< Hebrews 12 >
1 Therefore, we also having so great a cloud of witnesses set around us, having put off every weight, and the closely besetting sin, may we run the contest that is set before us through endurance,
Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, na dhambi ile inayotung'ang'ania. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
2 looking to the Author and Perfecter of the faith—Jesus, who, for the joy set before Him, endured a cross, having despised shame, and sat down at the right hand of the throne of God;
Tumwelekee Yesu ambaye ndiye aliyeianzisha imani yetu na ambaye ataikamilisha. Kwa ajili ya furaha iliyokuwa inamngojea, yeye alivumilia kifo msalabani, bila kujali juu ya aibu yake, na sasa anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 for again consider Him who endured such contradiction from the sinners to Himself, that you may not be wearied in your souls—being faint.
Fikirini juu ya mambo yaliyompata Yesu, jinsi alivyostahimili upinzani mkubwa kwa watu wenye dhambi. Basi, msife moyo, wala msikate tamaa.
4 You did not yet resist to blood—striving with sin;
Maana katika kupambana na dhambi, ninyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu.
5 and you have forgotten the exhortation that speaks fully to you as to sons, “My son, do not despise [the] discipline of [the] LORD, nor be faint, being reproved by Him,
Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja ninyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.
6 for whom the LORD loves He disciplines, and He scourges every son whom He receives”;
Maana Bwana humwadhibu kila anayempenda, humpinga kila anayekubali kuwa mwanae.”
7 if you endure discipline, God bears Himself to you as to sons, for who is a son whom a father does not discipline?
Vumilieni adhabu kwani ni mafundisho; Mungu huwatendea ninyi kama wanawe. Maana ni mwana gani asiyeadhibiwa na baba yake?
8 And if you are apart from discipline, of which all have become partakers, then you are bastards, and not sons.
Lakini msipoadhibiwa kama wana wengine, basi, ninyi si wanawe, bali ni wana haramu.
9 Then, indeed, we have had fathers of our flesh, correctors, and we respected [them]; will we not much rather be subject to the Father of the spirits, and live?
Zaidi ya hayo sisi tunawaheshimu wazazi wetu waliotuzaa hata wanapotuadhibu. Basi, tunapaswa kumtii zaidi Baba yetu wa kiroho ili tupate kuishi.
10 For they, indeed, for a few days, according to what seemed good to them, were disciplining, but He for profit, to be partakers of His separation;
Wazazi wetu hapa duniani walituadhibu kwa muda, kama wao wenyewe walivyoona kuwa vema; lakini Mungu anatuadhibu kwa ajili ya faida yetu wenyewe, tupate kuushiriki utakatifu wake.
11 and all discipline for the present, indeed, does not seem to be of joy, but of sorrow, yet afterward it yields the peaceable fruit of righteousness to those exercised through it.
Kuadhibiwa si jambo la kufurahisha bali la kuhuzunisha. Lakini wale waliofunzwa kuwa na nidhamu mwishowe watavuna tuzo la amani kutoka katika maisha adili!
12 For this reason, lift up the hanging-down hands and the loosened knees;
Basi, inueni mikono yenu inayolegea na kuimarisha magoti yenu yaliyo dhaifu.
13 and make straight paths for your feet, so that which is lame may not be turned aside, but rather be healed;
Endeleeni kutembea katika njia iliyonyoka, ili kile kilicholemaa kisiumizwe, bali kiponywe.
14 pursue peace with all, and the separation, apart from which no one will see the LORD,
Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo.
15 observing lest anyone be failing of the grace of God, lest any root of bitterness springing up may give trouble, and through this many may be defiled;
Jitahidini sana mtu yeyote asije akapoteza neema ya Mungu. Muwe waangalifu ili mti mchungu usizuke kati yenu na kuwaua wengi kwa sumu yake.
