< Exodus 35 >
1 And Moses assembles all the congregation of the sons of Israel and says to them, “These [are] the things which YHWH has commanded—to do them:
Musa akawakusanya jamii yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndio mambo Yahweh aliyo waamuru mfanye.
2 [For] six days work is done, and on the seventh day there is a holy [day] for you, a Sabbath of rest to YHWH; any who does work in it is put to death;
Kwa siku sita kazi ya weza fanywa, lakini kwako, siku ya saba lazima iwe siku takatifu, siku ya Sabato ya mapumziko, takatifu kwa Yahweh. Yeyote atakaye fanya kazi hiyo siku lazima auawe.
3 you do not burn a fire in any of your dwellings on the Sabbath day.”
Haupaswi kuwasha moto kwenye nyumba zenu siku ya Sabato.”
4 And Moses speaks to all the congregation of the sons of Israel, saying, “This [is] the thing which YHWH has commanded, saying,
Musa akasema na jamii yote ya Waisraeli, kwa kusema, “Hichi ndicho kitu Yahweh alicho amuru.
5 Take a raised-offering for YHWH from among you; everyone whose heart [is] willing brings it [as] the raised-offering of YHWH: gold, and silver, and bronze,
Chukuwa sadaka kwa ajili ya Yahweh, wote wenye moyo mkunjufu. Leta sadaka kwa Yahweh - dhahabu, fedha, shaba,
6 and blue, and purple, and scarlet, and linen, and goats’ [hair],
buluu, zambarau, sufu nyekundu na kitambaa kizuri; nywele za mbuzi;
7 and rams’ skins made red, and tachashim skins, and shittim wood,
ngozi za kondoo zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za pomboo; na mbao za mshita;
8 and oil for the light, and spices for the anointing oil, and for the spice-incense,
mafuta ya taa kwa pahali patakatifu, viungo vya manukato kwa hayo mafuta ya kutiwa,
9 and shoham stones, and stones for settings, for an ephod, and for a breastplate.
kwa uvumba mzuri na vito vya shohamu na vito vya kutiwa kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani.
10 And all the wise-hearted among you come in, and make all that YHWH has commanded:
Kila mwanaume mwenye ustadi kati yenu aje na afanye kila kitu ambacho Yahweh aliyaamuru —
11 the Dwelling Place, its tent, and its covering, its hooks, and its boards, its bars, its pillars, and its sockets,
hema la kuabudia, na kifuniko chake, na vifungo vyake, na mbao zake, nguzo, na sakafu;
12 the Ark and its poles, the propitiatory covering, and the veil of the covering,
pia sanduku na nguzo zake, kiti cha rehema, na pazia la kusitiri.
13 the table and its poles, and all its vessels, and the Bread of the Presentation,
Walileta meza na miguu yake, vyombo vyake vyote, na mkate wa wonyesho;
14 and the lampstand for the light, and its vessels, and its lamps, and the oil for the light,
kinara cha taa, vyombo vyake, taa, na mafuta ya zile taa;
15 and the altar of incense, and its poles, and the anointing oil, and the spice-incense, and the covering of the opening at the opening of the Dwelling Place,
ile madhabahu ya uvumba na nguzo zake, mafuta ya upako na uvumba ulitiwa maukato; kishikizo cha mwingilio wa hema ya kuabudia;
16 the altar of burnt-offering and the bronze grate which it has, its poles, and all its vessels, the laver and its base,
madhabahu ya sadaka ya kuteketeza na kitunzi cha shaba na nguzo na vyombo; na ile beseni kubwa na sakafu yake.
17 the hangings of the court, its pillars, and their sockets, and the covering of the gate of the court,
Walileta vishikizo kwa ajili ya nyuani na nguzo zake na sakafu yake, na pazia kwa ajili mwingilio wa nyauni;
18 the pins of the Dwelling Place, and the pins of the court, and their cords,
na ile misumari ya hema la kuabudia na nyuani, pamoja na kamba zake.
19 the colored garments, to do service in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons to act as priest in.”
Walileta mavazi yaliyofumwa kutumikia sehemu takatifu, mavazi takatifu ya Aruni kuhani na wanae, kwa wao kutumika kama makuhani.”
20 And all the congregation of the sons of Israel go out from the presence of Moses,
Kisha makabila yote ya Israeli yakaondoka na kwenda kutoka uweponi mwa Musa.
21 and they come in—every man whom his heart has lifted up, and everyone whom his spirit has made willing—they have brought in the raised-offering of YHWH for the work of the Tent of Meeting, and for all its service, and for the holy garments.
