< Hebrews 5 >
1 For every chief priest taken out of men is set in things [pertaining] to God in behalf of men, that he may offer both gifts and sacrifices for sins,
Kwani kila kuhani mkuu, aliyechaguliwa kutoka miongoni mwa watu, amechaguliwa kusimama badala yao katika vitu vinavyohusiana na Mungu, ili aweze kutoa kwa pamoja zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.
2 being able to be gentle to those being ignorant and going astray, since he is also surrounded with weakness;
Anaweza kujishughulisha kwa upole na wajinga na wabishi kwa kuwa yeye mwenyewe pia amezungukwa na udhaifu.
3 and because of this [weakness] he ought, just as for the people, so also for himself, to bring forward [sacrifices] for sins;
Kwa sababu ya hili, ana wajibu wa kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi zake kama afanyavyo kwa dhambi za watu.
4 and no one takes the honor to himself, but he who is called by God, as also Aaron.
Na hakuna mtu achukuaye heshima hii kwa ajili yake mwenyewe, lakini badala yake, lazima aitwe na Mungu, kama alivyokuwa Haruni.
5 So also the Christ did not glorify Himself to become Chief Priest, but He who spoke to Him: “You are My Son, today I have begotten You”;
Hata Kristo hakujipa heshimu mwenyewe kwa kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Badala yake, Mungu alisema kwake, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa Baba yako.”
6 just as He also says in another [place], “You [are] a priest throughout the age, according to the order of Melchizedek”; (aiōn )
Ni kama asemavyo pia sehemu nyingine, “Wewe ni kuhani milele baada ya mfumo wa Melkizedeki.” (aiōn )
7 who in the days of His flesh having offered up both prayers and supplications with strong crying and tears to Him who was able to save Him from death, and having been heard in respect to that which He feared,
Wakati wa kipindi chake katika mwili, aliomba na kuombea, alimwomba Mungu kwa machozi, kwa yeye awezaye kumwokoa kutoka kwenye kifo. Kwa sababu ya unyenyekevu wake kwa Mungu, alisikiwa.
8 though being a Son, [He] learned obedience by the things which He suffered,
Ijapokuwa alikua mwana, alijifunza kutii kwa mambo yaliyomtesa.
9 and having been made perfect, He became the cause of continuous salvation to all those obeying Him, (aiōnios )
Alikamilishwa na kwa njia hii alifanyika kwa kila mtu amwaminiye kuwa sababu ya wokovu wa milele, (aiōnios )
10 having been called by God a Chief Priest according to the order of Melchizedek,
kwa kutengwa na Mungu kama kuhani Mkuu baada ya zamu ya Melkizedeki.
11 concerning the Word, of whom we have much [to speak], and of hard explanation to say, since you have become dull of hearing,
Tuna mengi ya kusema kuhusu Yesu, lakini ni vigumu kuwaelezea kwa kuwa ninyi ni wavivu wa kusikia.
12 for even owing to be teachers, because of the time, again you have need that one teach you what [are] the elements of the beginning of the oracles of God, and you have become having need of milk, and not of strong food,
Ijapokuwa kwa kipindi hiki mlipaswa kuwa walimu, bado kuna umuhimu wa mtu kuwafundisha mafundisho ya awali ya kanuni za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa na si chakula kigumu.
13 for everyone who is partaking of milk [is] unskilled in the word of righteousness—for he is an infant,
Kwa kuwa yeyote anywaye maziwa tu hana uzoefu katika ujumbe wa haki, kwa kuwa bado ni mtoto.
14 and the strong food is of perfect men, who because of the use are having the senses exercised, to both the discernment of good and of evil.
Kwa upande mwingine, chakula kigumu ni cha watu wazima, wale ambao kwa sababu ya uzoefu wao katika kutofautisha haki na ubaya wamefundishwa kutambua jema na ovu.