< Genesis 5 >

1 This [is] an account of the generations of Adam. In the day of God’s creating man, in the likeness of God He has made him;
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 a male and a female He has created them, and He blesses them, and calls their name Man, in the day of their being created.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 And Adam lives one hundred and thirty years [[or two hundred and thirty years]], and begets [a son] in his likeness, according to his image, and calls his name Seth.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 And the days of Adam after his begetting Seth are eight hundred years [[or seven hundred years]], and he begets sons and daughters.
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 And all the days of Adam which he lived are nine hundred and thirty years, and he dies.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 And Seth lives one hundred and five years [[or two hundred and five years]], and begets Enos.
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 And Seth lives after his begetting Enos eight hundred and seven years [[or seven hundred and seven years]], and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 And all the days of Seth are nine hundred and twelve years, and he dies.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 And Enos lives ninety years [[or one hundred and ninety years]], and begets Cainan.
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 And Enos lives after his begetting Cainan eight hundred and fifteen years [[or seven hundred and fifteen years]], and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 And all the days of Enos are nine hundred and five years, and he dies.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 And Cainan lives seventy years [[or one hundred and seventy years]], and begets Mahalaleel.
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 And Cainan lives after his begetting Mahalaleel eight hundred and forty years [[or seven hundred and forty years]], and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 And all the days of Cainan are nine hundred and ten years, and he dies.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 And Mahalaleel lives sixty-five years [[or one hundred and sixty-five years]], and begets Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 And Mahalaleel lives after his begetting Jared eight hundred and thirty years [[or seven hundred and thirty years]], and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 And all the days of Mahalaleel are eight hundred and ninety-five years, and he dies.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 And Jared lives one hundred and sixty-two years, and begets Enoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 And Jared lives after his begetting Enoch eight hundred years, and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 And all the days of Jared are nine hundred and sixty-two years, and he dies.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 And Enoch lives sixty-five years [[or one hundred and sixty-five years]], and begets Methuselah.
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 And Enoch habitually walks with God after his begetting Methuselah three hundred years [[or two hundred years]], and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 And all the days of Enoch are three hundred and sixty-five years.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 And Enoch habitually walks with God, and he is not, for God has taken him.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 And Methuselah lives one hundred and eighty-seven years, and begets Lamech.
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 And Methuselah lives after his begetting Lamech seven hundred and eighty-two years, and begets sons and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 And all the days of Methuselah are nine hundred and sixty-nine years, and he dies.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 And Lamech lives one hundred and eighty-two years [[or one hundred and eighty-eight years]], and begets a son,
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 and calls his name Noah, saying, “This [one] comforts us concerning our work, and concerning the labor of our hands, because of the ground which YHWH has cursed.”
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 And Lamech lives after his begetting Noah five hundred and ninety-five years [[or five hundred and sixty-five years]], and begets sons and daughters.
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 And all the days of Lamech are seven hundred and seventy-seven years [[or seven hundred and fifty-three years]], and he dies.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 And Noah is a son of five hundred years, and Noah begets Shem, Ham, and Japheth.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

< Genesis 5 >