Kila mtu moyo wake ulimchochea na aliye andaliwa na roho yake alikuja na kuleta sadaka kwa Yahweh kwa matengenezo ya hema ya kuabudia, kwa vitu vyote kwajili ya huduma ndani yake, na kwa vazi takatifu.
22 And they come in—the men with the women—every willing-hearted one—they have brought in nose-ring, and earring, and seal-ring, and necklace, all golden goods, even everyone who has waved a wave-offering of gold to YHWH.
Walikuja, wote wanaume kwa wanawake, wote waliokuwa na moyo wa utayari. Walileta madini, hereni, pete, na vitu vya thamani, vitu vyote tofauti vyenye madini ya dhahabu. Waliwasilisha sadaka za dhahabu kama sadaka ya kupunga kwa Yahweh.
23 And every man with whom has been found blue, and purple, and scarlet, and linen, and goats’ [hair], and rams’ skins made red, and tachashim skins, have brought [them] in;
Kila mmoja alikuwa na sufu ya buluu, dhambarau, au nyekundu, nguo nzuri, singa za mbuzi, ngozi za kondoo zilizobadili kuwa nyekundu, na ngozi ya pomboo walivileta.
24 everyone lifting up a raised-offering of silver and bronze has brought in the raised-offering of YHWH; and everyone with whom has been found shittim wood for any work of the service brought [it] in.
kila mmoja alitengeneza sadaka ya fedha au shaba walizileta kama sadaka kwa Yahweh, na kila mmoja aliyekuwa na mti wa mshita kwa matumizi ya kazi aliuleta.
25 And every wise-hearted woman has spun with her hands, and they bring in yarn—of the blue, and the purple, [and] the scarlet—and the linen;
kila mwanamke mwenye ustadi walisokota sufu kwa mikono yao na walileta sufu walizosokota za buluu, dhambarau, au sufu nyekundu, au nguo nzuri.
26 and all the women whose heart has lifted them up in wisdom, have spun the goats’ [hair].
Wanawake wote wenye mioyo iliyochochewa na walio na ustadi walisokota singa za mbuzi.
27 And the princes have brought in the shoham stones, and the stones for settings, for the ephod, and for the breastplate,
Viongozi walileta mawe ya shohamu na mawe mengine kwaajili ya kuwekwa kwenye hiyo naivera na hicho kifuko cha kifuani;
28 and the spices, and the oil for the light, and for the anointing oil, and for the spice-incense;
walileta viungo na mafuta kwaajili ya taa, kwa mafuta ya upako, na kwa uvumba wa manukato.
29 every man and woman of the sons of Israel (whom their heart has made willing to bring in for all the work which YHWH commanded to be done by the hand of Moses) brought in a willing-offering to YHWH.
Waisraeli walileta sadaka ya hiyari kwa Yahweh; kila mwanaume na mwanamke ambao mioyo yao ilikuwa tayari walileta vifaa kwaajili kazi zote ambazo Yahweh aliamuru kupitia Musa zifanyike.
30 And Moses says to the sons of Israel, “See, YHWH has called Bezaleel, son of Uri, son of Hur, of the tribe of Judah, by name,
Musa alisema kwa waisraeli, “Tazama, Yahweh ameita kwa jina juu ya Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, kutoka kabila la Yuda.
31 and He fills him [with] the Spirit of God, in wisdom, in understanding, and in knowledge, and in all work,
Aliijaza Bezaleli kwa Roho yake, kumpa hekima, uwelewa, na maarifa, kwa aina zote za ujenzi,
32 even to devise inventions to work in gold, and in silver, and in bronze,
kufanya sanaa ya ubunifu na kufanya kazi za dhahabu, shaba, na shaba;
33 and in a carving of stones for settings, and in a carving of wood to work in any work of design.
pia kukata na kupanga mawe na mbao iliochongwa- kufanya kazi za aina zote kwa ubunifu na ujenzi.
34 And He has put [it] in his heart to direct, he and Aholiab, son of Ahisamach, of the tribe of Dan;
Aliiweka kufundisha ndani ya moyo wake, yeye pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, kutoka kabila la Dani.
35 He has filled them with wisdom of heart to do every work, of engraver, and designer, and embroiderer (in blue, and in purple, in scarlet, and in linen), and weaver, who does any work, and of designers of designs.”
Aliwajaza kwa ustadi wa kufanya kazi za aina zote, kufanya kazi ya kama kuchora mawe, kama mwerevu, kama mtia taraza katika nyuzi za rangu ya buluu, dhambarau, na nyekundu na nguo nzuri, na kama washonaji. Walikuwa wachonga mawe wa kazi zote, na walikuwa wabunifu wa sanaa.