< Exodus 2 >
1 And there goes a man of the house of Levi, and he takes the daughter of Levi,
Sasa mwanamme wa kabila la Lawi alimuoa mwanamke Mlawi.
2 and the woman conceives, and bears a son, and she sees him, that he [is] beautiful, and she hides him [for] three months,
Yule mwanamke akapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume. Alipoona ya kuwa alikuwa mtoto mwenye afaya, alimficha kwa miezi mitatu.
3 and she has not been able to hide him anymore, and she takes an ark of rushes for him, and covers it with bitumen and with pitch, and puts the boy in it, and puts [it] in the weeds by the edge of the River;
Lakini alipokuwa hawezi kuendelea kumficha tena, alichukua kikapu cha manyasi akakipaka sifa na lami. Akamtia mtoto ndani yake na kukiweka juu ya maji katika majani kando ya mto.
4 and his sister stations herself far off, to know what is done to him.
Dada yake akasimama kwa mbali ili ajue yatakayompata.
5 And a daughter of Pharaoh comes down to bathe at the River, and her girls are walking by the side of the River, and she sees the ark in the midst of the weeds, and sends her handmaid, and she takes it,
Binti Farao akashuka kuoga mtoni wakati vijakazi wake wakitembea kando ya mto. Naye akaona kile kikapu katika majani na akamtuma kijakazi wake kwenda kukileta.
6 and opens, and sees him—the boy, and behold, a child weeping! And she has pity on him and says, “This is [one] of the Hebrews’ children.”
Alipokifungua, aliomwona mtoto. Tazama, mtoto alikuwa analia. Alimhurumia na kusema, “Bila shaka huyu ni mmoja wapo wa watoto wa Waebrania.”
7 And his sister says to the daughter of Pharaoh, “Do I go? When I have called a suckling woman of the Hebrews for you, then she suckles the boy for you”;
Basi dada wa yule mtoto akamwambia binti Farao, “Je naweza kwenda kukutafutia mwanamke wa Kiebrania aje akulele mtoto kwa ajili yako?”
8 and the daughter of Pharaoh says to her, “Go”; and the virgin goes, and calls the mother of the boy,
Binti Farao akamwambia, “Nenda.” Hivyo yule binti akaenda na kumwita mama yake yule mtoto.
9 and the daughter of Pharaoh says to her, “Take this boy away, and suckle him for me, and I give your hire”; and the woman takes the boy, and suckles him.
Binti Farao akamwambia mama yake yule mtoto, “Mchukue mtoto huyu ukaninyonyeshee, nami nitakupa posho.” Hivyo yule mwanamke akamchukua mtoto na kumnyonyesha.
10 And the boy grows, and she brings him to the daughter of Pharaoh, and he is to her for a son, and she calls his name Moses, and says, “Because I have drawn him from the water.”
Mtoto alipokuwa mkubwa, akamleta kwa binti Farao, na akawa mtoto wake. Akamwita jina lake Musa akisema, “Kwa sababu nilimtoa katika maji.”
11 And it comes to pass, in those days, that Moses is grown, and he goes out to his brothers, and looks on their burdens, and sees a man, an Egyptian, striking a man, a Hebrew, [one] of his brothers,
Musa alipokuwa mtu mzima, alienda kwa watu wake na kuona kazi ngumu walizokuwa wanafanya. Alimuona Mmisri akimpiga Mwebrania, mmoja wa watu wa jamii yake.
12 and he turns here and there, and sees that there is no man, and strikes the Egyptian, and hides him in the sand.
Aliangalia huku na kule, na alipoona ya kuwa hakuna mtu, alimuua yule mmisri na kuuficha mwili wake katika mchanga.
13 And he goes out on the second day, and behold, two men, Hebrews, are striving, and he says to the wrongdoer, “Why do you strike your neighbor?”
Alienda tena siku iliyofuata, na tazama, Waebrania wawili walikuwa wanapigana. Alimwambia yule aliyekuwa na makosa, “Kwa nini unampigia mwenzako?”
14 And he says, “Who set you for a head and judge over us? Are you saying [it] to slay me as you have slain the Egyptian?” And Moses fears and says, “Surely the thing has been known.”
Lakini yule mtu alisema, “Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi juu yetu? Unataka kuniua na mimi kama ulivyomuua yule mmisri?” Ndipo Musa akaogopa na kusema, “Hakika niliyoyafanya yamejulikana.”
15 And Pharaoh hears of this thing, and seeks to slay Moses, and Moses flees from the face of Pharaoh, and dwells in the land of Midian, and dwells by the well.
Farao aliposikia habari hizi, alijaribu kumuua Musa. Lakini Musa alikimbia na kwenda kuishi katika nchi ya Wamidiani. Kule alikaa chini kando ya mto.
16 And to a priest of Midian [are] seven daughters, and they come and draw, and fill the troughs to water the flock of their father,
Wakati huo kuhani wa Midiani alikuwa na mabinti saba. Walikuja mtoni kuchota maji na kujaza vyombo vyao ili wawanyweshe mifuko ya baba yao.
17 and the shepherds come and drive them away, and Moses arises, and saves them, and waters their flock.
Wachungaji walikuja na kutaka kuwafukuza, lakini Musa alienda kuwasaidia. Kisha akawanywesha mifugo wao.
18 And they come to their father Reuel, and he says, “Why have you hurried to come in today?”
Wale mabinti walipoenda kwa Reueli baba yao, aliwauliza, “Kwa nini mmerudi nyumbani mapema hivi leo?”
19 And they say, “A man, an Egyptian, has delivered us out of the hand of the shepherds, and has also diligently drawn for us, and waters the flock”;
Wakamwambia, “Mmisri mmoja alituokoa dhidi ya wachungaji. Pia alichota maji na kuwanywesha mifugo wetu.”
20 and he says to his daughters, “And where [is] he? Why [is] this [that] you left the man? Call for him, and he eats bread.”
Kisha akawauliza binti zake, “Yu wapi sasa? Kwa nini mlimwacha? Mwiteni ili apate kula chakula pamoja nasi.”
21 And Moses is willing to dwell with the man, and he gives his daughter Zipporah to Moses,
Musa akakubali kukaa na yule mtu ambaye pia alimpa binti yake Zipora ili amuoe.
22 and she bears a son, and he calls his name Gershom, for he said, “I have been a sojourner in a strange land.”
Alizaa mtoto wa kiume, na Musa akamwita jina lake Geshomu; akisema; “Nimekuwa mkazi katika nchi ya ugeni.”
23 And it comes to pass during these many days, that the king of Egypt dies, and the sons of Israel sigh because of the service, and cry, and their cry goes up to God, because of the service;
Muda mrefu baadaye, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli walilalamika kwa sababu ya kazi za utumwa. Walilia kutafuta msaada, na maombi yao yakamfikia Mungu kwa sababu ya mateso yao.
24 and God hears their groaning, and God remembers His covenant with Abraham, with Isaac, and with Jacob;
Mungu aliposikia malalamiko yao, Mungu alikumbuka agano lake na Abrahamu, na Isaka, na Yakobo.
25 and God sees the sons of Israel, and God knows.
Mungu aliwaona Waisraeli na akaielewa hali yao.