< Genesis 45 >
1 And Joseph has not been able to refrain himself before all those standing by him, and he calls, “Put out every man from me”; and no man has stood with him when Joseph makes himself known to his brothers,
Ndipo Yusufu hakuweza kujizuia mwenyewe mbele ya watumishi waliosimama kando yake. Akasema kwa sauti, “Kila mtu aondoke.” Hivyo hakuna mtumishi aliyesimama kando yake wakati Yusufu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
2 and he gives forth his voice in weeping, and the Egyptians hear, and the house of Pharaoh hears.
Akalia kwa sauti, Wamisri wakasikia, na nyumba ya Farao wakasikia kuhusu hilo.
3 And Joseph says to his brothers, “I [am] Joseph, is my father yet alive?” And his brothers have not been able to answer him, for they have been troubled at his presence.
Yusufu akawambia ndugu zake, “Mimi ni Yusufu. Je baba yangu ni mzima bado? Ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwani walitishwa na uwepo wake.
4 And Joseph says to his brothers, “Please come near to me,” and they come near; and he says, “I [am] your brother Joseph, whom you sold into Egypt;
Kisha Yusufu akawambia ndugu zake, “Nikaribieni, tafadhari.” Nao wakasogea. Akawambia, “Mimi ni Yusufu ndugu yenu, mliyemwuza Misri.
5 and now, do not be grieved, nor let it be displeasing in your eyes that you sold me here, for God has sent me before you to preserve life.
Lakini sasa msihuzunike au kukasirika miongoni mwenu kwamba mliniuza huku, kwani Mungu alinituma mbele yenu ili kutunza uhai.
6 Because these two years the famine [is] in the heart of the land, and yet five years [remain in] which there is neither plowing nor harvest;
Maana ni miaka miwili njaa imekuwa katika nchi, na bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.
7 and God sends me before you, to place a remnant of you in the land, and to give life to you by a great escape;
Mungu alinituma mbele yenu kuwahifadhi kama masalia duniani, na kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu.
8 and now, you have not sent me here, but God, and He sets me for a father to Pharaoh, and for lord to all his house, and ruler over all the land of Egypt.
Hivyo si ninyi mlionipeleka huku bali ni Mungu, na amenifanya baba kwa Farao, bwana wa nyumba yake yote, na mtawala wa nchi yote ya Misri.
9 Hurry, and go up to my father, then you have said to him, Thus said your son Joseph: God has set me for lord to all Egypt; come down to me, do not stay,
Fanyeni haraka mwende kwa baba yangu na mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, “Mungu amenifanya bwana kwa Wamisri wote. Shuka kwangu, usikawie.
10 and you have dwelt in the land of Goshen, and been near to me, you and your sons, and your son’s sons, and your flock, and your herd, and all that you have,
Utaishi katika nchi ya Gosheni, nawe utakuwa karibu nami, wewe na watoto wako na watoto wa watoto wako, na kondoo wako na mbuzi wako, na yote uliyonayo.
11 and I have nourished you there—for yet [are] five years of famine—lest you become poor, you and your household, and all that you have.
Nami nitakuhudumia pale, kwa maana bado kuna miaka mitano ya njaa, hivyo usije ukaingia katika uhitaji, wewe, nyumba yako, na yote uliyonayo.”
12 And behold, your eyes are seeing, and the eyes of my brother Benjamin, that [it is] my mouth which is speaking to you;
Tazama, macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu, kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi.
13 and you have declared to my father all my glory in Egypt, and all that you have seen, and you have hurried, and have brought down my father here.”
Mtamwambia baba yangu juu ya heshima yangu yote huku Misri na yote mliyoyaona. Mtaharakisha na kumleta baba yangu huku.”
14 And he falls on the neck of his brother Benjamin, and weeps, and Benjamin has wept on his neck;
Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shongoni mwake.
15 and he kisses all his brothers, and weeps over them; and afterward his brothers have spoken with him.
Akawabusu ndugu zake wote na kulia kwa ajili yao. Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye.
16 And the sound has been heard in the house of Pharaoh, saying, “The brothers of Joseph have come”; and it is good in the eyes of Pharaoh, and in the eyes of his servants,
Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: “Ndugu zake Yusufu wamekuja.” Ikampendeza sana Farao na watumishi wake.
17 and Pharaoh says to Joseph, “Say to your brothers, This you do: load your beasts, and go, enter the land of Canaan,
Farao akamwambia Yusufu, “Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani.
18 and take your father, and your households, and come to me, and I give to you the good of the land of Egypt, and you eat the fat of the land.
Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'
19 Indeed, you have been commanded: this you do, take for yourselves out of the land of Egypt, wagons for your infants, and for your wives, and you have brought your father, and come;
Basi mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja.
20 and your eye has no pity on your vessels, for the good of all the land of Egypt [is] yours.”
Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu.”
21 And the sons of Israel do so, and Joseph gives wagons to them by the command of Pharaoh, and he gives to them provision for the way;
Wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yusufu akawapa mikokoteni, kwa kadili ya agizo la Farao, na akawapa mahitaji ya safari.
22 to all of them has he given—to each changes of garments, and to Benjamin he has given three hundred pieces of silver, and five changes of garments;
Akawapa wote mavazi ya kubadilisha, lakini akampa Benjamini vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha.
23 and to his father he has sent thus: ten donkeys carrying of the good things of Egypt, and ten female donkeys carrying grain and bread, even food for his father for the way.
Akampelekea baba yake: punda kumi waliobeba mema ya Misri, punda majike kumi wamebeba nafaka, mikate, na mahitaji mengine kwa baba yake kwa ajili ya safari.
24 And he sends his brothers away, and they go; and he says to them, “Do not be angry in the way.”
Hivyo akawaruhusu ndugu zake nao wakaondoka. Akawambia, “Angalieni msijemkagombana njiani.”
25 And they go up out of Egypt, and come to the land of Canaan, to their father Jacob,
Wakapanda kutoka Misri na kuja katika nchi ya Kanaani, kwa Yakobo baba yao.
26 and they declare to him, saying, “Joseph [is] yet alive,” and that he [is] ruler over all the land of Egypt; and his heart ceases, for he has not given credence to them.
Wakamwambia “Yusufu bado yu hai, na ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri.” Na moyo wake ulishikwa na ushangao, kwani hakuwaamini.
27 And they speak to him all the words of Joseph, which he has spoken to them, and he sees the wagons which Joseph has sent to carry him away, and the spirit of their father Jacob lives;
Wakamwambia maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewambia. Yakobo alipoona mikokoteni Yusufu aliyokuwa amepeleka kuwabeba, roho ya Yakobo baba yao ikafufuka.
28 and Israel says, “Enough! My son Joseph [is] yet alive; I go and see him before I die.”
Israeli akasema, “Inatosha. Yusufu mwanangu yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”