< Galatians 6 >
1 Brothers, even if a man may be overtaken in any trespass, you who [are] spiritual restore such a one in a spirit of meekness, considering yourself—lest you also may be tempted.
Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
2 Bear the burdens of one another, and so fill up the law of the Christ,
Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
3 for if anyone thinks [himself] to be something—being nothing—he deceives himself;
Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
4 and let each one prove his own work, and then he will have the glorying in regard to himself alone, and not in regard to the other,
Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
5 for each one will bear his own burden.
Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
6 And let him who is instructed in the word share with him who is instructing in all good things.
Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
7 Do not be led astray: God is not mocked; for what a man may sow—that he will also reap,
Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
8 because he who is sowing to his own flesh, of the flesh will reap corruption; and he who is sowing to the Spirit, of the Spirit will reap continuous life; (aiōnios )
Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios )
9 and in doing good we should not be weary, for at the proper time we will reap—not desponding;
Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
10 therefore, then, as we have opportunity, may we work the good to all, and especially to those of the household of faith.
Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
11 You see in how large letters I have written to you with my own hand;
Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
12 as many as are willing to make a good appearance in the flesh, these constrain you to be circumcised—only that they may not be persecuted for the Cross of the Christ,
Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
13 for neither do those circumcised keep the Law themselves, but they wish you to be circumcised, that they may glory in your flesh.
Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
14 And for me, let it not be—to glory, except in the Cross of our Lord Jesus Christ, through which the world has been crucified to me, and I to the world;
Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
15 for in Christ Jesus neither circumcision avails anything, nor uncircumcision, but a new creation;
Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
16 and as many as walk by this rule—peace on them, and kindness, and on the Israel of God!
Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
17 From now on, let no one give me trouble, for I carry the scars of the Lord Jesus in my body.
Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
18 The grace of our Lord Jesus Christ [is] with your spirit, brothers! Amen.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.