< Ezekiel 36 >
1 “And you, son of man, prophesy to mountains of Israel, and you have said, O mountains of Israel, hear a word of YHWH!
“Na wewe, mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, 'Milima ya Israeli, lisikilizeni neno la Yahwe.
2 Thus said Lord YHWH: Because the enemy said against you, Aha! The high places of old have also become our possession,
Bwana Yahwe asema hivi: Adui amesema kuhusu ninyi, “Aha!” na “Mahala pa juu pa zamani pamekuwa milki yetu.”'
3 therefore, prophesy, and you have said, Thus said Lord YHWH: Because, even because, of desolating, And of swallowing you up from all around, For your being a possession to the remnant of the nations, And you are taken up on the tip of the tongue, And [are] an evil report to the people.
Kwa hiyo tabiri na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu ya ukiwa wenu na kwa sababu mashambulizi yaliyokuja juu yenu kutoka pande zote, mmekuwa milki ya mataifa mengine; mmeambiwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu.
4 Therefore, O mountains of Israel, Hear a word of Lord YHWH! Thus said Lord YHWH, to mountains, and to hills, To streams, and to valleys, And to ruins that [are] desolate, And to cities that are forsaken, That have been for a prey, And for a scorn, to the remnant of the surrounding nations,
Kwa hiyo, milima ya Israeli, sikilizeni neno la Bwana Yahwe: Bwana Yahwe asema hivi kwa milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, mahali palipoharibika kuwa ukiwa na miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kutokuwa huru kwa kutaniwa na mataifa yaliyowazunguka-
5 Therefore, thus said Lord YHWH: Have I not, in the fire of My jealousy, Spoken against the remnant of the nations, And against Edom—all of it, Who gave My land to themselves for a possession, With the joy of the whole heart—with despite of soul, For the sake of casting it out for a prey?
kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Hakika nimeongea katika moto wa hasira yangu juu ya mataifa meningine, juu ya Edemu na wote waliochukua nchi yangu kwa ajili yao wenyewe kama milki, dhidi ya wale walikuwa na furaha yote katika mioyo yao na dharau katika roho zao, kama walivyoitwaa nchi yangu kwamba wangeweza kudai nchi za malisho kwa ajili yao.
6 Therefore, prophesy concerning the ground of Israel, And you have said to mountains, and to hills, To streams, and to valleys, Thus said Lord YHWH: Behold, I, in My jealousy and in My fury, have spoken, Because you have borne the shame of nations.
Kwa hiyo, tabiri kwa nchi ya Israeli na sema kwa milima na vilima, hata kwenye mifereji na mabonde, Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Katika ghadhabu yangu na hasira yangu nasema hivi kwa sababu mmechukua fedheha za mataifa.
7 Therefore, thus said Lord YHWH: I have lifted up My hand, Do the nations who [are] surrounding you not bear their own shame?
Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Mimi mwenyewe nitainua mkono wangu kuapa kwamba mataifa yanayowazunguka yamkini yatawabebea aibu yao wenyewe.
8 And you, O mountains of Israel, You give out your branch, And you bear your fruits for My people Israel, For they have drawn near to come.
Lakini ninyi, milima ya Israeli, mtachipuza matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa kuwa watarudi kwenu.
9 For behold, I [am] for you, and have turned to you, And you have been tilled and sown.
Maana tazama, nipo kwa ajili yenu, na kuwachukulia kwa fadhili; mtalimwa na kupandwa mbegu.
10 And I have multiplied men on you, All the house of Israel—all of it, And the cities have been inhabited, And the ruins are built.
Hivyo nitawaongeza juu ya milima yenu watu katika nyumba ya Israeli, yote. Miji itakaa na palipoharibiwa kujengwa.
11 And I have multiplied man and beast on you, And they have multiplied and been fruitful, And I have caused you to dwell according to your former states, And I have done better than at your beginnings, And you have known that I [am] YHWH.
