< Genesis 2 >

1 And the heavens and the earth are completed, and all their host;
Kisha mbingu na nchi zilimalizika, na viumbe hai vyote vilivyo jaza mbingu na nchi.
2 and God completes by the seventh day His work which He has made, and ceases by the seventh day from all His work which He has made.
Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake ambayo aliifanya, na kwa hiyo alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote.
3 And God blesses the seventh day, and sanctifies it, for in it He has ceased from all His work which God had created for making.
Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji.
4 These [are] the generations of the heavens and of the earth in their being created, in the day of YHWH God’s making the earth and the heavens;
Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi, wakati vilipoumbwa, katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba nchi na mbingu.
5 and no shrub of the field is yet in the earth, and no herb of the field yet sprouts, for YHWH God has not rained on the earth, and there is not a man to serve the ground,
Hapakuwa na msitu wa shambani uliokuwa katika nchi, na hapakuwa na mmea wa shambani uliokuwa umechipuka, kwa kuwa Yahwe Mungu alikuwa hajasababisha mvua kunyesha juu ya nchi, na hapakuwa na mtu wa kulima ardhi.
6 and a mist goes up from the earth, and has watered the whole face of the ground.
Lakini ukungu uliinuka juu kutoka kwenye nchi na kuutia maji uso wote wa ardhi.
7 And YHWH God forms the man—dust from the ground, and breathes into his nostrils breath of life, and the man becomes a living creature.
Yahwe Mungu aliumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, na akampulizia puani pumzi ya uhai, na mtu akawa kiumbe hai.
8 And YHWH God plants a garden in Eden, at the east, and He sets there the man whom He has formed;
Yahwe Mungu aliotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, na pale akamuweka mtu ambaye alimuumba.
9 and YHWH God causes to sprout from the ground every tree desirable for appearance, and good for food, and the Tree of Life in the midst of the garden, and the Tree of the Knowledge of Good and Evil.
Kutoka ardhini Yahwe Mungu alifanya kila mti uote ambao unapendeza na ni mzuri kwa chakula. Hii ni pamoja na mti wa uzima ambao ulikuwa katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
10 And a river is going out from Eden to water the garden, and from there it is parted, and has become four chief [rivers];
Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
11 the name of the first [is] Pison, it [is] that which is surrounding the whole land of Havilah where the gold [is],
Jina la ule wa kwanza ni Pishoni. Huu ni ule ambao unatiririka kupitia nchi yote ya Havila, ambapo kuna dhahabu.
12 and the gold of that land [is] good; the bdellium and the shoham stone [are] there;
Dhahabu ya inchi ile ni nzuri. pia kuna bedola na jiwe shohamu.
13 and the name of the second river [is] Gihon, it [is] that which is surrounding the whole land of Cush;
Jina la mto wa pili ni Gihoni. Huu unatiririka kupitia nchi yote ya kushi.
14 and the name of the third river [is] Hiddekel, it [is] that which is going east of Asshur; and the fourth river is the Euphrates.
Jina la mto wa tatu ni Hidekeli, ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
15 And YHWH God takes the man, and causes him to rest in the Garden of Eden, to serve it and to keep it.
Yahwe Mungu alimtwaa mtu na kumweka ndani ya bustani ya Edeni kuilima na kuitunza.
16 And YHWH God lays a charge on the man, saying, “From every tree of the garden eating you eat;
Yahwe Mungu alimuagiza mtu akisema, “kutoka kwenye kila mti bustanini waweza kula kwa uhuru.
17 but from the Tree of the Knowledge of Good and Evil, you do not eat from it, for in the day of your eating from it—dying you die.”
Lakini kutoka kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa kuwa siku utakayo kula kutoka katika mti huo, utakufa hakika.”
18 And YHWH God says, “[It is] not good for the man to be alone; I make him a helper as his counterpart.”
Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
19 And YHWH God forms from the ground every beast of the field, and every bird of the heavens, and brings [them] to the man, to see what he calls it; and whatever the man calls a living creature, that [is] its name.
Kutoka ardhini Yahwe Mungu akafanya kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani. Kisha akawaleta kwa mtu huyu aone angewapatia majina gani. Jina ambalo mtu huyu alimwita kila kiumbe hai, hili ndilo lilikuwa jina lake.
20 And the man calls names to all the livestock, and to bird of the heavens, and to every beast of the field; but for man a helper has not been found as his counterpart.
Mtu huyu akawapatia majina wanyama wote, ndege wote wa angani, na kila mnyama wa mwitu. Lakini kwa mtu mwenyewe hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye.
21 And YHWH God causes a deep sleep to fall on the man, and he sleeps, and He takes one of his ribs, and closes up flesh in its stead.
Yahwe Mungu akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu, kwa hiyo mtu huyu akalala. Yahwe Mungu akatwaa moja ya mbavu za mtu huyu na akapafunika pale alipo chukua ubavu.
22 And YHWH God builds up the rib which He has taken out of the man into a woman, and brings her to the man;
Kwa ubavu ambao Yahwe Mungu alichukua toka kwa mtu huyu, akafanya mwanamke na akamleta kwa mtu huyu.
23 and the man says, “This at last! Bone of my bone, and flesh of my flesh!” For this is called Woman, for this has been taken from Man;
Mwanaume akasema, “kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu. ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume.
24 therefore a man leaves his father and his mother, and has cleaved to his wife, and they have become one flesh.
Kwa hiyo mwanaume atawaacha baba yake na mama yake, ataungamanika na mke wake, na watakuwa mwili mmoja.
25 And both of them are naked, the man and his wife, and they are not ashamed of themselves.
Wote wawili walikuwa uchi, mwanaume na mke wake, lakini hawakuona aibu.

< Genesis 2 >