< Isaiah 58 >

1 “Call with the throat, do not restrain, lift up your voice as a horn, And declare to My people their transgression, And to the house of Jacob their sins;
“Piga kelele, usizuie. Paza sauti yako kama tarumbeta. Watangazieni watu wangu uasi wao, na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.
2 They seek Me day by day, And they desire the knowledge of My ways, As a nation that has done righteousness, And has not forsaken the judgment of its God, They ask of Me judgments of righteousness, They desire the drawing near of God:
Kwa maana kila siku hunitafuta, wanaonekana kutaka kujua njia zangu, kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa, na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake. Hutaka kwangu maamuzi ya haki, nao hutamani Mungu awakaribie.
3 Why have we fasted, and You have not seen? We have afflicted our soul, and You do not know. Behold, you find pleasure in the day of your fast, And exact all your laborers.
Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona? Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’ “Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.
4 Behold, you fast for strife and debate, And to strike with the fist of wickedness, You do not fast as [this] day, To sound your voice in the high place.
Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano, na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu. Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.
5 Is this like the fast that I choose? The day of a man’s afflicting his soul? To bow his head as a reed, And spread out sackcloth and ashes? Do you call this a fast, And a desirable day—to YHWH?
Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua, siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza? Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete, na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu? Je, huo ndio mnaouita mfungo, siku iliyokubalika kwa Bwana?
6 Is this not the fast that I chose—To loose the bands of wickedness, To shake off the burdens of the yoke, And to send out the oppressed free, And draw off every yoke?
“Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua: kufungua minyororo ya udhalimu, na kufungua kamba za nira, kuwaweka huru walioonewa, na kuvunja kila nira?
7 Is it not to deal your bread to the hungry, And bring home the wandering poor, That you see the naked and cover him, And do not hide yourself from your own flesh?
Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi, unapomwona aliye uchi, umvike, wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?
8 Then your light breaks forth as the dawn, And your health springs up in haste, Your righteousness has gone before you, The glory of YHWH gathers you.
Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko na uponyaji wako utatokea upesi; ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako, na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.
9 Then you call, and YHWH answers, You cry, and He says, Behold Me. If you turn aside the yoke from your midst, The sending forth of the finger, And the speaking of vanity,
Ndipo utaita, naye Bwana atajibu, utalia kuomba msaada, naye atasema: Mimi hapa. “Kama ukiiondoa nira ya udhalimu, na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,
10 And bring out your soul to the hungry, And satisfy the afflicted soul, Then your light has risen in the darkness, And your thick darkness [is] as noon.
nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani, nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.
11 And YHWH continually leads you, And has satisfied your soul in drought, And He arms your bones, And you have been as a watered garden, And as an outlet of waters, whose waters do not lie.
Bwana atakuongoza siku zote, atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame, naye ataitia nguvu mifupa yako. Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri, kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.
12 And they have built the ancient ruins from you, You raise up the foundations of many generations, And one calls you, Repairer of the breach, Restorer of paths to rest in.
Watu wako watajenga tena magofu ya zamani na kuinua misingi ya kale; utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka, Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.
13 If you turn your foot from the Sabbath, [From] doing your own pleasure on My holy day, And have cried to the Sabbath, A delight, To the holy of YHWH, Honored, And have honored it, without doing your own ways, Without finding your own pleasure, And speaking a word.
“Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato, na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu, kama ukiita Sabato siku ya furaha na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa, kama utaiheshimu kwa kutoenenda katika njia zako mwenyewe, na kutokufanya yakupendezayo au kusema maneno ya upuzi,
14 Then you delight yourself on YHWH, And I have caused you to ride on high places of earth, And have caused you to eat the inheritance of your father Jacob, For the mouth of YHWH has spoken!”
ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana, nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.” Kinywa cha Bwana kimenena haya.

< Isaiah 58 >