< Hebrews 13 >
1 Let brotherly love remain.
Endeleeni kupendana kidugu.
2 Do not be forgetful of hospitality, for through this some entertained messengers unaware.
Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
3 Be mindful of those in bonds, as having been bound with them, of those maltreated, as yourselves also being in the body.
Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
4 The marriage [is to be] honored by all, and the bed undefiled, for God will judge whoremongers and adulterers.
Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
5 [Be] without covetous behavior, being content with the things present, for He has said, “No, I will not leave, no, nor forsake you,”
Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: “Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa.”
6 so that we boldly say, “The LORD [is] to me a helper, and I will not fear what man will do to me.”
Ndiyo maana tunathubutu kusema: “Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?”
7 Be mindful of those leading you, who spoke to you the word of God, who, considering the outcome of [their] behavior, imitate [their] faith:
wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
8 Jesus Christ—the same yesterday and today and for all ages. (aiōn )
Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele. (aiōn )
9 Do not be carried away with strange and manifold teachings, for [it is] good that by grace the heart is confirmed, not with meats, in which they who were occupied were not profited;
Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
10 we have an altar from which they who are serving the Dwelling Place have no authority to eat,
Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
11 for of those beasts whose blood is brought for sin into the holy places through the chief priest—of these the bodies are burned outside the camp.
Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12 For this reason, also Jesus—that He might sanctify the people through [His] own blood—suffered outside the gate;
Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
13 now then, may we go forth to Him outside the camp, bearing His reproach;
Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
14 for we have no abiding city here, but we seek the coming one.
Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
15 Through Him, then, we may always offer up a sacrifice of praise to God, that is, the fruit of lips, giving thanks to His Name.
Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
16 And do not be forgetful of doing good and of fellowship, for God is well-pleased with such sacrifices.
Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
17 Be obedient to those leading you, and be subject, for these watch for your souls, as about to give account, that they may do this with joy, and not sighing, for this [is] unprofitable to you.
Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18 Pray for us, for we trust that we have a good conscience, willing to behave well in all things,
Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
19 and I call on [you] to do this more abundantly, that I may be restored to you more quickly.
Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
20 And the God of peace, who brought up the Great Shepherd of the sheep out of the dead—by the blood of a perpetual covenant—our Lord Jesus, (aiōnios )
Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele. (aiōnios )
21 make you perfect in every good work to do His will, doing in you that which is well-pleasing before Him, through Jesus Christ, to whom [is] the glory through the ages of the ages! Amen. (aiōn )
Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina. (aiōn )
22 And I beg you, brothers, endure the word of the exhortation, for I have also written to you through few words.
Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
23 Know that the brother Timotheus is released, with whom I will see you, if he may come more shortly.
Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
24 Greet all those leading you, and all the holy ones. Those from Italy greet you.
Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
25 The grace [is] with you all! Amen.
Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.