< Esther 5 >
1 And it comes to pass on the third day, that Esther puts on royalty, and stands in the inner-court of the house of the king in front of the house of the king, and the king is sitting on his royal throne, in the royal-house, opposite the opening of the house,
Baada ya siku tatu, Esta akajivika mavazi yake ya kimalkia na akasimama sehemu ya ndani ya ua wa ikulu ya mfalme, mbele ya nyumba ya mfalme. mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi na akitazama mlango wa kuingilia.
2 and it comes to pass, at the king’s seeing Esther the queen standing in the court, she has received grace in his eyes, and the king holds out to Esther the golden scepter that [is] in his hand, and Esther draws near, and touches the top of the scepter.
Mfalme alipomwona malkia Esta alipata kibali kwa mfalme. Alimpa fimbo ya dhahabu mikononi mwa Esta. Hivyo Esta akamsogelea mfalme na kuishika fimbo ya utawala.
3 And the king says to her, “What do you [want], Esther, O queen? And what [is] your request? To the half of the kingdom—and it is given to you.”
Kisha mfalme akamwambia Malkia Esta, “Unahitaji upewe nini? Ombi lako ni lipi? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
4 And Esther says, “If to the king [it be] good, the king comes in, and Haman, today, to the banquet that I have made for him”;
Malkia Esta akamwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, naomba wewe na Hamani muhudhurie leo katika karamu niliyoiandaa kwa ajili yake.”
5 and the king says, “Hurry Haman—to do the word of Esther”; and the king comes in, and Haman, to the banquet that Esther has made.
Mfalme akasema, “Mleteni haraka Hamani sawa sawa na matakwa ya Malkia Esta.” Mfalme pamoja na Hamani wakahuduria katika karamu aliyoandaa malkia Esta.
6 And the king says to Esther, during the banquet of wine, “What [is] your petition? And it is given to you; and what [is] your request? To the half of the kingdom—and it is done.”
Mvinyo ulipohudumiwa katika karamu, mfalme akamuuliza Malkia Esta hitaji lako ni nini? Na ombi lako ni lipi? Utapewa hata nusu ya ufalme.”
7 And Esther answers and says, “My petition and my request [is]:
Esta akajibu mfalme, “Hitaji na ombi langu ni hili,
8 if I have found grace in the eyes of the king, and if to the king [it be] good, to give my petition, and to perform my request, the king comes, and Haman, to the banquet that I make for them, and tomorrow I do according to the word of the king.”
kama ikikupendeza mfalme, kwa kunipa haja yangu na kuheshimu ombi langu, wewe na Hamani muhudhurie tena katika karamu nitakayoiandaa kesho na hapo ndipo nitakapo kuambia haja yangu.
9 And Haman goes forth on that day rejoicing and glad in heart, and at Haman’s seeing Mordecai in the gate of the king, and he has not risen nor moved for him, then is Haman full of fury against Mordecai.
Hamani akaenda nyumbani kwakwe huku akiwa amejawa na furaha moyoni mwake. Lakini alipomwona Modekai katika lango la mfalme, modekai hasimami wala kutetemeka mbele zake, alijawa na ghadhabu kwa ajili ya Modekai.
10 And Haman forces himself, and comes into his house, and sends, and brings in his friends, and his wife Zeresh,
Lakini akajizuia na akaenda nyumbani kwake. Akawaarika marafiki zake wakakusanyika pamoja na Zereshi, mkewe.
11 and Haman recounts to them the glory of his wealth, and the abundance of his sons, and all that with which the king made him great, and with which he lifted him up above the heads and servants of the king.
Hamani akawaeleza juu ya utukufu wa mali na idadi ya watoto aliokuwa nao, na vile alivyo juu kuliko wasimamizi na watumishi wote wa mfalme.
12 And Haman says, “Indeed, Esther the queen brought none in with the king, to the feast that she made, except myself, and also for tomorrow I am called to her, with the king,
Hamani akawambia, “Hata jana Malkia Esta aliandaa karamu kwa ajili ya mfalme na ni mimi tu na mfalme tulio hudhuria katika karamu aliyoiandaa Malkia Esta. Na hata kesho tuna mwaliko mwingine pamoja na mfalme.
13 and all this is not profitable to me, during all the time that I am seeing Mordecai the Jew sitting in the gate of the king.”
Lakini haya yote sio kitu kama Modekai ataendelea kukaa katika lango la mfalme.
14 And his wife Zeresh says to him, and all his friends, “Let them prepare a tree, in height fifty cubits, and in the morning speak to the king, and they hang Mordecai on it, and go in with the king to the banquet rejoicing”; and the thing is good before Haman, and he prepares the tree.
Kisha Zereshi, mkewe Hamani akamwambia Mmewe na rafiki zake wote, “Andaeni mti wenye urefu wa futi hamsini. Na wakati wa ahsubuhi ongea na mfalme ili Modekai atundikwe katika mti huo. Kisha nenda kwa furaha na mfalme katika karamu aliyoiandaa Malkia.