< Job 14 >
1 “Man, born of woman! Of few days, and full of trouble!
Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
2 As a flower he has gone forth, and is cut off, And he flees as a shadow and does not stand.
Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
3 Also—on this You have opened Your eyes, and bring me into judgment with You.
Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
4 Who gives a clean thing out of an unclean? Not one.
Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
5 If his days are determined, The number of his months [are] with You, You have made his limit, And he does not pass over;
Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
6 Look away from off him that he may cease, Until he enjoy as a hired worker his day.
Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
7 For there is hope for a tree, if it is cut down, That it changes again, That its tender branch does not cease.
Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
8 If its root becomes old in the earth, And its stem dies in the dust,
Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
9 From the fragrance of water it flourishes, And has made a crop as a plant.
hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
10 And a man dies, and becomes weak, And man expires, and where [is] he?
Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
11 Waters have gone away from a sea, And a river becomes waste and dry.
Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
12 And man has lain down, and does not rise, Until the wearing out of the heavens they do not awaken, Nor are roused from their sleep.
vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
13 O that You would conceal me in Sheol, Hide me until the turning of Your anger, Set a limit for me, and remember me. (Sheol )
Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol )
14 If a man dies—does he revive? All [the] days of my warfare I wait, until my change comes.
Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
15 You call, and I answer You; To the work of Your hands You have desire.
Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
16 But now, You number my steps, You do not watch over my sin.
Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
17 My transgression [is] sealed up in a bag, and You sew up my iniquity.
Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
18 And yet, a falling mountain wastes away, and a rock is removed from its place.
Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
19 Waters have worn away stones, Their outpourings wash away the dust of earth, And You have destroyed the hope of man.
maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
20 You prevail [over] him forever, and he goes, He is changing his countenance, And You send him away.
Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
21 His sons are honored, and he does not know; And they are little, and he does not attend to them.
Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
22 Only—his flesh is pained for him, And his soul mourns for him.”
Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.