< Genesis 3 >

1 And the serpent has been cunning above every beast of the field which YHWH God has made, and he says to the woman, “Is it true that God has said, You do not eat from every tree of the garden?”
Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini ambao Bwana Mungu aliwafanya. Nyoka akamwambia mwanamke, “Ati kweli Mungu alisema, ‘Kamwe msile matunda ya mti wowote wa bustanini’?”
2 And the woman says to the serpent, “From the fruit of the trees of the garden we eat,
Mwanamke akamjibu nyoka, “Tunaweza kula matunda ya miti iliyoko bustanini,
3 but from the fruit of the tree which [is] in the midst of the garden, God has said, You do not eat of it, nor touch it, lest you die.”
lakini Mungu alisema, ‘Kamwe msile tunda la mti ulio katikati ya bustani, wala kuugusa, la sivyo mtakufa.’”
4 And the serpent says to the woman, “Dying, you do not die,
Lakini nyoka akamwambia mwanamke, “Hakika hamtakufa.
5 for God knows that in the day of your eating of it—your eyes have been opened, and you have been as God, knowing good and evil.”
Kwa maana Mungu anajua ya kuwa wakati mtakapoyala, macho yenu yatafumbuliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
6 And the woman sees that the tree [is] good for food, and that it [is] pleasant to the eyes, and the tree is desirable to make [one] wise, and she takes from its fruit and eats, and also gives [some] to her husband with her, and he eats;
Mwanamke alipoona ya kuwa tunda la mti huo lilikuwa zuri kwa chakula na la kupendeza macho, tena linatamanika kwa kujipatia hekima, basi akachuma katika matunda yake, akala, pia akampa mumewe, aliyekuwa pamoja naye, naye akala.
7 and the eyes of them both are opened, and they know that they [are] naked, and they sew fig-leaves, and make girdles for themselves.
Ndipo macho yao wote wawili yakafumbuliwa, wakajiona kwamba walikuwa uchi; hivyo wakashona majani ya mtini, wakajifunika.
8 And they hear the sound of YHWH God walking up and down in the garden at the breeze of the day, and the man and his wife hide themselves from the face of YHWH God in the midst of the trees of the garden.
Ndipo yule mwanaume na mkewe, waliposikia sauti ya Bwana Mungu alipokuwa akitembea bustanini jioni, wakajificha kutoka mbele za Bwana Mungu katikati ya miti ya bustani.
9 And YHWH God calls to the man and says to him, “Where [are] you?”
Lakini Bwana Mungu akamwita Adamu, “Uko wapi?”
10 And he says, “I have heard Your sound in the garden, and I am afraid, for I am naked, and I hide myself.”
Naye akajibu, “Nilikusikia katika bustani nikaogopa kwa sababu nilikuwa uchi, hivyo nikajificha.”
11 And He says, “Who has declared to you that you [are] naked? Have you eaten from the tree of which I have commanded you not to eat?”
Mungu akamuuliza, “Ni nani aliyekuambia ya kuwa ulikuwa uchi? Je, umekula matunda ya mti niliokuamuru usile?”
12 And the man says, “The woman whom You placed with me—she has given to me from the tree, and I eat.”
Adamu akasema, “Huyu mwanamke uliyenipa awe pamoja nami alinipa sehemu ya tunda kutoka kwenye huo mti, nami nikala.”
13 And YHWH God says to the woman, “What [is] this you have done?” And the woman says, “The serpent has caused me to forget, and I eat.”
Ndipo Bwana Mungu akamuuliza mwanamke, “Ni nini hili ambalo umelifanya?” Mwanamke akajibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”
14 And YHWH God says to the serpent, “Because you have done this, cursed [are] you above all the livestock, and above every beast of the field: on your belly you go, and dust you eat, [for] all days of your life;
Hivyo Bwana Mungu akamwambia nyoka, “Kwa kuwa umefanya hili, “Umelaaniwa kuliko wanyama wote wa kufugwa na wa porini! Utatambaa kwa tumbo lako na kula mavumbi siku zote za maisha yako.
15 and I put enmity between you and the woman, and between your seed and her Seed; He bruises your head, and you bruise His heel.”
Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, yeye atakuponda kichwa, nawe utamuuma kisigino.”
16 To the woman He said, “Multiplying I multiply your sorrow and your conception; you will bear children in sorrow, and your desire [is] toward your Man [[or husband]], and He [[or he]] will rule over you.”
Kwa mwanamke akasema, “Nitakuzidishia sana utungu wakati wa kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto. Tamaa yako itakuwa kwa mumeo naye atakutawala.”
17 And to the man He said, “Because you have listened to the voice of your wife, and eat from the tree concerning which I have charged you, saying, You do not eat of it, cursed [is] the ground on your account; in sorrow you eat of it [for] all days of your life,
Kwa Adamu akasema, “Kwa sababu umemsikiliza mke wako na ukala kutoka kwenye mti niliokuamuru, ‘Msile tunda lake,’ “Ardhi imelaaniwa kwa sababu yako, kwa kazi ngumu utakula chakula kitokacho humo siku zote za maisha yako.
18 and it brings forth thorn and bramble for you, and you have eaten the herb of the field;
Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako, nawe utakula mimea ya shambani.
19 by the sweat of your face you eat bread until your return to the ground, for you have been taken out of it, for dust you [are], and to dust you return.”
Kwa jasho la uso wako utakula chakula chako hadi utakaporudi ardhini, kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo, kwa kuwa wewe u mavumbi na mavumbini wewe utarudi.”
20 And the man calls his wife’s name Eve, for she has been mother of all living.
Adamu akamwita mkewe Eva, kwa kuwa atakuwa mama wa wote walio hai.
21 And YHWH God makes coats of skin [for] the man and his wife, and clothes them.
Bwana Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
22 And YHWH God says, “Behold, the man was as one of Us, as to the knowledge of good and evil; and now, lest he send forth his hand, and has also taken from the Tree of Life, and eaten, and lived for all time.”
Kisha Bwana Mungu akasema, “Sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya. Sharti asiruhusiwe kunyoosha mkono wake na kuchuma pia kutoka mti wa uzima akala, naye akaishi milele.”
23 YHWH God sends him forth from the Garden of Eden to serve the ground from which he has been taken;
Hivyo Bwana Mungu akamfukuzia mbali kutoka Bustani ya Edeni, akalime ardhi ambamo alitolewa.
24 indeed, He casts out the man, and causes the cherubim to dwell at the east of the Garden of Eden with the sword of flame whirling around to guard the way of the Tree of Life.
Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.

< Genesis 3 >