< Ezekiel 30 >
1 And there is a word of YHWH to me, saying,
Neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 “Son of man, prophesy, and you have said, Thus said Lord YHWH: Howl, Aah! For the day!
“Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
3 For a day [is] near, a day [is] near to YHWH! It is a time of cloud [over] the nations.
siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
4 And a sword has come into Egypt, And there has been great pain in Cush, In the falling of the wounded in Egypt, And they have taken its store, And its foundations have been broken down.
Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
5 Cush, and Phut, and Lud, and all the mixture, and Chub, And the sons of the land of the covenant fall by sword with them,
Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
6 Thus said YHWH: And those supporting Egypt have fallen, And the arrogance of her strength has come down, From Migdol to Syene, they fall by sword in her, A declaration of Lord YHWH.
Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
7 And they have been desolated in the midst of desolate lands, And its cities are in the midst of cities [that are] laid waste.
Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
8 And they have known that I [am] YHWH, In My giving fire against Egypt, And all her helpers have been broken.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
9 In that day messengers go forth from before Me in ships, To trouble confident Cush, And there has been great pain among them, As the day of Egypt, for behold, it has come.
Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
10 Thus said Lord YHWH: I have caused the multitude of Egypt to cease, By the hand of Nebuchadnezzar king of Babylon,
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
11 He and his people with him—the terrible of nations, Are brought in to destroy the land, And they have drawn their swords against Egypt, And have filled the land [with] the wounded.
Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
12 And I have made floods a dry place, And I have sold the land into the hand of evildoers, And I have made the land desolate, And its fullness, by the hand of strangers, I, YHWH, have spoken.
Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
13 Thus said Lord YHWH: And I have destroyed idols, And caused vain things to cease from Noph, And there is no longer a prince of the land of Egypt, And I give fear in the land of Egypt.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
14 And I have made Pathros desolate, And I have given fire against Zoan, And I have done judgments in No,
Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
15 And I have poured out My fury on Sin, the stronghold of Egypt, And I have cut off the multitude of No.
Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
16 And I have given fire against Egypt, Sin is greatly pained, and No is to be broken, And Noph has daily distresses.
Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
17 The youths of Aven and Pi-Beseth fall by sword, And these go into captivity.
Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
18 And the day has been dark in Tehaphnehes, In My breaking the yokes of Egypt there, And the excellence of her strength has ceased in her, Her! A cloud covers her, And her daughters go into captivity.
Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
19 And I have done judgments in Egypt, And they have known that I [am] YHWH.”
Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
20 And it comes to pass, in the eleventh year, in the first [month], on the seventh of the month, a word of YHWH has been to me, saying, “Son of man,
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
21 I have broken the arm of Pharaoh, king of Egypt, And behold, it has not been bound up to give healing, To put a bandage to bind it, To strengthen it—to lay hold on the sword.
“Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
22 Therefore, thus said Lord YHWH: Behold, I [am] against Pharaoh, king of Egypt, And I have broken his arms, The strong one and the broken one, And have caused the sword to fall out of his hand,
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
23 And I have scattered the Egyptians among nations, And have spread them through lands,
Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
24 And I have strengthened the arms of the king of Babylon, And have given My sword into his hand, And I have broken the arms of Pharaoh, And he has groaned the groans of a pierced one—before him.
Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
25 And I have strengthened the arms of the king of Babylon, And the arms of Pharaoh fall down, And they have known that I [am] YHWH, In My giving My sword into the hand of the king of Babylon, And he has stretched it out toward the land of Egypt.
Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
26 And I have scattered the Egyptians among nations, And I have spread them through lands, And they have known that I [am] YHWH!”
Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'