< Jeremiah 42 >
1 And they come near—all the heads of the forces, and Johanan son of Kareah, and Jezaniah son of Hoshaiah, and all the people from the least even to the greatest—
Ndipo maafisa wote wa jeshi, pamoja na Yohanani mwana wa Karea, na Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana wakamjia
2 and they say to Jeremiah the prophet, “Please let our supplication fall before you, and pray for us to your God YHWH for all this remnant; for we have been left a few out of many, as your eyes see us;
Yeremia nabii na kumwambia, “Tafadhali sikia maombi yetu na umwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watu hawa wote waliosalia. Kwa kuwa kama unavyoona sasa, ingawa wakati fulani tulikuwa wengi, sasa tumesalia wachache tu.
3 and your God YHWH declares to us the way in which we walk, and the thing that we do.”
Omba ili Bwana Mungu wako atuambie twende wapi na tufanye nini.”
4 And Jeremiah the prophet says to them, “I have heard: behold, I am praying to your God YHWH according to your words, and it has come to pass, the whole word that YHWH answers you, I declare to you—I do not withhold a word from you.”
Nabii Yeremia akajibu, “Nimewasikia. Kwa hakika nitamwomba Bwana Mungu wenu kama mlivyoomba. Nitawaambia kila kitu asemacho Bwana, wala sitawaficha chochote.”
5 And they have said to Jeremiah, “YHWH is against us for a true and faithful witness, if—according to all the word with which your God YHWH sends you to us—we do not do so.
Kisha wakamwambia Yeremia, “Bwana na awe shahidi wa kweli na mwaminifu kati yetu kama hatutafanya sawasawa na kila kitu Bwana Mungu wako atakachokutuma utuambie.
6 Whether [it is] good or evil, to the voice of our God YHWH, to whom we are sending you, we listen; because it is good for us when we listen to the voice of our God YHWH.”
Likiwa jema au likiwa baya, tutamtii Bwana Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yote yawe mema kwetu, kwa maana tutamtii Bwana Mungu wetu.”
7 And it comes to pass, at the end of ten days, that there is a word of YHWH to Jeremiah,
Baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
8 and he calls to Johanan son of Kareah, and to all the heads of the forces that [are] with him, and to all the people, from the least even to the greatest,
Kwa hiyo akawaita pamoja Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote kuanzia mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana.
9 and he says to them, “Thus said YHWH, God of Israel, to whom you sent me, to cause your supplication to fall before Him:
Akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kuwasilisha maombi yenu:
10 If you certainly dwell in this land, then I have built you up, and I do not throw down; and I have planted you, and I do not pluck up; for I have relented concerning the calamity that I have done to you.
‘Kama mkikaa katika nchi hii, nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, kwani ninahuzunishwa na maafa niliyowapiga nayo.
11 Do not be afraid of the king of Babylon, whom you are afraid of; do not be afraid of him—a declaration of YHWH—for I [am] with you, to save you, and to deliver you from his hand.
Msimwogope mfalme wa Babeli, ambaye sasa mnamwogopa. Msimwogope, asema Bwana, kwa kuwa niko pamoja nanyi, nami nitawaokoa na kuwaponya kutoka mikononi mwake.
12 And I give mercies to you, and he has pitied you, and caused you to return to your own ground.
Nitawaonea huruma ili naye awe na huruma nanyi na kuwarudisha katika nchi yenu.’
13 And if you are saying, We do not dwell in this land—not to listen to the voice of your God YHWH,
“Hata hivyo, kama mkisema, ‘Hatutakaa katika nchi hii,’ hivyo mkaacha kumtii Bwana Mungu wenu,
14 saying, No; but we enter the land of Egypt, that we see no war, and do not hear the sound of a horn, and are not hungry for bread; and we dwell there—
nanyi kama mkisema, ‘Hapana, tutakwenda kuishi Misri, mahali ambapo hatutaona vita au kusikia sauti ya tarumbeta au kuwa na njaa ya chakula,’
15 And now, therefore, hear a word of YHWH, O remnant of Judah! Thus said YHWH of Hosts, God of Israel: If you really set your faces to enter Egypt, and have gone to sojourn there,
basi sikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Ikiwa mmekusudia kwenda Misri na kufanya makazi huko,
16 then it has come to pass, the sword that you are afraid of, overtakes you there, in the land of Egypt; and the hunger, because of which you are sorrowful, cleaves after you there in Egypt, and there you die.
basi ule upanga mnaouogopa utawapata huko, na njaa mnayoihofia itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.
17 Thus are all the men who have set their faces to enter Egypt to sojourn there; they die—by sword, by hunger, and by pestilence, and there is not a remnant and an escaped one to them, because of the calamity that I am bringing in on them;
Naam, wote waliokusudia kwenda kuishi Misri watakufa kwa upanga, njaa na tauni; hakuna hata mmoja wao atakayenusurika au kuokoka maafa nitakayoyaleta juu yao.’
18 for thus said YHWH of Hosts, God of Israel: As My anger and My fury have been poured out on the inhabitants of Jerusalem, so My fury is poured out on you in your entering Egypt, and you have been for an execration, and for an astonishment, and for a reviling, and for a reproach, and you do not see this place anymore.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama vile hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wale walioishi Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu mtakapokwenda Misri. Mtakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha kulaumia na cha kushutumia, nanyi kamwe hamtaona mahali hapa tena.’
19 YHWH has spoken against you, O remnant of Judah, do not enter Egypt: certainly know that I have testified against you today;
“Enyi mabaki ya Yuda, Bwana amewaambia, ‘Msiende Misri.’ Hakikisheni jambo hili: Ninawaonya leo
20 for you have showed yourselves perverse in your souls, for you sent me to your God YHWH, saying, Pray for us to our God YHWH, and according to all that our God YHWH says, so declare to us, and we have done [it];
kwamba mmefanya kosa kubwa mioyoni mwenu mliponituma kwa Bwana Mungu wenu na kusema, ‘Mwombe Bwana Mungu wetu kwa ajili yetu, nawe utuambie kila kitu atakachosema, nasi tutafanya.’
21 and I declare to you today, and you have not listened to the voice of your God YHWH, and to anything with which He has sent me to you.
Nimewaambieni leo, lakini bado ninyi hamtaki kumtii Bwana Mungu wenu katika yote aliyonituma niwaambie.
22 And now, certainly know that by sword, by famine, and by pestilence you die, in the place that you have desired to go to sojourn there.”
Basi sasa, hakikisheni jambo hili: Mtakufa kwa upanga, njaa na tauni mahali ambapo mnataka kwenda kuishi.”