< Hebrews 8 >
1 And the sum concerning the things spoken of [is]: we have such a Chief Priest, who sat down at the right hand of the throne of the Greatness in the heavens,
Basi, jambo muhimu katika hayo tunayosema ni hili: sisi tunaye Kuhani Mkuu wa namna hiyo, ambaye anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu mbinguni.
2 a servant of the holy places, and of the true dwelling place, which the LORD set up, and not man,
Yeye hutoa huduma ya Kuhani Mkuu katika Mahali Patakatifu sana, yaani ndani ya ile hema ya kweli iliyojengwa na Bwana, siyo na binadamu.
3 for every chief priest is appointed to offer both gifts and sacrifices, from where [it is] necessary for this One to also have something that He may offer;
Kila Kuhani Mkuu ameteuliwa kumtolea Mungu vipawa na dhabihu, na hivyo Kuhani Mkuu wetu lazima pia awe na kitu cha kutolea.
4 for if, indeed, He were on earth, He would not be a priest (there being the priests who are offering the gifts according to the Law,
Kama yeye angekuwa wa hapa duninani, asingekuwa kamwe kuhani, kwani wako makuhani wengine wanaotoa sadaka kufuatana na Sheria.
5 who to an example and shadow serve of the heavenly things, as Moses has been divinely warned, being about to construct the Dwelling Place, for, “See,” He says, “[that] you will make all things according to the pattern that was shown to you on the mountain”),
Huduma zao za kikuhani ni mfano tu na kivuli cha yale yaliyoko mbinguni. Ndivyo pia ilivyokuwa kwa Mose. Wakati alipokuwa karibu kuitengeneza ile hema, Mungu alimwambia: “Tengeneza kila kitu kufuatana na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.”
6 but now He has obtained a more excellent service, how much He is also mediator of a better covenant, which has been sanctioned on better promises,
Lakini sasa Yesu amepewa huduma ya kikuhani iliyo bora zaidi kuliko yao, kama vile agano alilothibitisha kati ya watu na Mungu ni bora zaidi, kwani lina msingi wake katika ahadi za mambo yaliyo bora zaidi.
7 for if that first were faultless, a place would not have been sought for a second.
Maana kama lile agano la kwanza halingalikuwa na dosari, hakungalikuwa na haja ya agano la pili.
8 For finding fault, He says to them, “Behold, days come, says the LORD, and I will complete with the house of Israel, and with the house of Judah, a new covenant,
Lakini Mungu aliwalaumu watu wake aliposema: “Siku zinakuja, asema Bwana, ambapo nitafanya agano jipya na watu wa Israeli na kabila la Yuda.
9 not according to the covenant that I made with their fathers, in the day of My taking [them] by their hand, to bring them out of the land of Egypt—because they did not remain in My covenant, and I did not regard them, says the LORD—
Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao siku ile nilipowaongoza kwa mkono kutoka nchi ya Misri. Hawakuwa waaminifu kwa agano langu; na hivyo mimi sikuwajali, asema Bwana.
10 because this [is] the covenant that I will make with the house of Israel, after those days, says the LORD, giving My laws into their mind, and I will write them on their hearts, and I will be to them for a God, and they will be to Me for a people;
Na hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa Israeli siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu akilini mwao, na kuziandika mioyoni mwao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
11 and they will not each teach his neighbor, and each his brother, saying, Know the LORD, because they will all know Me—from the small one of them to the great one of them,
Hakuna mtu atakayemfundisha mwananchi mwenzake, wala atakayemwambia ndugu yake: Mjue Bwana. Maana watu wote, wadogo na wakubwa, watanijua mimi.
12 because I will be merciful to their unrighteousness, and I will remember their sins and their lawlessnesses no more.”
Nitawasamehe makosa yao, wala sitakumbuka tena dhambi zao.”
13 In the saying “new,” He has made the first obsolete, and what is becoming obsolete and growing old [is] near disappearing.
Kwa kusema juu ya agano jipya, Mungu alilichakaza lile la kwanza; na chochote kinachochakaa na kuwa kikuukuu kitatoweka karibuni.