< Hosea 7 >
1 “When I give healing to Israel, Then the iniquity of Ephraim is revealed, And the wickedness of Samaria, For they have worked falsehood, And a thief comes in, A troop has stripped off in the street,
kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
2 And they do not say to their heart, [That] I have remembered all their evil, Now their doings have surrounded them, They have been before My face.
lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
3 With their wickedness they make a king glad, And with their lies—princes.
“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
4 All of them [are] adulterers, Like a burning oven of a baker, He ceases from stirring up after kneading the dough, until its leavening.
Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
5 A day of our king! Princes have defiled themselves [with] the poison of wine, He has drawn out his hand with scorners.
Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 For they have drawn near, Their heart [is] as an oven In their lying in wait—their baker sleeps all night, Morning! He is burning as a flaming fire.
Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
7 All of them are warm as an oven, And they have devoured their judges, All their kings have fallen, There is none calling to Me among them.
Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 Ephraim! He mixes himself among peoples, Ephraim has been an unturned cake.
“Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 Strangers have devoured his power, And he has not known, Also old age has sprinkled [itself] on him, And he has not known.
Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
10 And the excellence of Israel has been humbled to his face, And they have not turned back to their God YHWH, Nor have they sought Him for all this.
Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
11 And Ephraim is as a simple dove without heart, Egypt they called on—[to] Asshur they have gone.
“Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
12 When they go I spread over them My net, As the bird of the heavens I bring them down, I discipline them as their congregation has heard.
Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
13 Woe to them, for they wandered from Me, Destruction to them, for they transgressed against Me, And I ransom them, and they have spoken lies against Me,
Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 And have not cried to Me with their heart, but howl on their beds; They assemble themselves for grain and new wine, They turn aside against Me.
Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
15 And I instructed—I strengthened their arms, And concerning Me they think evil!
Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They turn back—not to the Most High, They have been as a deceitful bow, Their princes fall by sword, From the insolence of their tongue, This [is] their derision in the land of Egypt!”
Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.