< Exodus 11 >

1 And YHWH says to Moses, “One more plague I bring in on Pharaoh and on Egypt, afterward he sends you away from this; when he is sending you away, he surely casts you out from this [place] altogether;
Basi Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Nitaleta pigo moja zaidi kwa Farao na katika nchi ya Misri. Baada ya hilo, atawaacha mwondoke hapa na atakapofanya hivyo, atawafukuza mtoke kabisa.
2 now speak in the ears of the people, and they ask—each man from his neighbor, and each woman from her neighbor—[for] vessels of silver and vessels of gold.”
Waambie watu wote waume kwa wake wawaombe majirani zao vitu vya fedha na vya dhahabu.”
3 And YHWH gives the grace of the people in the eyes of the Egyptians; also the man Moses [is] very great in the land of Egypt, in the eyes of the servants of Pharaoh, and in the eyes of the people.
(Bwana akawafanya Wamisri wawe na moyo wa ukarimu kwa Waisraeli, naye Mose mwenyewe akaheshimiwa sana na maafisa wa Farao na watu wote katika nchi ya Misri.)
4 And Moses says, “Thus said YHWH: About midnight I am going out into the midst of Egypt,
Kwa hiyo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Panapo usiku wa manane Mimi nitapita katika nchi yote ya Misri.
5 and every firstborn in the land of Egypt has died, from the firstborn of Pharaoh who is sitting on his throne, to the firstborn of the maidservant who [is] behind the millstones, and all the firstborn of beasts;
Kila mwanaume kifungua mimba katika Misri atakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Farao, aketiye penye kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mtumwa wa kike, anayesaga nafaka kwa jiwe, pamoja na kila mzaliwa wa kwanza wa mifugo.
6 and there has been a great cry in all the land of Egypt, such as there has not been, and such as there is not again;
Patakuwepo kilio kikubwa katika nchi yote ya Misri, kilio kibaya ambacho hakijakuwepo wala kamwe hakitakuwepo tena.
7 and against all the sons of Israel a dog does not sharpen its tongue, from man even to beast, so that you know that YHWH makes a separation between the Egyptians and Israel.
Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna hata mbwa atakayembwekea mwanadamu wala mnyama yeyote.’ Ndipo mtakapojua kuwa Bwana huweka tofauti kati ya Misri na Israeli.
8 And all these servants of yours have come down to me, and bowed themselves to me, saying, Go out, you and all the people who [are] at your feet; and afterward I go out”; and he goes out from Pharaoh in the heat of anger.
Maafisa hawa wako wote watanijia, wakisujudu mbele yangu, wakisema, ‘Ondoka, wewe pamoja na watu wako wote wanaokufuata!’ Baada ya haya nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa amewaka hasira, akamwacha Farao.
9 And YHWH says to Moses, “Pharaoh does not listen to you, so as to multiply My wonders in the land of Egypt”;
Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Farao atakataa kukusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka katika nchi ya Misri.”
10 and Moses and Aaron have done all these wonders before Pharaoh, and YHWH strengthens Pharaoh’s heart, and he has not sent the sons of Israel out of his land.
Mose na Aroni wakafanya maajabu haya yote mbele ya Farao, lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke katika nchi yake.

< Exodus 11 >