< Isaiah 6 >
1 In the year of the death of King Uzziah—I see the Lord, sitting on a throne, high and lifted up, and His train is filling the temple.
Katika mwaka ule Mfalme Uzia alikufa, nilimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu na kilichotukuzwa sana, nalo pindo la joho lake likajaza Hekalu.
2 Seraphim are standing above it: each one has six wings; with two [each] covers its face, and with two [each] covers its feet, and with two [each] flies.
Juu yake walikuwepo maserafi, kila mmoja alikuwa na mabawa sita: Kwa mabawa mawili walifunika nyuso zao, kwa mengine mawili walifunika miguu yao, na kwa mawili walikuwa wakiruka.
3 And this one has called to that, and has said: “HOLY, HOLY, HOLY, [is] YHWH of Hosts, The fullness of all the earth [is] His glory!”
Nao walikuwa wakiitana kila mmoja na mwenzake: “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; dunia yote imejaa utukufu wake.”
4 And the posts of the thresholds are moved by the voice of him who is calling, and the house is full of smoke.
Kwa sauti zao, miimo ya milango na vizingiti vilitikisika, nalo Hekalu likajaa moshi.
5 And I say, “Woe to me, for I have been silent, For I [am] a man of unclean lips, And I am dwelling in [the] midst of a people of unclean lips, Because the King, YHWH of Hosts, my eyes have seen.”
Ndipo nikalia, “Ole wangu! Nimeangamia! Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninaishi katikati ya watu wenye midomo michafu, nayo macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
6 And one of the seraphim flees to me, and in his hand—a burning coal (with tongs he has taken [it] from off the altar),
Ndipo mmoja wa wale maserafi akaruka kunijia akiwa na kaa la moto linalowaka mkononi mwake, ambalo alikuwa amelichukua kwa koleo kutoka madhabahuni.
7 and he strikes against my mouth and says: “Behold, this has struck against your lips, And your iniquity is turned aside, And your sin is covered.”
Akanigusa nalo kinywa changu na kusema, “Tazama, hili limegusa midomo yako, uovu wako umeondolewa, nayo dhambi yako imesamehewa.”
8 And I hear the voice of the Lord, saying, “Whom do I send? And who goes for Us?” And I say, “Here I [am], send me.”
Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, “Nimtume nani? Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Nami nikasema, “Mimi hapa. Nitume mimi!”
9 And He says, “Go, and you have said to this people, Hearing you hear, and you do not understand, And seeing you see, and you do not know.
Akasema, “Nenda ukawaambie watu hawa: “‘Mtaendelea daima kusikiliza, lakini kamwe hamtaelewa; mtaendelea daima kutazama, lakini kamwe hamtatambua.’
10 Declare the heart of this people fat, And declare its ears heavy, And declare its eyes dazzled, Lest it see with its eyes, And hear with its ears, and consider with its heart, And it has turned back, and has health.”
Fanya mioyo ya watu hawa kuwa migumu, fanya masikio yao yasisikie, na upofushe macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, nao wakageuka, nikawaponywa.”
11 And I say, “Until when, O Lord?” And He says, “Surely until cities have been ruined without inhabitant, And houses without man, And the ground is ruined—a desolation,
Ndipo nikasema, “Hadi lini, Ee Bwana?” Naye akanijibu: “Hadi miji iwe imeachwa magofu na bila wakazi, hadi nyumba zitakapobaki bila watu, na mashamba yatakapoharibiwa na kuangamizwa,
12 And YHWH has put man far off, And the forsaken part [is] great in the heart of the land.
hadi Bwana atakapokuwa amekwisha kumpeleka kila mmoja mbali sana, na nchi itakapokuwa imeachwa kabisa.
13 And yet a tenth in it, and it has turned, And has been for a burning, As a teil-tree, and as an oak, that in falling, Has substance in them, The holy seed [is] its substance!”
Hata kama sehemu ya kumi ya watu watabaki katika nchi, itaharibiwa tena. Lakini kama vile mvinje na mwaloni ibakizavyo visiki inapokatwa, ndivyo mbegu takatifu itakavyokuwa kisiki katika nchi.”