< Ezekiel 21 >

1 And there is a word of YHWH to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “Son of man, set your face toward Jerusalem, and prophesy to the holy places, and prophesy to the ground of Israel;
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 and you have said to the ground of Israel, Thus said YHWH: Behold, I [am] against you, And have brought out My sword from its scabbard, And have cut off righteous and wicked from you.
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Because that I have cut off righteous and wicked from you, Therefore My sword goes out from its scabbard, To all flesh, from south to north.
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 And all flesh has known that I, YHWH, Have brought out My sword from its scabbard, It does not turn back anymore.
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 And you, son of man, sigh with breaking of loins, indeed, sigh before their eyes with bitterness,
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 and it has come to pass, when they say to you, Why are you sighing? That you have said: Because of the report, for it is coming, And every heart has melted, And all hands have been feeble, And every spirit is weak, And all knees go [as] waters, Behold, it is coming, indeed, it has been, A declaration of Lord YHWH.”
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 And there is a word of YHWH to me, saying,
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 “Son of man, prophesy, and you have said, Thus said YHWH: Say, A sword, a sword is sharpened, and also polished.
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 It is sharpened so as to slaughter a slaughter. It is polished so as to have brightness, Or do we rejoice? It is despising the scepter of My son [as] every tree.
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 And He gives it for polishing, For laying hold of by the hand. It is sharpened—the sword—and polished, To give it into the hand of a slayer.
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Cry and howl, son of man, For it has been among My people, It [is] among all the princes of Israel, My people have been cast to the sword. Therefore strike on your thigh,
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 Because [it is] a trier, And what if it is even despising the scepter? It will not be, a declaration of Lord YHWH.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 And you, son of man, prophesy, And strike hand on hand, And the sword is bent a third time, The sword of the wounded! It [is] the sword of the wounded—the great one, That is entering the inner chamber to them.
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 To melt the heart, and to multiply the ruins, I have set the point of a sword by all their gates. Aah! It is made for brightness, Wrapped up for slaughter.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Take possession of the right, place yourself at the left, To where your face is appointed.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 And I also, I strike My hand on My hand, And have caused My fury to rest; I, YHWH, have spoken.”
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 And there is a word of YHWH to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 “And you, son of man, appoint two ways for yourself, for the coming in of the sword of the king of Babylon; they come forth from one land, both of them. And create a station; create [it] at the top of the way of the city.
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Appoint a way for the coming of the sword, To Rabbath of the sons of Ammon, And to Judah, in fortified Jerusalem.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 For the king of Babylon has stood at the head of the way, At the top of the two ways, to use divination, He has moved lightly with the arrows, He has inquired of the teraphim, He has looked on the liver.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 The divination [for] Jerusalem has been at his right, To place battering-rams, To open the mouth with slaughter, To lift up a voice with shouting, To place battering-rams against the gates, To pour out a mound, to build a fortification.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 And it has been to them as a false divination in their eyes, Who have sworn oaths to them, But he is causing iniquity to be remembered [so they] are caught.
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 Therefore, thus said Lord YHWH: Because of your causing your iniquity to be remembered, In your transgressions being revealed, For your sins being seen, in all your doings, Because of your being remembered, You are caught by the hand.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 And you, wounded, wicked one, Prince of Israel, whose day has come, In the time of the iniquity of the end,
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 Thus said Lord YHWH: Turn aside the turban, and carry away the crown, This—not this—make high the low, And make low the high.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 An overturn, overturn, overturn, I make it, Also this has not been until the coming of Him, Whose [is] the judgment, and I have given it.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 And you, son of man, prophesy, and you have said, Thus said Lord YHWH concerning the sons of Ammon, and concerning their reproach, and you have said: A sword, a sword, open for slaughter, Polished to the utmost for brightness!
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 In seeing a vain thing for you, In divining a lie for you, To put you on the necks of the wounded of the wicked, whose day has come, In the time of the iniquity of the end.
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 Turn [it] back to its scabbard; I judge you In the place where you were produced, In the land of your birth.
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 And I have poured My indignation on you, I blow against you with [the] fire of My wrath, And have given you into the hand of brutish men—craftsmen of destruction.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 You are fuel for the fire, Your blood is in the midst of the land, You are not remembered, For I, YHWH, have spoken!”
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”

< Ezekiel 21 >