the vineyard of the wicked.
Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.
7 They cause the naked to lodge without clothing. And there is no covering in the cold.
Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.
8 From the inundation of hills they are wet, And without a refuge—have embraced a rock.
Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.
9 They take away violently The orphan from the breast, And they lay a pledge on the poor.
Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.
10 Naked, they have gone without clothing, And hungry—have taken away a sheaf.
Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.
11 They make oil between their walls, They have trodden winepresses, and thirst.
Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia; hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.
12 Men groan because of enmity, And the soul of pierced ones cries, And God does not give praise.
Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini, nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada. Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote kwa kutenda mabaya.
13 They have been those rebelling against light, They have not discerned His ways, Nor abided in His paths.
“Wako wale wanaoiasi nuru, wasiofahamu njia zake wala hawakai katika mapito yake.
14 The murderer rises at the light, He slays the poor and needy, And in the night he is as a thief.
Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka naye huwaua maskini na mhitaji; wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.
15 And the eye of an adulterer Has observed the twilight, Saying, No eye beholds me. And he puts the face in secret.
Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
16 He has dug in the darkness—houses; By day they shut themselves up, They have not known light.
Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
17 When together, morning [is] death-shade to them, When he discerns the terrors of death-shade.
Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
18 He [is] light on the face of the waters, Their portion is vilified in the earth, He does not turn the way of vineyards.
“Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
19 Drought—also heat—consume snow-waters, Sheol—[those who] have sinned. (Sheol )
Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol )
20 The womb forgets him, The worm sweetens [on] him, He is remembered no more, And wickedness is broken as a tree.
Tumbo lililowazaa huwasahau, nao huwa karamu ya mabuu; watu waovu hawakumbukwi tena, lakini huvunjika kama mti.
21 Treating evil the barren [who] does not bear, And he does no good [to] the widow,
Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto, nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.
22 And [God] has drawn the mighty by His power, He rises, and none believes in life.
Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake; ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.
23 He gives to him confidence, and he is supported, And His eyes [are] on their ways.
Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama, lakini macho yake yanaona njia zao.
24 They were high [for] a little, and they are not, And they have been brought low. They are shut up as all [others], And cut off as the head of an ear of grain.
Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka; hushushwa na kukusanywa kama wengine wote, hukatwa kama masuke ya nafaka.
25 And if not now, who proves me a liar, And makes my word of nothing?”
“Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo, na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”