< Job 17 >

1 “My spirit has been destroyed, My days extinguished—graves [are] for me.
Roho yangu imemezwa, na siku zangu zimekwisha; kaburi lipo tayari kwa ajili yangu mimi.
2 If not—mockeries [are] with me. And my eye lodges in their provocations.
Hakika kuna wenye mzaha pamoja nami; ni lazima daima jicho langu litazame kukasirisha kwao.
3 Now place my pledge with You; Who is he that strikes hand with me?
Nipe sasa ahadi, uwe uthibitisho kwangu mimi pamoja na wewe mwenyewe; nani mwingine yuko pale ambaye atanisaidia mimi?
4 For You have hidden their heart from understanding, Therefore You do not exalt them.
Kwa kuwa wewe Mungu umemeitunza mioyo yao kutoka katika ufahamu; kwa hiyo, wewe hautawaheshimisha wao juu yangu mimi.
5 For a portion he shows friendship, And the eyes of his sons are consumed.
Yeye ambaye huwapinga rafiki zake hadharani, kwa ajili ya tuzo, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
6 And He set me up for a proverb of the peoples, And I am a wonder before them.
Lakini amenifanya mimi kuwa neno la kuzungumziwa na watu; wao wananitemea mate katika uso wangu mimi.
7 And my eye is dim from sorrow, And my members—all of them—as a shadow.
Jicho langu pia halioni vizuri kwa sababu ya huzuni; sehemu zangu zote za mwili ni nyembamba kama vivuli.
8 The upright are astonished at this, and the innocent stirs himself up against the profane.
Watu wanyoofu watapendezwa na hiki; mtu asiye na hatia atajitia yeye mwenyewe juu ya kushindana dhidi ya watu wasiomcha Mungu.
9 And the righteous lays hold [on] his way, And the clean of hands adds strength.
Mtu mwenye haki ataendelea katika njia yake; yeye ambaye ana mikono iliyo safi ataendelea kuwa mwenye nguvu zaidi na zaidi.
10 But please return and come in, all of you, And I do not find a wise man among you.
Lakini kama ilivyo kwenu ninyi nyote, njooni sasa; Mimi sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu ninyi.
11 My days have passed by, My plans have been broken off, The possessions of my heart!
Siku zangu zimepita; mipango yangu imenyamazishwa na hivyo ni matumaini ya moyo wangu.
12 They appoint night for day, Light [is] near because of darkness.
Watu hawa, wenye kukejeli, badili usiku kuwa mchana; mchana uko karibu kuwa giza.
13 If I wait—Sheol [is] my house, In darkness I have spread out my bed. (Sheol h7585)
Tangu mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu; tangu Mimi nimetandaza kiti changu katika giza; (Sheol h7585)
14 To corruption I have called: You [are] my father. To the worm: My mother and my sister.
tangu Mimi nimesema na shimo 'Wewe ni baba yangu,' na kwa funza, 'Wewe ni mama yangu au dada yangu;
15 And where [is] my hope now? Indeed, my hope, who beholds it?
liko wapi tena tumaini langu? Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?
16 You go down [to] the parts of Sheol, If we may rest together on the dust.” (Sheol h7585)
Tumaini litakwenda pamoja na mimi katika milango ya Kuzimu wakati sisi tutakapokwenda katika mavumbi? (Sheol h7585)

< Job 17 >