< Isaiah 29 >
1 Woe [to] Ariel, Ariel, The city of the encampment of David! Add year to year, let festivals go around.
Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
2 And I have sent distress to Ariel, And it has been lamentation and mourning, And it has been to me as Ariel.
Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
3 And I encamped, O babbler, against you, And I laid siege against you—a camp. And I raised up bulwarks against you.
Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
4 And you have been low, You speak from the earth, And make your saying low from the dust, And your voice has been from the earth, As one having a familiar spirit, And your saying whispers from the dust,
Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
5 And as small dust has been The multitude of those scattering you, And as chaff passing on the multitude of the terrible, And it has been in an instant—suddenly.
Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
6 You are inspected by YHWH of Hosts, With thunder, and with an earthquake, And great noise, windstorm, and whirlwind, And flame of devouring fire.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
7 And as a dream, a vision of night, Has been the multitude of all the nations Who are warring against Ariel, And all its warriors, and its bulwark, Even of those distressing her.
Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
8 And it has been, as when the hungry dreams, And behold, he is eating, And he has awoken, And his soul [is] empty, And as when the thirsty dreams, And behold, he is drinking, And he has awoken, And behold, he is weary, And his soul is longing, So is the multitude of all the nations Who are warring against Mount Zion.
kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
9 Linger and wonder, look, indeed, look, Be drunk, and not with wine, Stagger, and not with strong drink.
Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
10 For YHWH has poured out a spirit of deep sleep on you, And He closes your eyes—the prophets, And your heads—the seers—He covered.
Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
11 And the vision of the whole is to you, As words of the sealed scroll, That they give to one knowing scrolls, Saying, “Please read this,” And he has said, “I am not able, for it [is] sealed”;
Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
12 And the scroll is given to him who has not known scrolls, Saying, “Please read this,” And he has said, “I have not known scrolls.”
Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
13 And the Lord says: “Because this people has drawn near with its mouth, And they have honored Me with its lips, And it has put its heart far off from Me, And their fear of Me is a precept taught by men!
Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
14 Therefore, behold, I am adding to do wonderfully with this people, A wonder, and a marvel, And the wisdom of its wise ones has perished, And the understanding of its intelligent ones hides itself.”
Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
15 Woe [to] those going deep from YHWH to hide counsel, And whose works have been in darkness. And they say, “Who is seeing us? And who is knowing us?”
Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
16 Your perversion! Is the potter esteemed as clay, That the work says of its maker, “He has not made me?” And the framed thing said of its framer, “He did not understand?”
Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
17 Is it not yet a very little [while], And Lebanon has turned into a fruitful field, And the fruitful field is reckoned for a forest?
Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
18 And the deaf have heard the words of a scroll in that day, And out of thick darkness, and out of darkness, The eyes of the blind see.
Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
19 And the humble have added joy in YHWH, And the poor among men Rejoice in the Holy One of Israel.
Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
20 For the terrible one has ceased, And the scorner has been consumed, And all watching for iniquity have been cut off,
Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
21 Who cause men to sin in word, And lay a snare for a reprover in the gate, And turn aside the righteous into emptiness.
wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
22 Therefore, thus said YHWH, Who ransomed Abraham, Concerning the house of Jacob: “Jacob is not ashamed now, Nor does his face now become pale,
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
23 For in his seeing his children, The work of My hand, in his midst, They sanctify My Name, And have sanctified the Holy One of Jacob, And they declare the God of Israel fearful.
Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
24 And the erring in spirit have known understanding, And murmurers learn doctrine!”
Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”