< James 2 >
1 My brothers, do not hold the faith of the glory of our Lord Jesus Christ in favor by appearance,
Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2 for if there may come into your synagogue a man with gold ring, in radiant clothing, and there may also come in a poor man in vile clothing,
Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3 and you may look on him bearing the radiant clothing, and may say to him, “You—sit here well,” and may say to the poor man, “You—stand there,” or, “Sit here under my footstool,”
Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: “Keti hapa mahali pazuri,” na kumwambia yule maskini: “Wewe, simama huko,” au “Keti hapa sakafuni miguuni pangu,”
4 you did not judge fully in yourselves, and became ill-reasoning judges.
je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5 Listen, my beloved brothers, did God not choose the poor of this world, rich in faith, and heirs of the kingdom that He promised to those loving Him?
Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6 But you dishonored the poor one. Do the rich not oppress you and themselves draw you to judgment-seats?
Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7 Do they not themselves speak evil of the good Name having been called on you?
Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8 If, indeed, you fulfill royal law, according to the Writing: “You will love your neighbor as yourself,” you do well;
Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe”, mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9 but if you favor by appearance, you work sin, being convicted by the Law as transgressors;
Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10 for whoever will keep the whole Law, but will stumble in one [point], he has become guilty of all;
Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11 for He who is saying, “You may not commit adultery,” also said, “You may not murder”; but if you will not commit adultery, but will commit murder, you have become a transgressor of law;
Maana yuleyule aliyesema: “Usizini,” alisema pia “Usiue”. Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12 thus, speak and so act as [one] about to be judged by a law of liberty,
Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13 for the judgment without mercy [is] to him having not done mercy, and mercy exults over judgment.
Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14 What [is] the profit, my brothers, if anyone may speak of having faith, but he may not have works? Is that faith able to save him?
Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15 And if a brother or sister may be naked, and may be destitute of daily food,
Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16 and anyone of you may say to them, “Depart in peace, be warmed, and be filled,” but may not give to them the things necessary for the body, what [is] the profit?
Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: “Nendeni salama mkaote moto na kushiba,” bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17 So also faith, if it may not have works, is dead by itself.
Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18 But someone may say, “You have faith, and I have works.” Show me your faith without works, and I will show you my faith out of works.
Lakini mtu anaweza kusema: “Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!” Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19 You believe that God is one; you do well! The demons also believe—and shudder!
Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20 And do you wish to know, O vain man, that faith apart from works is dead?
Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21 Was not our father Abraham considered righteous out of works, having brought up his son Isaac on the altar?
Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22 Do you see that faith was working with his works, and faith was perfected out of the works?
Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23 And the Writing was fulfilled that is saying, “And Abraham believed God, and it was reckoned to him for righteousness”; and, “Friend of God” he was called.
Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu.”
24 You see, then, that man is considered righteous out of works, and not out of faith only;
Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25 and in like manner also Rahab the prostitute—was she not considered righteous out of works, having received the messengers, and having sent [them] forth by another way?
Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26 For as the body apart from [the] spirit is dead, so also the faith apart from works is dead.
Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.