< Jeremiah 41 >
1 And it comes to pass, in the seventh month, Ishmael son of Nethaniah, son of Elishama, of the royal seed, and of the chiefs of the king, and ten men with him, have come to Gedaliah son of Ahikam, to Mizpah, and there they eat bread together in Mizpah.
Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
2 And Ishmael son of Nethaniah rises, and the ten men who have been with him, and they strike Gedaliah son of Ahikam, son of Shaphan, with the sword, and he puts him to death whom the king of Babylon has appointed over the land.
Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
3 And all the Jews who have been with him, with Gedaliah, in Mizpah, and the Chaldeans who have been found there—the men of war—Ishmael has struck.
Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
4 And it comes to pass, on the second day of the putting of Gedaliah to death (and no one has known),
Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
5 that men come in from Shechem, from Shiloh, and from Samaria—eighty men—with shaven beards, and torn garments, and cutting themselves, and [with] an offering and frankincense in their hand, to bring [them] to the house of YHWH.
watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
6 And Ishmael son of Nethaniah goes forth to meet them, from Mizpah, going on and weeping, and it comes to pass, at meeting them, that he says to them, “Come to Gedaliah son of Ahikam.”
Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
7 And it comes to pass, at their coming into the midst of the city, that Ishmael son of Nethaniah slaughters them, at the midst of the pit, he and the men who [are] with him.
Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
8 And ten men have been found among them, and they say to Ishmael, “Do not put us to death, for we have things hidden in the field—wheat, and barley, and oil, and honey.” And he refrains, and has not put them to death in the midst of their brothers.
Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
9 And the pit to where Ishmael has cast all the carcasses of the men whom he has struck along with Gedaliah, is that which King Asa made because of Baasha king of Israel—Ishmael son of Nethaniah has filled it with the pierced.
Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
10 And Ishmael takes captive all the remnant of the people who [are] in Mizpah, the daughters of the king, and all the people who are left in Mizpah, whom Nebuzar-Adan, chief of the executioners, has committed [to] Gedaliah son of Ahikam, and Ishmael son of Nethaniah takes them captive, and goes to pass over to the sons of Ammon.
Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
11 And Johanan son of Kareah, and all the heads of the forces that [are] with him, hear of all the evil that Ishmael son of Nethaniah has done,
Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
12 and they take all the men, and go to fight with Ishmael son of Nethaniah, and they find him at the great waters that [are] in Gibeon.
waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
13 And it comes to pass, when all the people who [are] with Ishmael see Johanan son of Kareah, and all the heads of the forces who [are] with him, that they rejoice.
Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
14 And all the people whom Ishmael has taken captive from Mizpah turn around, indeed, they turn back, and go to Johanan son of Kareah.
Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
15 And Ishmael son of Nethaniah has escaped, with eight men, from the presence of Johanan, and he goes to the sons of Ammon.
Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
16 And Johanan son of Kareah, and all the heads of the forces who [are] with him, take all the remnant of the people whom he has brought back from Ishmael son of Nethaniah, from Mizpah—after he had struck Gedaliah son of Ahikam—mighty ones, men of war, and women, and infants, and eunuchs, whom he had brought back from Gibeon,
Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
17 and they go and abide in the habitations of Chimham, that [are] near Beth-Lehem, to go to enter Egypt,
Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
18 from the presence of the Chaldeans, for they have been afraid of them, for Ishmael son of Nethaniah had struck Gedaliah son of Ahikam, whom the king of Babylon had appointed over the land.
ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.