16 lest anyone be a fornicator, or a profane person, as Esau, who in exchange for one morsel of food sold his birthright,
Jihadharini ili miongoni mwenu pasiwe na mtu mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, aliyeuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mlo mmoja.
17 for you know that also afterward, wishing to inherit the blessing, he was disapproved of, for he did not find a place of conversion, though having sought it with tears.
Ninyi mnafahamu kwamba hata alipotaka kuipata tena ile baraka iliyokuwa yake, alikataliwa, maana hakupata tena nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
18 For you did not come near to the mountain touched and scorched with fire, and to blackness, and darkness, and storm,
Ninyi hamkuwasili mlimani Sinai, ambao unaweza kushikika kama walivyofanya watu wa Israeli, hamkufika kwenye moto uwakao, penye giza, tufani,
19 and a sound of a trumpet, and a voice of sayings, which those having heard begged that a word might not be added to them,
mvumo wa tarumbeta na sauti ya maneno. Wale waliosikia sauti hiyo waliomba wasisikie tena neno jingine,
20 for they were not bearing that which is commanded, “And if a beast may touch the mountain, it will be stoned, or shot through with an arrow,”
kwani hawakuweza kustahimili amri iliyotolewa: “Atakayegusa mlima huu, hata kama ni mnyama, atapigwa mawe.”
21 and (so terrible was the sight), Moses said, “I am exceedingly fearful, and trembling.”
Hayo yote yalionekana ya kutisha mno, hata Mose akasema, “Naogopa na kutetemeka.”
22 But you came to Mount Zion, and to [the] city of the living God, to the heavenly Jerusalem, and to myriads of messengers,
Lakini ninyi mmefika katika mlima wa Sioni, kwenye mji wa Mungu aliye hai. Mmefika Yerusalemu, mji wa mbinguni, ambapo wamekusanyika malaika elfu nyingi wasiohesabika.
23 to the assembly-place and Assembly of the Firstborn registered in Heaven, and to God the judge of all, and to spirits of righteous men made perfect,
Mmefika kwenye kusanyiko kubwa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mnasimama mbele ya Mungu aliye hakimu wa wote, na mbele ya roho za watu waadilifu waliofanywa kuwa wakamilifu.
24 and to a mediator of a new covenant—Jesus, and to blood of sprinkling, speaking better things than that of Abel!
Mmefika kwa Yesu ambaye ameratibisha agano jipya, na ambaye damu yake iliyomwagika inasema mambo mema zaidi kuliko ile ya Abeli.
25 Watch out lest you refuse Him who is speaking, for if those did not escape who refused him who was divinely speaking on earth—much less we who turn away from Him who [speaks] from Heaven,
Basi, jihadharini msije mkakataa kumsikiliza yeye ambaye anasema nanyi. Kama wale walikataa kumsikiliza yule aliyewaonya hapa duniani hawakuokoka, sisi tutawezaje kuokoka kama tukikataa kumsikiliza yule anayetuonya kutoka mbinguni?
26 whose voice shook the earth then, and now He has promised, saying, “Yet once [more]—I shake not only the earth, but also Heaven”;
Wakati ule sauti ilitetemesha nchi, lakini sasa ameahidi: “Nitatetemesha nchi tena, lakini si nchi tu bali pia mbingu.”
27 and this, “Yet once [more],” makes evident the removal of the things shaken, as of things having been made, that the things not shaken may remain;
Neno hili: “tena” linatuonyesha kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vitatetemeshwa na kutoweka ili vibaki vile visivyotetemeshwa.
28 for this reason, receiving a kingdom that cannot be shaken, may we have grace, through which we may serve God well-pleasingly, with reverence and fear,
Sisi basi, na tushukuru kwani tunapokea utawala usiotikisika. Tuwe na shukrani na kumwabudu Mungu kwa namna itakayompendeza, kwa ibada na hofu;
29 for our God [is] also a consuming fire.
maana Mungu wetu kweli ni moto mkali unaoteketeza.