Nitaongeza mtu na wanyama juu yenu milima ili kwamba itaongezeka na kuzaa. Kisha nitawafanya kuishi kama mlivyokuwa, na nitawafanya kustawi zaidi kuliko mlivyokuwa zamani, kwa kuwa mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
12 And I have caused man to walk over you—My people Israel, And they possess you, and you have been their inheritance, And you no longer add to bereave them.
Nitawaleta watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watakumiliki, na utakuwa urithi wao, na hutasababisha tena watoto wao kufa.
13 Thus said Lord YHWH: Because they are saying to you, You [are] a devourer of men, And you have been a bereaver of your nations,
Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu wanakwambia, “Wewe unakula watu, na watoto wa nchi yako wamekufa,”
14 Therefore, you no longer devour man, And you do not cause your nations to stumble anymore, A declaration of Lord YHWH.
kwa hiyo hautawala watu wangu tena, na hutalifanya tena taifa lako kuomboleza vifo vyao. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 And I do not proclaim the shame of the nations to you anymore, And you no longer bear the reproach of peoples, And your nations do not stumble anymore, A declaration of Lord YHWH.”
Wala sintokuruhusu kusikiliza fedhiha za mataifa tena; hautachukua tena aibu ya watu au kufanya taifa lako kuanguka-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
16 And there is a word of YHWH to me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
17 “Son of man, The house of Israel are dwelling on their land, And they defile it by their way and by their doings, Their way has been as the uncleanness of a separated one before Me.
“Mwanadamu, wakati nyumba ya Israeli walipoikalia nchi yao, waliinajisi kwa njia zao na matendo yao. Njia zao zilikuwa kama uchafu wa hedhi ya mwanamke mbele yangu.
18 And I pour out My fury on them For the blood that they shed on the land, And they have defiled it with their idols.
Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa ajili ya damu ambayo waliyoimwaga juu ya nchi na kwa ajili ya uchafu wa hiyo kwa sanamu zao.
19 And I scatter them among nations, And they are spread through lands, According to their way, and according to their doings, I have judged them.
Nimewatawanya miongoni mwa mataifa; walitawanyika katika nchi nyingi. Nimewahukumu kulingana na njia zao na matendo yao.
20 And one goes to the nations to where they have gone, And they defile My holy Name by saying to them, These [are] the people of YHWH, And they have gone forth from His land.
Kisha wakaenda kati ya mataifa, na popote walipoenda, walilitukana jina langu takatifu wakati watu waliwasema, 'Je! hawa kweli ni watu wa Yahwe? Kwa kuwa wamefukuzwa nje ya nchi yake.
21 And I have pity on My holy Name, That the house of Israel has defiled Among the nations to where they have gone in.
Lakini nilikuwa na huruma kwa ajili ya jina langu takatifu ambalo nyumba ya Israeli walilinajisi miongoni mwa mataifa, walipoenda huko.
22 Therefore, say to the house of Israel, Thus said Lord YHWH: I am not working for your sake, O house of Israel, but for My holy Name That you have defiled Among the nations to where you have gone in.
Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Sifanyi haya kwa ajili yenu, nyumba ya Israeli, lakini jina langu, mlilolitukana miongoni mwa mataifa kila sehemu mlipoenda.
23 And I have sanctified My great Name, That is profaned among the nations, That you have defiled in your midst, And the nations have known that I [am] YHWH, A declaration of Lord YHWH, In My being sanctified in you before your eyes.
Kwa kuwa nitalifanya jina langu kuu kuwa takatifu, mlilolitukana miongoni mwa mataifa-katikati ya mataifa, mmelitukana. Kisha mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe-asemavyo-wakati mtakapoona kwamba mimi ni mtakatifu.
24 And I have taken you out of the nations, And have gathered you out of all the lands, And I have brought you into your land,
Nitawachukua kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka kila nchi, na nitawaleta hata nchi yenu.
25 And I have sprinkled clean water over you, And you have been clean; I cleanse you from all your uncleannesses, And from all your idols.
Kisha nitanyunyiza maji masafi juu yenu ili muwe wasafi kutoka kwenye uchafu wote, na nitawasafisha kutoka sanamu zenu zenu.
