< Exodus 7 >
1 And YHWH says to Moses, “See, I have given you [as] a god to Pharaoh, and your brother Aaron is your prophet;
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 you speak all that I command you, and your brother Aaron speaks to Pharaoh, and he has sent the sons of Israel out of his land.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 And I harden the heart of Pharaoh, and have multiplied My signs and My wonders in the land of Egypt,
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 and Pharaoh does not listen, and I have put My hand on Egypt, and have brought out My hosts, My people, the sons of Israel, from the land of Egypt by great judgments;
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 and the Egyptians have known that I [am] YHWH, in My stretching out My hand against Egypt; and I have brought out the sons of Israel from their midst.”
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 And Moses does—Aaron also—as YHWH commanded them; so have they done;
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 and Moses [is] a son of eighty years, and Aaron [is] a son of eighty-three years, in their speaking to Pharaoh.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 And YHWH speaks to Moses and to Aaron, saying,
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 “When Pharaoh speaks to you, saying, Give a wonder for yourselves; then you have said to Aaron, Take your rod and cast [it] before Pharaoh—it becomes a dragon.”
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 And Moses goes in—Aaron also—to Pharaoh, and they do so as YHWH has commanded; and Aaron casts his rod before Pharaoh and before his servants, and it becomes a dragon.
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 And Pharaoh also calls for wise men and for sorcerers; and the enchanters of Egypt, they also, with their [enchanting] flames, do so,
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 and they each cast down his rod, and they become dragons, and the rod of Aaron swallows their rods;
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 and the heart of Pharaoh is strong, and he has not listened to them, as YHWH has spoken.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 And YHWH says to Moses, “The heart of Pharaoh has been hard, he has refused to send the people away;
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 go to Pharaoh in the morning, behold, he is going out to the water, and you have stood to meet him by the edge of the River, and the rod which was turned to a serpent you take in your hand,
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 and you have said to him: YHWH, God of the Hebrews, has sent me to you, saying, Send My people away, and they serve Me in the wilderness; and behold, you have not listened until now.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 Thus said YHWH: By this you know that I [am] YHWH; behold, I am striking with the rod which [is] in my hand, on the waters which [are] in the River, and they have been turned to blood,
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 and the fish that [are] in the River die, and the River has stunk, and the Egyptians have been wearied of drinking waters from the River.”
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 And YHWH says to Moses, “Say to Aaron, Take your rod, and stretch out your hand against the waters of Egypt, against their streams, against their rivers, and against their ponds, and against all their collections of waters; and they are blood—and there has been blood in all the land of Egypt, both in [vessels of] wood, and in [those of] stone.”
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 And Moses and Aaron do so, as YHWH has commanded, and he lifts up [his hand] with the rod, and strikes the waters which [are] in the River, before the eyes of Pharaoh and before the eyes of his servants, and all the waters which [are] in the River are turned to blood,
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 and the fish which [is] in the River has died, and the River stinks, and the Egyptians have not been able to drink water from the River; and the blood is in all the land of Egypt.
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 And the enchanters of Egypt do so with their secrets, and the heart of Pharaoh is strong, and he has not listened to them, as YHWH has spoken,
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 and Pharaoh turns and goes into his house, and has not set his heart even to this;
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 and all the Egyptians seek water all around the River to drink, for they have not been able to drink of the waters of the River.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 And seven days are completed after YHWH’s striking the River.
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.