< Jeremiah 30 >

1 The word that has been to Jeremiah from YHWH, saying,
Neno lilokuja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe likisema,
2 “Thus spoke YHWH, God of Israel, saying, Write for yourself all the words that I have spoken to you on a scroll.
“Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema, 'Jiandikie mwenyewe katika baraua maneno yote niliyotangaza kwako katika barua.
3 For behold, days are coming—a declaration of YHWH—and I have turned back [to] the captivity of My people Israel and Judah, said YHWH, and I have caused them to return to the land that I gave to their fathers, and they possess it.”
Maana ona, siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—nitakapowarudisha mateka wa watu wangu Israeli na Yuda. Mimi, Yahwe, nimesema hili. Kwa maana nitawarudisha kwenye nchi ambayo niliwapa babu zao, na wataimiliki.”'
4 And these [are] the words that YHWH has spoken concerning Israel and concerning Judah:
Haya ni maneno ambayo Yahwe anatangaza kuhusu Israeli na Yuda,
5 Surely thus said YHWH: “We have heard a voice of trembling, Fear—and there is no peace.
“Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Tumesikia sauti ya kutetemesha ya hofu na wala siyo ya amani.
6 Now ask and see, is a male bringing forth? Why have I seen every man [With] his hands on his loins, as a travailing woman, And all faces have been turned to paleness?
Ulizeni na muone kama mwanaume anamwogopa mtoto. Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake kama mwanamke anayejifungua mtoto? Kwa nini nyuso zao wote zimegeuka rangi?
7 Woe! For that day [is] great, without any like it, Indeed, it [is] the time of Jacob’s tribulation, Yet he is saved out of it.
Ole! Kwa maana siku hiyo itakuwa kuu, isiyofanana na yoyote. Utakuwa wakati wa huzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.
8 And it has come to pass in that day, A declaration of YHWH of Hosts, I break his yoke from off your neck, And I draw away your bands, And strangers lay no more service on him.
Kwa maana itakuwa katika siku hiyo—hili ni tangazo la Yahwe wa majeshi—kwamba nitaivunja nira ya shingo zenu, na nitaisambaza minyororo yenu, kwa hiyo wageni hawatawafanya watumwa tena.
9 And they have served their God YHWH, And David their king whom I raise up to them.
Bali watamwabudu Yahwe Mungu wao na kumtumikia Daudi mfalme wao, ambaye nitamfanya mfalme juu yao.
10 And you, do not be afraid, My servant Jacob, A declaration of YHWH, Nor be frightened, O Israel, For behold, I am saving you from afar, And your seed from the land of their captivity, And Jacob has turned back and rested, And is quiet, and there is none troubling.
Kwa hiyo wewe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope—hili ni tangazo la Yahwe—na usikate tamaa, Israeli. Maana ona, niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa, Yakobo atarudi na kuwa katika amani; ataokolewa, na hapatakuwa na hofu zaidi.
11 For I [am] with you,” A declaration of YHWH, “To save you, For I make an end of all the nations To where I have scattered you, Only, I do not make an end of you, And I have disciplined you in judgment, And do not entirely acquit you.”
Kwa maana niko pamoja nawe—hili ni tangazo la Yahwe—ili kukuokoa. Kisha nitaleta mwisho kamili kwa mataifa yote ambako nimewatawanya. Bali sitaweka mwisho kwako, ingawa ninakuadhibu kwa haki na kwa hakika sitakuacha bila kukuadhibu.'
12 For thus said YHWH: “Your breach is incurable, your stroke grievous,
Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Jeraha lako si la kupona; kidonda chako kimeenea.
13 There is none judging your cause to bind up, There are no healing medicines for you.
Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako; hakuna utetezi kwa ajili ya kidonda chako ili upone.
14 All loving you have forgotten you, They do not seek you, For I struck you with the stroke of an enemy, The discipline of a fierce one, Because of the abundance of your iniquity, your sins have been mighty!
Wapenzi wako wote wamekusahau. Hawatakuangalia, kwa maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui na nidhimu ya bwana mkatili kwa sababu ya uovu wako mwingi na dhambi zako zisizohesabika.
15 Why do you cry concerning your breach? Your pain [is] incurable, Because of the abundance of your iniquity, Your sins have been mighty! I have done these to you.
Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako? Maumivu yako hayaponyeki. kwa sambabu ya uovu wako mwingi, dhambi zako zisizohesabika, nimefanya mambo haya kwako.
16 Therefore all consuming you are consumed, And all your adversaries—all of them—Go into captivity, And your spoilers have been for a spoil, And I give up all your plunderers to plunder.
Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote wataenda utumwani. Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.
17 For I increase health to you, And I heal you from your strokes,” A declaration of YHWH, “For they have called you an outcast, [saying], It [is] Zion, There is none seeking for her.”
Kwa maana nitaleta uponyaji juu yako; nitakuponya majeraha yako—hili ni tangazo la Yahwe—nitafanya hivyo kwa sababu walikuita: Mwenyekutupwa. Hakuna anayeujali Sayuni.”
18 Thus said YHWH: “Behold, I turn back [to] the captivity of the tents of Jacob, And I pity his dwelling places, And the city has been built on its heap, And the palace remains according to its ordinance.
Yahwe anasema hivi, “Ona, niko karibu kuwarudisha mateka wa hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake. Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu, na jumba litakuwepo tena kama ilivyokuwa kawaida.
19 And thanksgiving has gone forth from them, And the voice of playful ones, And I have multiplied them and they are not few, And made them honorable, and they are not small.
Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya ya shangwe itasikika kutoka kwao, kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza; nitawaheshimu ili kwamba wasifanywe wanyonge.
20 And his sons have been as before, And his congregation is established before Me, And I have seen after all his oppressors.
Kisha watu watakuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu wakati nitakapowaadhibu wote wanaowatesa kwa sasa.
21 And his majestic one has been of himself, And his ruler goes forth from his midst, And I have caused him to draw near, And he has drawn near to Me, For who [is] he who has pledged his heart To draw near to Me?” A declaration of YHWH.
Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao nitakapomleta karibu na atakapanikaribia mimi. kama sitafanya hivyo, ni nani atakayethubutu kunisogelea? —hili ni tangazo la Yahwe.
22 “And you have been to Me for a people, And I am to you for God.”
Kisha mtakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu.
23 Behold, a whirlwind of YHWH—Fury has gone forth—a cutting whirlwind, It stays on the head of the wicked.
Ona, tufani ya Yahwe, ghadhabu yake, imekwenda nje. Ni tufani isiyokoma. Itazunguka juu ya vichwa vya watu waovu.
24 The fierceness of the anger of YHWH Does not turn back until He has done [it], Indeed, until His establishing the purposes of His heart. In the latter end of the days you consider it!
Hasira ya Yahwe haitarudi mpaka itoke na kutimiza makusudi ya moyo wake. Katika siku za mwisho mtalielewa hili.”

< Jeremiah 30 >