26 And I have given a new heart to you, And I give a new spirit in your midst, And I have turned aside the heart of stone out of your flesh, And I have given a heart of flesh to you.
Nitawapatia moyo mpya na roho mpya sehemu zenu za ndani, na nitautoa moyo wa jiwe kutoka kwenye nyama zenu. Kwa kuwa nitawapatia moyo wa nyama.
27 And I give My Spirit in your midst, And I have done this, so that you walk in My statutes, And you keep My judgments, and have done them.
Nitaiweka Roho yangu ndani yenu na kuwawezesha kutembea katika sheria zangu na kuziweka hukumu zangu, hivyo mtazitenda.
28 And you have dwelt in the land that I have given to your fathers, And you have been to Me for a people, And I am to you for God.
Kisha mtakaa katika nchi niliyowapa babu zenu; mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
29 And I have saved you from all your uncleannesses, And I have called to the grain, and multiplied it, And I have put no famine on you.
Kwa kuwa nitawaokoa kutokana na uchafu wenu wote. Nitaita ngano kuiongeza. Sitaweka tena njaa juu yenu.
30 And I have multiplied the fruit of the tree, And the increase of the field, So that you do not receive a reproach of famine among nations anymore.
Nitaongeza tunda la mti na kuzalisha kwenye mashamba ili kwamba msichukue tena aibu ya njaa juu ya mataifa.
31 And you have remembered your ways that [are] evil, And your doings that [are] not good, And have been loathsome in your own faces, For your iniquities, and for your abominations.
Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya na matendo yenu ambayo hayakuwa mazuri, na mtaonyesha chuki kwenye nyuso zenu kwa sababu ya dhambi zenu na matendo yenu maovu.
32 I am not working for your sake, A declaration of Lord YHWH, Be it known to you, Be ashamed and confounded, because of your ways, O house of Israel.
Sifanyi hili kwa ajili yenu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-ijulikane kwenu. Hivyo tahayarikeni na kufadhaika kwa sababu ya njia zenu, nyumba ya Israeli.
33 Thus said Lord YHWH: In the day of My cleansing you from all your iniquities, I have caused the cities to be inhabited, And the ruins have been built,
Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyowatakasa kutoka kwenye uovu wenu wote, nitawafanya miji ikaliwe na kuzijenga sehemu zilizoharibiwa.
34 And the desolate land is tilled, Instead of which it was a desolation before the eyes of everyone passing by,
Kwa kuwa mtailima nchi iliyoharibiwa hadi itakapoonekana haijaaharibika mbele za macho ya wote wapitao karibu.
35 And they have said: This land, that was desolated, Has been as the Garden of Eden, And the cities—the dried up, And the desolated, and the broken down, [And the] fortified have remained.
Kisha watasema, “Hii nchi ilikuwa ukiwa, lakini imekuwa kama bustani ya Edeni; miji ya ukiwa na isiyo na wakaaji iliyo magofu ambayo ilibomolewa sasa inakaliwa.
36 And the nations who are left around you have known That I, YHWH, have built the thrown down, I have planted the desolated: I, YHWH, have spoken, and I have done [it].
Kisha mataifa mengine waliowazunguka watajua yakwamba mimi ni Yahwe, kwamba nimejenga palipokuwa pameharibiwa na kuipanda mbegu sehemu iliyokuwa ukiwa.
37 Thus said Lord YHWH: Yet this I am inquired of by the house of Israel to do for them: I multiply them as a flock of men,
Bwana Yahwe asema hivi: Tena nitaulizwa na nyumba ya Israeli kufanya hivi kwa ajili yao, kuwaongeza kama kundi la watu.
38 As a flock of holy ones, as a flock of Jerusalem, In her appointed times, So the dried up cities are full of flocks of man, And they have known that I [am] YHWH!”
Kama kundi lililotengwa kwa ajili ya sadaka, kama kundi katika Yerusalimu katika sikukuu yake iliyoteuliwa, hivyo miji itaharibiwa kwa kujazwa na makundi ya watu na watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'